Neo Maema, apewa 'Thank You' na Mamelodi Sundowns, kutua Simba baada ya CHAN

Neo Maema, apewa 'Thank You' na Mamelodi Sundowns, kutua Simba baada ya CHAN

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Nahodha wa Bafana Bafana kwenye CHAN2024, Neo Maema amepewa mkono wa kwaheri na klabu yake ya Mamelodi Sundowns baada ya kuhudumu klabuni hapo kwa miaka minne na kuifungia magoli 13, akisaidia ‘assists’ mengine 14 kwenye mechi 120.

Maema 29, raia wa Afrika Kusini ambaye anatarajiwa kujiunga na Simba Sc baada ya kutamatika kwa michuano ya CHAN2024 ameisaidia Sundowns kushinda Mataji manne ya Ligi Kuu Afrika Kusini, taji moja la Nedbank Cup, taji moja la MTN8, na taji moja la African Football League kwa kipindi cha miaka minne cha utumishi wake klabuni hapo.

1755245144333.png
 
Miaka yote magoli 13 hamna mchezaji humo
Ngoja Scars aje atoe ufafanuzi juu ya huu mtazamo wako! Na isitoshe huyo Maema ni kiungo mshambuliaji.
Miaka minne akiwa Mamelodi amecheza mechi 120, amefunga magoli 13, na ametoa assist 14!
 
Ngoja Scars aje atoe ufafanuzi juu ya huu mtazamo wako! Na isitoshe huyo Maema ni kiungo mshambuliaji.
Miaka minne akiwa Mamelodi amecheza mechi 120, amefunga magoli 13, na ametoa assist 14!
Mechi 120 ni sawa na misimu 4 kwa ligi yetu. Kwa namba hizo ukipiga hesabu kama regular starter ni sawa na kusema alikuwa anamaliza msimu akiwa na magoli 3 na asisst 4

Hapo unazungumzia competition ya namba kwenye timu yenye wachezaji wa daraja la juu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom