NEMC yaifunga hotel ya 'Double Tree'

USTAADHI

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2011
Posts
1,516
Reaction score
136
wana JF

Kwa habari nilizopa hivi punde ni kuwa baraza la mazingira Tanzania (NEMC) limeifunga Hotel ya Double Tree ya jijini Dar es salaam kwa kosa la kutiririsha maji ya kinyesi BAHARI YA HINDI.

>>>>>>>>>Story<<<<<<<<<<<


Na Lulu Mussa na Ali Meja


Waziri wa Nchi wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais &#8211; Mazingira Dk. Terezya Huvisa hii leo ameifungia hotel ya Double Tree ya Jijini Dar es Salaam kutokana na kutiririsha maji taka baharini.

Waziri Huvisa ametoa agizo hilo mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza akiwa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mheshimiwa Charles Kitwanga.

Ziara hiyo ililenga kuona utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa awali na Naibu Waziri Mh. Charles Kitwanga mapema mwezi huu, alipofanya ziara kutembelea viwanda na hoteli zilizo pembezoni mwa bahari kuona mfumo wa maji taka.

Katika ziara hiyo, Hotel ya Double Tree iliagizwa kuwa na mpango wa muda mfupi na wa haraka wa kusitisha utiririshaji wa maji taka baharini ambao mpaka leo hotel hiyo ilikuwa bado haijatekeleza.

Sambamba na hilo na hilo Waziri Huvisa amefuta hati ya ukaguzi wa Mazingira (Environemental Audit) na kuitaka hoteli hiyo kurekebisha mara moja mfumo huo ikiwa ni sambamba na kulipa faini kwa baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC).


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dkt. Terezya Huvisa (katikati) akitoa amri ya kuifunga hotel ya Double Tree kutokana na kutiririsha maji taka baharini. Wa kwanza kushoto ni Bw. Karim Kanji - Mkurugenzi Mkazi wa hotel hiyo.
 
Walisema watafanya ivo km ni kweli bravoo but isiwe danganya toto
 
Double Tree ndo ile ipo pale Masaki karibu na palipokuwa Slipway right?

If this is accurate, then it's a shame that such a seemingly swanky place would do this.
 
hotel ya Double Tree yafungwa jijini Dar kutokana na kutiririsha maji taka baharini.
 
tatizo linaloweza kuwakumba hawa watu wa nemci kwenye nchi hii ya kifisadi ni kwamba ukitenda kazi kwa haki hujuma zinakuwa kubwa sana unaweza kustaajabu hata waziri au mtu yeyote mwenye mslahi na uharibifu huu anatumia cheo chake kuvuruga kazi njema na wakati mwingine kupanga hila za watu kutimuliwa kushikishwa rushwa, kufumaniwa,kila aina ya hujuma
 
kwani hayo maji/mavi yanatakiwa yapelekwe/yatiririshwe kwenda wapi?
 
Jamaa nyuso zimewashuka si haba, chezeiya tiririsha nya weeee!
 
Waziri wa mazingira ameifungia hotel hiyo kwa kukiuka taratibu za mazingira kwa kutiririsha kinyesi baharini(itv habari )
 
Waziri wa mazingira ameifungia hotel hiyo kwa kukiuka taratibu za mazingira kwa kutiririsha kinyesi baharini(itv habari )
Unafiki tu, kwa nini wasifunge mgodi wa north Mara? Tena kule wate wanaathirika sana
 
Aisee! Sasa ajira ndo zitakuwaje hapo?
 
Hivi Tanzania kuna serikali inayofuatilia mambo muhimu kama hayo au majamaa wamegoma kutoa kidogo dogo!
 
Waziri jinga hili! Anajua kinschofanywa na wawekezaji kwenye madini?
 
Hivi lile bomba kubwa linaloingia haharini pale karibu na mjengo wa mkuu wa nchi huwa linapeka nini kule?
 
Si hivyo tu, hiyo hotel imefanya bonge la land reclamation, sijui kama waliruhusiwa.

Lakini hii mikwara si ni ya kutafuta hela ya kipindi hiki cha masikukuu, nina wasiwasi.

Kumbukeni kamcheza ka Karibu Textile na ile mikwara ya Makamba kuvunja shell za kwenye makazi ya watu!
 
Double Tree ndo ile ipo pale Masaki karibu na palipokuwa Slipway right?

If this is accurate, then it's a shame that such a seemingly swanky place would do this.

with Indians onboard, expect anything
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…