yusufummaka
Member
- Apr 7, 2012
- 30
- 20
Mbwa anatabia ya kubwekea kila kitu kinachopita mbile yake hata kama uwezo wa kukikamata hana. Mbwa atambwekea hata chatu wakati akijua hatafua dafu kwa chatu na ataishia kuliwa. Fsi huwa anatabia ya kutoa adhabu ya kujambia vitu (mifupa, mawe) anavyoshindwa kuvitafuna ili kuviachia harufu kama adhabu.
Mh. Ngungulile amejaribu kuibwekea hoja ya mji wa kigamboni bila mafanikio, akaliwa. Maskini sijui alikuwa anafahamu vema alichokuwa anabwekea. Anajua nani yuko nyuma ya Kigamboni? Nini madhumuni yake? kipi kimeshaliwa na kipi bado? Ona sasa, yuko nje ya mjengo. Utapotea kisiasa Mh. ina wenyewe. Najua unajua kubweka lakini bwekea sebuleni tena uvunguni mwa meza usitoke nje utaliwa. Kigamboni "zalongwa mbali zatendwa mbali"
Mh. Ngungulile amejaribu kuibwekea hoja ya mji wa kigamboni bila mafanikio, akaliwa. Maskini sijui alikuwa anafahamu vema alichokuwa anabwekea. Anajua nani yuko nyuma ya Kigamboni? Nini madhumuni yake? kipi kimeshaliwa na kipi bado? Ona sasa, yuko nje ya mjengo. Utapotea kisiasa Mh. ina wenyewe. Najua unajua kubweka lakini bwekea sebuleni tena uvunguni mwa meza usitoke nje utaliwa. Kigamboni "zalongwa mbali zatendwa mbali"