Ndugu zangu waisilamu jifunzeni ya SYRIA, LIBYA na YEMEN. vurugu sio solution mtaonekana wajinga tu

Chilisosi

JF-Expert Member
Oct 19, 2008
3,051
747
kama vurugu ndio solution mbona wenzenu wa Syria ni mwaka sasa wanauana kama kuku lakini hakuna mshindi?
Oneni Libya ghadafi kafa jee mnajua yanayojiri huko sasa?
Msipende kuiga ujinga jifunzeni kwanza sio kuiga tu mnaona sifa hao waarabu kwao kufa siku hizi ni fasheni na nyie mnaiga
 
Ndugu watanzania wenzangu na hasa wale wenye dhamana na nchi yetu, jefunzeni ya TUNISIA , MISRI na RWANDA na mzibe ufa kabla ya kujenga ukuta. Mtachekwa na jamii pale jeshi linapoingia kupigana na raia wasio na hatia wala silaha.
 
Ndugu watanzania wenzangu na hasa wale wenye dhamana na nchi yetu, jefunzeni ya TUNISIA , MISRI na RWANDA na mzibe ufa kabla ya kujenga ukuta. Mtachekwa na jamii pale jeshi linapoingia kupigana na raia wasio na hatia wala silaha.
Waambie mkuu hawa wacheza bao wanaona mchezo wa kuua watu na kuchoma makanisa ni sifa hawajui mwisho wake utakuwaje, wakumbuke kuwa wakristo ndio tuliokamata jeshi
 
Mimi nilifikiri mzima kumbe ni viroba ndo vinaongea.Nyie ndugu zangu wakristo msije mkaleta ya Rwanda au liberia hapa nchini.Kwa hakika mtaisha simnajijua mko 30% ya hii nchi shauri lenu
 
Inaonyesha hujui vurugu za Libya,Tunisia,na Misri chanzo chake, ukitaka sasa hivi vurugu zisije hapa basi ukubali kuolewa na mwanaume mwenzako, au dadako anasagwa na msichana nyumba ya jirani
 
kama vurugu ndio solution mbona wenzenu wa syria ni mwaka sasa wanauana kama kuku lakini hakuna mshindi?
Oneni libya ghadafi kafa jee mnajua yanayojiri huko sasa?
Msipende kuiga ujinga jifunzeni kwanza sio kuiga tu mnaona sifa hao waarabu kwao kufa siku hizi ni fasheni na nyie mnaiga

tatizo la waislamu hawana uwezo wa kuchanganya akili zao na mafundisho ya allah.......msikilize allah sawa lkn hebu jaribuni kuchanganya na akili zenu ndogo
 
kama vurugu ndio solution mbona wenzenu wa Syria ni mwaka sasa wanauana kama kuku lakini hakuna mshindi?
Oneni Libya ghadafi kafa jee mnajua yanayojiri huko sasa?
Msipende kuiga ujinga jifunzeni kwanza sio kuiga tu mnaona sifa hao waarabu kwao kufa siku hizi ni fasheni na nyie mnaiga

Tuwe wakweli, wakristo ndio humu JF washabiki wa kuandika kuwatukana waislimu . Nimefuatilia sana hoja mbali mbali na thread nyingi. Tunasahau kuwa hawa mashabiki hawako huku , wengi wako ulaya na Marekani.
Kukiwaka huku tunaoumia ni sisi kondoo , Mapadri hao wajiitao mitume na Maaskofu ndio wa kwanza kukimbizwa ulaya
 
30% umeitoa wapi na ripoti ya sensa kina sheikh Pondwa waliyokuwa wakitaka kiingizwe kipangele cha dini bado haijatoka!?
 
Waislamu ni wastaarabu sana wanatukanwa sana pamoja na dini yao, wamechomewa kitabu chao huko mwanza,kigoma, znz,kitabu kimekojolewa dsm,humu jf nao wanawatusi sanaa.Ustaarabu wao hata siku mmoja wao hawaja wahi kuchoma kitabu chao na hata kumtusi mtu kupitia imani yake.Naona sasa wameachanza kuchoka kwa sababu sio serikali wala maaskofu wamejitokeza hadharani kupinga na kulaani yote hayo yaliotokea ina maana wanayafurahia hayo.Waaislamu uvumilivu umeanza kuota mbawa na wakiamua nchi hii itakuwa motoni ghafla coz wao hawaogopi kifo.Msijidanganye haya yanayotokea sasa yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na Serikali pamoja na Wakristo.
 
Ningependa ku paste here an Press Conference ya Wanazuoni wa KIISLAM, on Todays TANZANIA DAIMA, It says a lot and its an Honest reconcilatory One. Tufungamane kwa pamoja kuiunga mkono. We should never allow our country to be used as the jumping board to create conflict among its own:

"
Wanazuoni wa Kiislamu waonya
na Asha Bani


amka2.gif
TAASISI ya Masheikh na Wanazuoni wa Kiislam Tanzania imewaasa Watanzania kuzingatia utawala wa sheria na kutii amri za mamlaka zilizoundwa kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Taasisi hiyo, Sheikh Khamis Mataka, alisema kuwa wamelazimika kutoa kauli hiyo kutokana na baadhi ya Waislamu kuwa na ghadhabu na kusababisha uharibifu wa mali za watu wasio na hatia na kuchoma makanisa.
Alisema taasisi hiyo ilifanya mkutano kwa siku mbili kutafakari afya ya jamii kufuatia tukio la kunajisiwa kwa Kuran Tukufu na ghasia zilizotokea Mbagala zilizohusisha kutotii sheria na amri za mamlaka na uchomaji wa makanisa.
Sheikh Mataka aliongeza kuwa sekretarieti yao imetazama suala la vurugu zilizotokea Kariakoo ambapo baadhi ya waumini waliishia mikononi mwa vyombo vya dola na pia waliangalia vurugu za Zanzibar ndipo wakatoa tamko hilo.
Alisema taasisi hiyo imesikitishwa sana na baadhi ya Wasilamu kutumia mikusanyiko isiyo halali kupingana na Jeshi la Polisi chini ya shinikizo la kutaka kuachiwa watuhumiwa waliokuwa wamekamatwa.
Mataka alisema kinachofanyika sasa ni watu kutozingatia mafundisho ya dini kwani yanahimiza utulivu, amani na kuheshimu kila kilichowekwa kwa taratibu na kuwataka viongozi wote wanaohamasisha machafuko kurejea mafunzo hayo kama msingi wa kudumisha amani nchini.
Alibainisha kuwa taasisi hiyo imeshtushwa na baadhi ya matamko ya viongozi wa dini ya Kikristo yanayotaka kuitumia kadhia hii kuutia doa Uislamu na Waislamu na kujenga uhalali wa kuitikisa misingi ya udugu kiasi cha kutamani kuzaliwa Tanzania mpya.
Sheikh Mataka alisisitiza kuwa kauli ya maaskofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) iliyotolewa hivi karibuni ilikuwa na mafumbo na hivyo kuzua hofu.
Hata hivyo alisema kuwa taasisi hiyo imesikitishwa na baadhi ya askari waliotumia vibaya ruhusa ya kutumia nguvu katika kuzima fujo hizo, bila kuzingatia mazingira na maeneo yenye mikusanyiko mikubwa ya watu na shughuli za kiuchumi.
"Taasisi pia inatoa pole kwa Rais wa Zanzibar na Mkuu wa Jeshi la Polisi kufuatia kuuawa kinyama kwa askari asiye na hatia, Saidi Abdulrahman na pia kutokana na vurugu hizo tunatarajia kuitisha kikao cha masheikh na viongozi wa taasisi mbalimbali za Kiislamu ili kutafuta dawa ya tatizo hili," alisema Mataka.
Aliongeza kuwa mbali na kuitisha kikao cha viongozi wa Kiislamu lakini pia taasisi inatarajia kuitisha kikao cha viongozi wa dini mbalimbali ili kujadili miundo bora ya kudumisha amani, utulivu na uhusiano mwema baina ya wanadini kwa misingi ya kila mmoja kumheshimu mwenzake.
Taasisi hiyo pia iliwatahadharisha wanasiasa kujiepusha kwa namna moja au nyingine kubariki vurugu za vikundi vya kidini na jamii kwa ujumla na ikawataka waache kutoa ushawishi wa kujichukulia sheria mikononi na kuhamasisha kutotii amri halali za mamlaka za nchi.
Akijibu swali la waandishi waliotaka kujua endapo angekutana na Sheikh Ponda leo atamshauri nini, alisema atamwambia azingatie Uislamu katika kufanya mambo yake.


 
.Hatukufunzwa.Moja ya nguzo za Imaan za Kiislamu ni kuamini vitabu vya Mwenyezi Mungu yaani.INJIL,ZABUR,FURKAN NA QUR-AN.We will never do that.
Lakini makanisa lazima yachomwe au sio????
 
Waislam wasomi kimya ila wale wa drs la 7 wanapiga mdomo ile mbayaa...ving'asti na unywaji wa kahawa ndo kaz mnayoijua..
 
Lakini makanisa lazima yachomwe au sio????
.La khasha.Tumefika hapa kwa sababu ya serikali kuwa na upendeleo.si shabikii hilo lakini tumekuwa tukiangalia reaction bila yakuangalia tatizo limeanzia wapi.Haya ni matatizo ya muda mrefu na yamekuwa yakifumbiwa macho.Qur an imechomwa Mwanza,Kigoma,Zanzibar,DSM wamekojolea Qur an.Hakuna kiongozi wa Dini alielaani hata serikali ika kaa kimya.Hii inapelekea jamii kukata tamaa na kuamua kujichukulia hatua mkononi.
 
Back
Top Bottom