Ndoa sio mchezo hebu soma hii story

Galacha Maestro

JF-Expert Member
Sep 29, 2011
1,353
2,216
NDOA SIO MCHEZO SOMA STORY HII.

"Mkeo amefariki. Rudi nyumbani kwako haraka sana" Hezron alimwambia Daniel katika simu.

"Mke wangu amekufa? Nini kimetokea? Amekufaje?" Daniel aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa vibaya.

"Daktari amesema ni shinikizo la moyo lililosababishwa na stress kali. Daktari na polisi wapo hapa nyumbani kwako. Njoo haraka" Hezron akaongea kidogo na akakata simu.

Muda anapigiwa simu na Hezron, Daniel alikuwa mtoko na mwanamke mwingine mrembo katika moja ya hoteli kubwa iliyoko maeneo ya Kunduchi. Alikuwa akifurahi nae huku wakinywa vinywaji ghali na chakula cha hadhi ya nyota tano. Lakini baada ya kupokea tu ile simu ya taarifa ya kifo cha mkewe, Daniel alichanganyikiwa, uso wake ukabadilika.

Hezron ni rafiki yake wa karibu.

Daniel akainuka na kuondoka katika ile Hotel akimwacha yule mwanake Mrembo.

"Kuna tatizo gani?" Yule mrembo aliuliza.

"Siwezi kuzungumza" Daniel alijibu na kuondoka haraka.

Daniel akaenda alikopaki gari yake, akaingia, akaiwasha na kukanyaga mafuta, akaiondoa kwa kasi ya ajabu.

Akiwa anaendesha, Daniel akakumbuka jinsi yeye na mkewe anaeambiwa amefariki walivoenda pamoja Showroom ya magari na kununua hilo gari pamoja.

Akiwa anakata kona, akakumbuka jinsi alivyokuwa akimfundisha mkewe kuendesha gari. Hizo zilikua nyakati njema kabisa katika maisha yao ya ndoa.

"Mke wangu amekufa! Kweli mke wangu amekufa! Mungu wangu.." alilia sana huku akiendesha.

Akakumbuka siku ya ndoa yao. Agano waliloliweka pamoja. Akiwa anabadilisha gia, akaangalia vidole vyake asiione pete yake ya ndoa. Pete ya ndoa aliitoa ili kudanganya wanawake wengine kwamba hajaoa.

Daniel akakumbuka ni jinsi gani alivyokuwa akimjibu mkewe hovyo, kwamba anayo kila sababu ya kufurahia maisha na kuponda raha. Akakumbuka maneno ya kuchoma aliyokuwa akimwambia mkewe kwamba yeye amezaa na amezeeka!

"Mke wangu amefariki! Kwanini umefariki Lisa! Kwanini Mungu? Alijiuliza maswali lukuki.

Jibu likamjia. Akakumbuka ni nini Hezron alimwambia. Kwamba mkewe yawezekana amekufa kwa shinikizo la damu kutokana ma stress. Kwa hali hiyo Daniel nimemuua mke wangu.

"Nimemuua mke wangu mwenyewe. Mungu nisamehe..." alijutia huku akiendesha gari kwa kasi.

Majuto ni mjukuu.
 
Hii story pamoja na kwamba ni ya kutunga lakini kuna ukweli. Kuna jamaa mmoja ambaye alileta mchepuko wake nyumbani huku mke wake wa ndoa alikuwepo. Mama aliumia sana na si siku si nyingi mama alikufa kwa presha. Baada ya mke kufa, mchepuko alikuwa na mimba ya yule jamaa by then. Wakati huo naye mchepuko aligongwa na gari akafa. Jamaa aliishia kuchanganyikiwa. Hata huvyo jaamaa alikuwa na mchepuko mwingine na alimchukua kuwa mke wake. Mchepuko alikuwa na kiwanja chake na jamaa bila kufikiri akiwa amepata pension yake akaenda wakajenga nyumba ya gorofa na baada ya nyumba kwisha mwanamke akamwambia aishie zake, huna chako hapa. Hati zote za kiwanja zilikuwa na jina la mwanamke, Jamaa aliendelea kuchnganyikiwa maana pesa yake yote iliishia pale. Haya ni mambo ya kujifunza sana unapomfanyia mke wako wa ndoa vibaya hivyo unategemea maisha yako yatakuwa mazuri kweli?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom