Wakati mwingine maisha ya ndoa hayaitaji usanii hata kidogo maana ndoa ukicheza nayo lazima ikupwelepwete tuu.Kabla ya kuamua kuishi na mtu tafakari na ujiulize hivi niko tayari kupambana na changamoto zake usiwaze harusi tuu na kujaza watu ukumbini.Kikubwa mwamini na kumtegemea Mungu kwanza maana kwa akili zako huwezi.
Wanaacha kumuogopa Mungu wanaogopa ndoa!!!! Kweli majasiri hatunao kabisa siku hizi. Zamani ili uoe ilibidi ufanye tendo moja LA kishujaa ili kuuthibishia umma Kuwa wewe ni mwanaume wa shoka. Wamasai usipoenda ukweni na kichwa cha Simba walikuwa wana kuona kama shoga vile
Kuna ukweli fulani, usipokuwa makini na chaguo lako itakula kwako kwa maana kila siku ya maisha yako itakuwa ni jaka moyo kwa kwenda mbele.
Ni changamoto kwakweli usipokuwa jasiri na mvumilivu unakata tamaa mazima.