Ndejembi: Jambo la Mama limetimia

Ndejembi: Jambo la Mama limetimia

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
843
Reaction score
1,024
"JAMBO LA MAMA LIMETIMIA-NDEJEMBI"

Anaandika Naibu Waziri Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Deo Ndejembi


Mhe Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia mapendekezo ya nyongeza ya mshahara ikiwemo kima cha chini kwa watumishi wa umma kwa 23.3%.

Mhe Rais ameonyesha wazi kwamba ameweka maslahi ya watumishi wa umma mbele. Sisi wasaidizi wake tutahakikisha maagizo yake na maono alionayo juu ya kuboresha utumishi wa umma yanatekelezwa kwa wakati.

Toka aingie madarakani amepandisha madaraja watumishi zaidi ya 200,000. Amelipa madeni ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi 104,350 yenye thamani ya billioni 154.5. Amepunguza makato ya kodi ya mshahara (PAYE) kutoka asilimia 9 hadi asilimia 8 ambayo pia ina effect kwenye mshahara. Mhe Rais alifuta retention fee kwa wanufaika wa bodi ya mikopo. Na kwa budget ya mwaka 21/22 Mhe Rais ameridhia kupandisha madaraja watumishi 91,000 ambao utekelezaji umeanza mwezi huu.

Mhe Rais kaonyesha imani kwa watumishi wa umma. Imani hii ni deni. Tumlipe kwa kufanya kazi

IMG-20220514-WA0701(1).jpg
 
Kwa hiyo aliyekuwa na 1M sasa ni 1,230,000 kabla ya PAYE maana makato mengine kama mkopo wa elimu, mkopo wa benki, makato ya saccos tunatofautiana.
 
Kwa hiyo aliyekuwa na 1M sasa ni 1,230,000 kabla ya PAYE maana makato mengine kama mkopo wa elimu, mkopo wa benki, makato ya saccos tunatofautiana.
Nyongeza ya mshahara kwa kima cha chini kwa watumishi wa umma ndiyo itakuwa 23.3%. Asilimia hii hupungua kwa kadiri kima cha mshahara kinapokwenda juu.
 
Kwa hiyo aliyekuwa na 1M sasa ni 1,230,000 kabla ya PAYE maana makato mengine kama mkopo wa elimu, mkopo wa benki, makato ya saccos tunatofautiana.
Hiyo kitu mkuu haiko kihivyo unavyofikria. 23.3% ni ya wale wa 270k, huku kwingine pamoja na kuongezeka lakini mshahara haijapanda kwa hiyo asilimia yote.
 
Watumishi Wa Umma Waelewe Kwamba Rais Ameridhia Nyongeza ya 23.3% kwenye Bajeti ya 2022/2023.
.
So Wasitegemee Salary ya Mwezi Huu Wa 5 wakaiona Hyo nyongeza, Kwa mfano ya elfu69+

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
"JAMBO LA MAMA LIMETIMIA-NDEJEMBI"

Anaandika Naibu Waziri Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Deo Ndejembi


Mhe Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia mapendekezo ya nyongeza ya mshahara ikiwemo kima cha chini kwa watumishi wa umma kwa 23.3%.

Mhe Rais ameonyesha wazi kwamba ameweka maslahi ya watumishi wa umma mbele. Sisi wasaidizi wake tutahakikisha maagizo yake na maono alionayo juu ya kuboresha utumishi wa umma yanatekelezwa kwa wakati.

Toka aingie madarakani amepandisha madaraja watumishi zaidi ya 200,000. Amelipa madeni ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi 104,350 yenye thamani ya billioni 154.5. Amepunguza makato ya kodi ya mshahara (PAYE) kutoka asilimia 9 hadi asilimia 8 ambayo pia ina effect kwenye mshahara. Mhe Rais alifuta retention fee kwa wanufaika wa bodi ya mikopo. Na kwa budget ya mwaka 21/22 Mhe Rais ameridhia kupandisha madaraja watumishi 91,000 ambao utekelezaji umeanza mwezi huu.

Mhe Rais kaonyesha imani kwa watumishi wa umma. Imani hii ni deni. Tumlipe kwa kufanya kazi

View attachment 2224506
Ok
 
Jambo la mama ,amewateua kingai bedui,wambura bedui,biwsalo bedui ili waibe uchaguzi 2025
 
Back
Top Bottom