well done washairi niko class najifunza haya mambo nikirudi hamnikamati ..kila siku nawatamania nyie mlobarikiwa ktk hii fani
well done washairi niko class najifunza haya mambo nikirudi hamnikamati ..kila siku nawatamania nyie mlobarikiwa ktk hii fani
Vilio vyenu nimesikia, mie ndege nimetua
X-Paster mesikia, nenolo sikioni limetua
toka mbali mesikia, moyoni likanitua
ukungu najauondoa, nimerudi wako ndege
Choveki na Mwanakijiji, wito nimeuitika
Narudi kwangu kijiji, X-Paster kumwitika
Nimechoka na hili jiji, wito ninauitika
Kifuani kwako narejea, X-paster unipokee
Ngambo Ngali nimerudi, kwake X-Paster kifuani
Kurejea sina budi, nimpe raha siyo kifani
Anyisile obheli hodi, X-Paster wangu mwandani
Ndege mie narejea, kumwangukia mwandani
Compaq nawe Amani, niachieni wangu mwandani
mbona hamumpi amani, kumwandama wangu hani
hebu tulieni kwa amani, niko kwake kifuani
X-Paster wangu mpenzi, twende tukapumzike ndani.
Furaha ya leo kesha, Umma nautangazia
Mazuri yangu Maisha, Ndege wangu karejea
Namfanyia Tamasha, Kucha Kutwa twaongea
Mapenzi kweli matamu, Leo nimeyabaini
Tutapeana mapenzi, Dunia ipate jua
Kwa haki tamuenzi, Mwingine apati tua
Huyu Wangu la azizi, Moyo umepata poa
Mapenzi kweli matamu, Leo nimeyabaini
Amerudi ametubu, Kama si yule wa jana
Penzi letu limesibu, Wapenzi tumekutana
Watu wanastaajabu, Jinsi tunavyo pendana
Mapenzi kweli matamu, Leo nimeyabaini
Twakumbushana zamani, Penzi tulivyo peana
Mengi tulio tamani, Leo tunakumbushana
Mimi na wangu mwandani, Twakesha kibusiana
Mapenzi kweli matamu, Leo nimeyabaini
Namaliza tano beti, Mbele sito endelea
Mpenzi avuta shati, Ndani nipate rejea
Nikampe sharubati, roho ipate kutua
Mapenzi kweli matamu, Leo nimeyabaini
Tutapeana mapenzi, Dunia ipate jua
Kwa haki tamuenzi, Mwingine apati tua
Huyu Wangu la azizi, Moyo umepata poa
Mapenzi kweli matamu, Leo nimeyabaini