Nchi ya wanafiki watupu

Nchi ya wanafiki watupu

kmbwembwe

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
10,931
Reaction score
7,828
Katika clip zinazorushwa kuonesha utendaji mzuri wa Sabaya ni pamoja na ile inamuonyesha mkuu wa takukuru wa sasa Salum Hamduni akimtunukia Sabaya cheti kwa utendaji wake kusaidia jeshi la polisi kupambana na uhalifu mkoani kilimanjaro. Hapo Hamduni alikua kamanda wa mkoa wa jeshi la polisi kilimanjaro.

Leo muda mfupi baada ya kufa Magufuli Hamduni yuleyule akiwa na uteuzi wa Rais Samia kama mkuu wa TAKUKURU anaonekana kutoa amri kukamatwa Sabaya na kufikishwa mahakama akiwa amewekwa pingu na kudhalilishwa eti alifanya ujambazi kumpora mfanya biashara shs 35000 na kutakatisha hela akiwa Mkuu wa Wilaya Kilimanjaro.

Huyo Hamduni sijui alikua wapi wakati Sabaya kama mkuu wa wilaya akifanya ujambazi kumpora mtu shs 35000 hadi sasa anatunikiwa cheo na Rais Samia kuwa kamanda wa TAKUKURU. Tusisahau mama samia amesema yeye na Magufuli ni kitu kimoja.

Dunia kwa hakika inaenda mbio kwelikweli.
 
Nachoamini ni kuwa, Unaweza kufanikiwa saana tu, ukawapeleka wengine jela kwa njia ya uwongo na pengine ukajipatia umaarufu mkubwa kwa kuwafanyia ubaya walioko juu yako ili uwe juu

Unaweza kumfanyia fitina boss wako kwa kuitaka hiyo nafasi kwa mbinu mbalimbali na ukafanikiwa,, Lakini amini usiamini, Huo ubaya ni lazima ukurudie soon

ndivyo ilivyo,
 
Back
Top Bottom