Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Patashika ya Ligi Kuu Tanzania NBC Premier League, kupigwa leo March 16, 2022 kwenye Dimba la Ilulu mkoani Lindi, huku vita kubwa ikiwa ni kuwania nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi.
Namungo FC na Azam FC zote kwa pamoja zina alama 25 huku zikiwa zimecheza michezo 17 ambapo timu yoyote itakaposhinda mchezo wa leo itakaa kwenye nafasi ya tatu kwa tofauti ya alama na si tofauti ya mabao ya kufunga.
Namungo FC hawajapoteza mchezo wowote kati ya michezo mitano ya mwisho walizoshuka dimbani ambapo wameshinda michezo mitatu na kutoka sare michezo miwili.
Azam FC wanahitaji kupata matokeo ya alama tatu muhimu ili kurejesha timu kwenye morali ya ushindi ambayo imetoweka hivi karibuni, hivyo Azam FC wanahitaji kulifanya hilo kwa Namungo FC ambayo ipo kwenye fomu kwa sasa kuliko Azam FC.
Je? Ipi nafasi ya Namungo FC na Azam FC kwenye vita ya kuwania nafasi ya tatu NBC Premier League.
Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 10: 00 Jioni.
Namungo FC na Azam FC zote kwa pamoja zina alama 25 huku zikiwa zimecheza michezo 17 ambapo timu yoyote itakaposhinda mchezo wa leo itakaa kwenye nafasi ya tatu kwa tofauti ya alama na si tofauti ya mabao ya kufunga.
Namungo FC hawajapoteza mchezo wowote kati ya michezo mitano ya mwisho walizoshuka dimbani ambapo wameshinda michezo mitatu na kutoka sare michezo miwili.
Azam FC wanahitaji kupata matokeo ya alama tatu muhimu ili kurejesha timu kwenye morali ya ushindi ambayo imetoweka hivi karibuni, hivyo Azam FC wanahitaji kulifanya hilo kwa Namungo FC ambayo ipo kwenye fomu kwa sasa kuliko Azam FC.
Je? Ipi nafasi ya Namungo FC na Azam FC kwenye vita ya kuwania nafasi ya tatu NBC Premier League.
Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 10: 00 Jioni.