structuralist
JF-Expert Member
- Oct 13, 2012
- 1,230
- 909
Kama tunavofahamu jumamosi benk nyingi hufungwa sa sita mchana. Sasa katika mishemishe nikalazimika kulipa mahali kama 1.3 milioni,hivo nikaona ngoja nikachomoe fasta kwenye ATM za NBC( MOSHI) . Kilichotokea ni kwamba kila ATM inasema kiwango cha juu kabisa kutoa ni laki mbli(200000), (kuna ATM 4,moja ilikuwa off,yapili haikuwa na fedha,mbili zilizobakia ndio zinatoa hicho kiwango)kwahiyo nikalazimika kutoa mara sita ili angalau nipate 1.2mln. Hii si mara yakwanza kushuhudia hili,na binafsi naamini wanafanya makusudi ili kujiongezea pesa zitokanazo na makato ya kila muaamala unaofanyika. Inafahamika kuwa kiwango cha juu kilikuwa laki nne(400000)je kimeshushwa au ni wizi wa mchana kweupeeeeee.....