Nautamani wakati mmoja ufike ambapo polisi itakuwa ni taasisi huru ambayo haitakuwa inafanya kazi kwa kusubiria kauli kutoka kwa viongozi wa serikali. Taasisi ambayo mkuu wake itafanya kazi kutokana na taratibu, sheria na kanuni haki ikitawala. Taasisi ambayo itamwajibisha yeyote bila kujali ni nani katika nchi. Taasisi ambayo itakuwa tayari kutoa vibari na kuwalinda raia pale wanapohitaji kufikisha ujumbe fulani kwa njia ya maandamano. Nautamani wakati huu, nautamani siku moja uje hata ikiwezekana sasa kwa nchi yangu Tanzania