Nawezaje kuwa Usalama wa Taifa?

Nawezaje kuwa Usalama wa Taifa?

Behind the camera

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2019
Posts
315
Reaction score
757
Narudia tena kusema ‘MFICHA MARADHI, KIFO HUMUUMBUA’

Habari za muda huu ndugu zangu, waungwana wenzangu. BIla shaka afya zenu ni njema na mnaendelea vema kabisa na majukumu ya kulijenga taifa letu la Tanzania.

HONGERENI SANA
  • Waswahili walisema “Mficha maradhi, mauti humuumbua”
Kauli hii ina maana kubwa sana, kama utakaa na kuitafakari utagundua ukweli wake. Kwani kama una dukuduku ambalo limekukwaza ama linakuumiza katika moyo ni vema ukalisema kwa wahusika ili huenda ukapata msaada ama ushauri juu ya jambo lako. Kwani ukiendelea kunyamaza unaweza kuathirika na hatimaye kupoteza Maisha na baada ya kufa kwako watu wakagundua tatizo lililokuuwa na watu kukulaumu (marehemu) huenda ungesema usingekufa.

AMA BAADA YA UTANGULIZI

Lengo la kuandika uzi huu wa heshima, napenda kuelezea dukuduku langu kwa umma huenda siku moja uzi huu ukasomwa na ambaye anaweza kulitatua tatizo langu na kupata ufumbuzi.

Nafikiri utakubaliana na mimi kuwa kila mtu katka Maisha yake huwa ana ndoto na kutamani awe mtu Fulani ama kufanya kazi Fulani, lakini mara nyingi ndoto hizo huishia kuwa ndoto tu na si halisi.

Natumia fursa hii nami kuelezea ndoto zangu ambazo nilikuwa, ninazo na nitakuwa nazo mpaka mwisho wa umri wangu.

Mimi nilitamani sana kufanya kazi katika idara ya USALAMA WA TAIFA

Ndio namaanisha usalama wa Taifa langu la Tanzania katika sekta yoyote ambayo wao watanipangia. Uzalendo ndicho hasa kilinifanya nipende kuwa katika kulitumikia na kulilinda Taifa langu kikamilifu.

Sikufanya jitihada zozote kwani sijui wapi naweza kupata suluhisho la hitaji langu, wala sikuwa / sina mtu ambaye ana uwezo wa kunifanikishia suala langu hili pendwa.

Leo nimeona niliweke wazi katika mtandao huu nambari moja hapa Tanzani najua baadhi ya wadau watakuwemo humu. Huenda wakanisaidia.

Najua baadhi yao watanibeza na kuongea maneno yasio na nidhamu, lakini hili kwangu nachukulia kama changamoto nyingine tu za kimaisha.

Naipenda TANZANIA, Nawapenda Watanzania,

MUNGU IBARIKI TANZANIA

Natanguliza shukrani zangu za dhati.



Kwa maswali Zaidi unaweza kuja PM
 
Ila Hawa jamaa mungu anawaona

Mimi kitaa watu weng wanajua ni mtu wa usalama kutokana na life style yangu haieleweki naweza kuwepo sehem Mara sipo.

Hii kitu imejua kunitesa Sana hata nikijitetea kwa watu wanaonizunguka huwa hawaamini kabisa kwamba mm sipo huko but all in all siwalaumi wao mi nawalaumu hao watu wa usalama ni kwann hawakuniona mapema wakanitumia kuliko saiv nahisiwa vibaya halaf wao wapo tu wanazunguka...
 
Kwani wale wanatafuta mtu au mtu anajipeleka..?
Kama hata hili hujui inaweza kukutia ugumu!..
Nikushauri wakati umetia hiyo nia yako kumbuka na upande wapili pia.. usiwaze tu kuwa usalama huku kuja kushtuka hawaji na umri umekupiga ukaanza kujilaumu bora ungedili na mambo yako!!..
Ikiwapendeza watakufuata.. lkn mkuu isijekuwa unaiga kunya kwa tembo..😅
 
Uuzaji, utumiaji, utengenezaji (repair), COMPUTERS

Kwa shughuli zako hizo mbona tayari unaweza kuyaendeleza maisha bila hizo shughuli za usalama? Kwani ukiwa usalama utakuwa na shughuli gani specific? Kwa huo uzalendo wako, katika shughuli zako hizo uwe una ripoti uuzaji wa mali za wizi unazoletewa na repair, pia maswala ya programu tumishi za kufanyia uhalifu uwe unawasilisha taarifa zake katika vyombo vya usalama. Hapo tayari utakuwa mzalendo nha utakuwa umelitumikia taifa lako.
 
It'a press halafu tangazo kuunga mkono juhud,sifiasana
 
Back
Top Bottom