naweza kumsamehe MANGUNGO WA MSOVERO

nguvumali

JF-Expert Member
Sep 3, 2009
4,923
1,325
niliutazama Ujio wa rais wa China kwa masikitiko sana na Tangu jana nimekuwa nikiangalia Mbwembwe za kumpokea Rais Obama na Wamarekani wengine kama Kejeli ya wakati wote katika Taifa letu.
Wakuu wetu wametuambia kuwa Urafiki huu ni urafiki wa Kihistoria na hakika utasaidia pande zote mbili.(tunajilisha upepo).....!
Wachina , Wamarekani na mapebari wengine hawaji hapa kwakua wanatupenda au tuna demokrasia yakutilia mfano barani Afrika, bali wanakuja hapa kwakua ni moja ya maeneo machache yenye raslimali adhimu duniani, wanakuja kuweka mirija yao ya unyonyaji na wapo tayari kwa hilo.
Jiulize kwa gharama zote hizi wanazoingia hawa watu ni kwa mapanzi ya dhati kwetu ?
Inaumiza kwakua tunawavika mataji ya maua wanyonyaji wetu, tunawafagilia barabara na kuzipiga deki njia watakazopita, inakera kwakua Mbele ya safari wajukuu zetu watattuona kizazi cha mambulura kama ambavyo sisi tunawaona wazee waliouza nchi hii kwa vipande vya kioo na shanga kuwa hawakuwa makini na wazalendo.
wajukuu zetu watajiuliza mengi watakapokuwa wanasoma kwenye historia kuwa tuliwahi kuwa na dhahabu, Gas, Mafuta na raslimali zingine, watatuzodoa sana.

heri waliotusaliti kipindi cha utumwa na ukoloni hawakuwa hata na uelewa mpana wa mambo kuliko hawa wasomi, wanaojua mambo kwa kina lakini macho na akili zimepofuka na hakika hatutafika.

NIMEWASAMEHE KINA MANGUNGO, NIMESAMEHE WALIOSAIDIA UKOLONI LAKINI HAWA WANAOTUUZA LEO SITAWASAMEHE.

Four-soldiers-of-the-Kings-African-Rifles.jpg
 
niliutazama Ujio wa rais wa China kwa masikitiko sana na Tangu jana nimekuwa nikiangalia Mbwembwe za kumpokea Rais Obama na Wamarekani wengine kama Kejeli ya wakati wote katika Taifa letu.
Wakuu wetu wametuambia kuwa Urafiki huu ni urafiki wa Kihistoria na hakika utasaidia pande zote mbili.(tunajilisha upepo).....!
Wachina , Wamarekani na mapebari wengine hawaji hapa kwakua wanatupenda au tuna demokrasia yakutilia mfano barani Afrika, bali wanakuja hapa kwakua ni moja ya maeneo machache yenye raslimali adhimu duniani, wanakuja kuweka mirija yao ya unyonyaji na wapo tayari kwa hilo.
Jiulize kwa gharama zote hizi wanazoingia hawa watu ni kwa mapanzi ya dhati kwetu ?
Inaumiza kwakua tunawavika mataji ya maua wanyonyaji wetu, tunawafagilia barabara na kuzipiga deki njia watakazopita, inakera kwakua Mbele ya safari wajukuu zetu watattuona kizazi cha mambulura kama ambavyo sisi tunawaona wazee waliouza nchi hii kwa vipande vya kioo na shanga kuwa hawakuwa makini na wazalendo.
wajukuu zetu watajiuliza mengi watakapokuwa wanasoma kwenye historia kuwa tuliwahi kuwa na dhahabu, Gas, Mafuta na raslimali zingine, watatuzodoa sana.

heri waliotusaliti kipindi cha utumwa na ukoloni hawakuwa hata na uelewa mpana wa mambo kuliko hawa wasomi, wanaojua mambo kwa kina lakini macho na akili zimepofuka na hakika hatutafika.

NIMEWASAMEHE KINA MANGUNGO, NIMESAMEHE WALIOSAIDIA UKOLONI LAKINI HAWA WANAOTUUZA LEO SITAWASAMEHE.

Four-soldiers-of-the-Kings-African-Rifles.jpg
Unajua kitu Kimoja ni Kwamba Hamna rafiki duniani. Hapa ni biashara tu. Kama unafikiri kuwa Tanzania itatajirika kwa kufunga mipaka basi inabidi uelewe zaidi biashara za kimataifa na Sheria zake. Tanzania haiwezi kutoruhusu wageni kufanya biashara ( wewe unaita unyonjaji) lakini watanzania Wauze nje wenyewe. La muhimu ni kuhakikisha kuwa wanaokuja kufanya shughuli hapa wanaleta teknolojia, fedha na kazi Nzuri kwa jamii. Hakuna hata nchi Moja imeendea peke Yake. Duniani ya Leo ni Ndogo sana na mawazo yako ya kuwaona kila mgeni anayeluja Tanzania kufanya kazi Kama ni Adui au mwizi wa rasilimali ya nchi, imepitwa na Wakati. Ipi ni bora, ulimaji unatumia trekta na teknolojia mpya ili izalishe zaidi na kwa wingi au kumwachia mkulima masikini na asiye na elimu ya juu, Hela Moja ????
Mawazo Kama yako Ndio yanaendelesha umasikini Tanzania, tumshukuru Nyerere kwa kutuonyesha kila bepari ni Adui wa nchi. Hata mchina amesutuka, Sisi bado tunasinzia.
 
Bepari peke Yake Ndio anajenga nchi, Sio serikali. Onyesha nchi Moja imeendelea kwa kumbana bepari?
 
niliutazama Ujio wa rais wa China kwa masikitiko sana na Tangu jana nimekuwa nikiangalia Mbwembwe za kumpokea Rais Obama na Wamarekani wengine kama Kejeli ya wakati wote katika Taifa letu.
Wakuu wetu wametuambia kuwa Urafiki huu ni urafiki wa Kihistoria na hakika utasaidia pande zote mbili.(tunajilisha upepo).....!
Wachina , Wamarekani na mapebari wengine hawaji hapa kwakua wanatupenda au tuna demokrasia yakutilia mfano barani Afrika, bali wanakuja hapa kwakua ni moja ya maeneo machache yenye raslimali adhimu duniani, wanakuja kuweka mirija yao ya unyonyaji na wapo tayari kwa hilo.
Jiulize kwa gharama zote hizi wanazoingia hawa watu ni kwa mapanzi ya dhati kwetu ?
Inaumiza kwakua tunawavika mataji ya maua wanyonyaji wetu, tunawafagilia barabara na kuzipiga deki njia watakazopita, inakera kwakua Mbele ya safari wajukuu zetu watattuona kizazi cha mambulura kama ambavyo sisi tunawaona wazee waliouza nchi hii kwa vipande vya kioo na shanga kuwa hawakuwa makini na wazalendo.
wajukuu zetu watajiuliza mengi watakapokuwa wanasoma kwenye historia kuwa tuliwahi kuwa na dhahabu, Gas, Mafuta na raslimali zingine, watatuzodoa sana.

heri waliotusaliti kipindi cha utumwa na ukoloni hawakuwa hata na uelewa mpana wa mambo kuliko hawa wasomi, wanaojua mambo kwa kina lakini macho na akili zimepofuka na hakika hatutafika.

NIMEWASAMEHE KINA MANGUNGO, NIMESAMEHE WALIOSAIDIA UKOLONI LAKINI HAWA WANAOTUUZA LEO SITAWASAMEHE.

Four-soldiers-of-the-Kings-African-Rifles.jpg

Waje tu hao wazungu kuchukua rasilimali zetu. Tumekalia majungu tu. Kazi hatufanyi. Kila kitu siasa. Ujanja ujanja, ubabaishaji, rushwa, wizi, undugunaizesheni, uzembe, wivu, kutokuheshimu kazi, ukosefu wa uzalendo, ndio mambo yetu hayo. Kwa taarifa yako, wajukuu zetu hawatauliza kuhusu matumizi ya rasilimali zetu, kama ambavyo wajukuu wa akina mangungo (kikwete na wenzake) ambavyo hawajajiuliza. Fikria, Mangungo aligawa kipande cha msowero zaidi ya karne moja iliyopita. Mbona akina kikwete hawajajiuliza kwa nini akina mangungo walifanya yale waliyofanya. Sana sana, wanachofanya ni kubariki mambo waliyoyafanya akina mangungo.

 
Unajua kitu Kimoja ni Kwamba Hamna rafiki duniani. Hapa ni biashara tu. Kama unafikiri kuwa Tanzania itatajirika kwa kufunga mipaka basi inabidi uelewe zaidi biashara za kimataifa na Sheria zake. Tanzania haiwezi kutoruhusu wageni kufanya biashara ( wewe unaita unyonjaji) lakini watanzania Wauze nje wenyewe. La muhimu ni kuhakikisha kuwa wanaokuja kufanya shughuli hapa wanaleta teknolojia, fedha na kazi Nzuri kwa jamii. Hakuna hata nchi Moja imeendea peke Yake. Duniani ya Leo ni Ndogo sana na mawazo yako ya kuwaona kila mgeni anayeluja Tanzania kufanya kazi Kama ni Adui au mwizi wa rasilimali ya nchi, imepitwa na Wakati. Ipi ni bora, ulimaji unatumia trekta na teknolojia mpya ili izalishe zaidi na kwa wingi au kumwachia mkulima masikini na asiye na elimu ya juu, Hela Moja ????
Mawazo Kama yako Ndio yanaendelesha umasikini Tanzania, tumshukuru Nyerere kwa kutuonyesha kila bepari ni Adui wa nchi. Hata mchina amesutuka, Sisi bado tunasinzia.

Tanzania inanufaika kiwenda wazimu na raslimali za asili, Rejea mikataba ya madini .... na kauli ya Kikwete alipoingia Ikulu kuhusu mikataba na sheria mbaya ambazo yeye akiwa waziri alishiriki kuzipitisha kwa maslahi yao.

Tokyo, hawa Wamerekani waliwahi kwenda kwa Museven kumshawishi kuhusu kuchimba mafuta kule kaskazini magharibi ya Uganda walijibiwa fifty~fity ownership, maana wao wana mitaji teknolojia na waganda wana Mtaji madini..! hivyo ndivyo taifa linapaswa kuwa.
Hebu jiulize tunamiliki kiasi gani kwenye migodi ya Barick ? je faida baada ya kodi inaenda wapi ? hatuwezi kwenda kwa mikataba dhaifu ya kimangungo kama wanayoingia viongozi wa TAIFA LETU....hakika Mangungo namsamehe lakini haya ya serikali hiii hayavumiliki
 
Waje tu hao wazungu kuchukua rasilimali zetu. Tumekalia majungu tu. Kazi hatufanyi. Kila kitu siasa. Ujanja ujanja, ubabaishaji, rushwa, wizi, undugunaizesheni, uzembe, wivu, kutokuheshimu kazi, ukosefu wa uzalendo, ndio mambo yetu hayo. Kwa taarifa yako, wajukuu zetu hawatauliza kuhusu matumizi ya rasilimali zetu, kama ambavyo wajukuu wa akina mangungo (kikwete na wenzake) ambavyo hawajajiuliza. Fikria, Mangungo aligawa kipande cha msowero zaidi ya karne moja iliyopita. Mbona akina kikwete hawajajiuliza kwa nini akina mangungo walifanya yale waliyofanya. Sana sana, wanachofanya ni kubariki mambo waliyoyafanya akina mangungo.


hawa ni MANGUNGO WA KARNE MPYA NA KIZAZI KIPYA
 
Bora mara 100 kina mangungo kuliko hawa madokta dokta na maporofeseli wanasiani mikataba ambayo hata mtoto wa darasa la pili anayejua english ya std 2 hawezi saini.
 
alipokuja Rais wa china walitujuza kuwa mikataba 17 ilisainiwa, huyu OBAMA kaja na kuondoka wanaona hata aibu kusema wamesaini mikataba thelathini na ngapi
 
tatizo la viongozi wa taifa letu wanaona kupata misada ndio maendeleo hivyo kwa maksudi wanaamua kujitoa ufahamu na kutudanganya kuwa wamarekani ni marafiki wazuri cha ajabu hatuonyeshwi uzuri huo uko wapi zaidi ya kutupa vyandarua na mseto tena mseto wenyewe upo katika majaribio na hao huchukua rasili mali zetu kiulaini haya c ndo yale yale ya kina mangungo kupewa marumaru kisha akauza ardhi?!...hakika sioni tofauti ya viongozi wetu na akina mangungo maana kwa sasa tunajengewa barabara,kupewa vyandarua with exchange of our precious resources na hii inatoka na viongoz wetu kujifikiria wao kwanza kuliko wananchi.
 
Dar wamependeza kama magwanda ya peoples ..........Power. Ila ni kweli afadhali mangungo wa msowelo kuliko hawa watawala wa sasa.
 
Mangungo wa MSOWERO(MSOVERO) hakua na ufahamu na nini anakifanya na wakati mwingine machifu wetu walisaini mikataba under presha toka kwa wazungu/wakoloni,Hawa THE SO CALLED viongozi Wetu wanasaini ili khali wakiwa na uelewa na nini wanafanya halafu eti mikataba ya kina MANGUNGO mnaiita BOGUS TREATIES!;-( ile ilikua Fake na ya sasa ndio BOGUS tena BOGUS KWELIKWELI;-> na vio.ngozi nao ni maBOGUS tu
 
Back
Top Bottom