ellyrehema
JF-Expert Member
- Jan 13, 2012
- 1,199
- 989
Jamani habari zenu. kama kuna daktari ataweza kunisaidia tatizo langu hili nitafurahi sana. mimi nina miaka 34 na tangu nikiwa na umri wa miaka 24 nilianza kusikia kama maralia muda wote mara iningine ukipima inakuwepo ukinywa dawa hujisikii nafuu ila ukipima tena unakuta hakuna maralia, baadae nikaiona ni hali ya kawaida baada ya kuzoea. nahisi maumivu ya mifupa, masikio yanavuma ziiiiii!!!!, pia kichwa kinauma ila si sana. hali hii ni muda wote tangu nikiwa na umri huo. nimetumia dawa nyingi tu bila mafanikio. nilienda kwa watu wa tiba mbadala nikaambiwa eti mifupa yangu imezeeka kuliko umri wangu, pia nina sumu nyingi mwilini nahitaji kufanyiwa Detoxin, nilishindwa bei ya matibabu yao kwani niliambiwa laki tano. maisha yangu si mabaya na pia si mazuri saaana ni mtu wa kawaida kwani nina kipato cha wastani.na ninaishi kwa kufuata kanuni zote za afya.
kinachonishangaza naugua sana kila mwezi lazima niugue maralia nilishapima ukimwi sina,
SWALI je kuna hduma ya kuondoa sumu kitaalam(hospitalini?) na hii huduma inapatikana hospitali gani na kwa bei gani?. sasa naona nitakufa mapema na muda mwingine huwa naacha kunywa dawa tu na sizidiwi ila mwili wangu unaugua tu muda wote. naomba tuwasiliane kwa email yangu derick4u@ymail.com
kinachonishangaza naugua sana kila mwezi lazima niugue maralia nilishapima ukimwi sina,
SWALI je kuna hduma ya kuondoa sumu kitaalam(hospitalini?) na hii huduma inapatikana hospitali gani na kwa bei gani?. sasa naona nitakufa mapema na muda mwingine huwa naacha kunywa dawa tu na sizidiwi ila mwili wangu unaugua tu muda wote. naomba tuwasiliane kwa email yangu derick4u@ymail.com