Safi sana Jide. Wale mbwa koko watabweka hadi makoo yawakakuke kudadadeki.
We naona umebadili kituo cha kazi leo toka Kona Bar kwenda hapo kwa kibibi.
Nilisoma ujumbe wa jide kwenye tweeter anasema SUGU KASHANGILIWA SANAAAAA,,,
na humu kuna wadau walim'beza sana SUGU HAPA
Nimefurahia show ya JIDE hapa Nyumbani Lounge, hakika ni mapinduzi makubwa JIDE akiwa na mama yake mzazi ameonyesha njia kwa wasanii wa kike kufanya kazi zao kwa bidii na kuwa na heshima. JIDE ameungwa mkono na watu wazima, vijana na watoto , ni heshima kubwa na namsihi sana atunze na kulinda heshima hii, kama ana mapungufu kadhaa ya kibinadamu ajirekebishe, umatu uliomuunga mkono katika kipindi hiki cha mifarakano ni hazina kubwa.
JIDE amepigana dhidi ya mfumo dume , kandamizi na wenye minyororo wenye kutaka kuabudiwa, hivyo basi wasanii wazinduke wawe huru kufanya kazi popote na mtu yeyote ili kujiondoa kwenye uonevu, kazi ndiyo uwe msingi wa ushindani na sio kubebwa na kubembeleza.
Nikamate KLM nirejee kazini.
Phd (Dar es salaam)