Natoa shukrani kwa wadau wote waliotutumia rambirambi

MK254

JF-Expert Member
May 11, 2013
31,760
48,408
Shukran wadau kwa rambirambi zote mlizotupa, binafsi nimepokea nyingi tu kwenye Whatsapp kutoka kwa washkaji ukanda huu, ni dhahiri likija suala la magaidi Afrika mashariki huungana na kuwa wamoja. Hawa watu hawana mipaka, ni mazombi yaliyozaliwa kwa bahati mbaya, yameaminishwa mambo ya kiajabu ajabu, na nia yao huwa kueneza uwoga, ila wakiona jamii inaungana kwa ujasiri na kuwa wamoja dhidi yao, wanahesabu kama hasara kubwa sana.

Hivyo binafsi natoa shukrani kwa majirani wote waliotutumia rambirambi, lakini pia kwa wale kizazi cha nyoka Watanzania wachache waliokesha humu JF wakibeza na kuchekea mauaji yaliyokua yanaendelea, nawapa zoezi rahisi sana, nenda kajiangalie kwenye kioo kwa zaidi ya dakika kumi, ujiulize huyo mtu aliye ndani ya hicho kioo anakutazama, kama ndiye ulikusudia kuishi naye kwa miaka yote ijayo, au anahitaji kurekebisha kitu.

Utani wetu ubaki kwenye mitandao, lakini likija suala linalogusa uti wa mgongo wa jamii yetu, tunafaa kulikemea sote kwa pamoja, ifahamike hii mipaka imechorwa na mzungu na kutupa majina ya kutumia kwenye utaifa.
 
Shukran wadau kwa rambirambi zote mlizotupa, binafsi nimepokea nyingi tu kwenye Whatsapp kutoka kwa washkaji ukanda huu, ni dhahiri likija suala la magaidi Afrika mashariki huungana na kuwa wamoja. Hawa watu hawana mipaka, ni mazombi yaliyozaliwa kwa bahati mbaya, yameaminishwa mambo ya kiajabu ajabu, na nia yao huwa kueneza uwoga, ila wakiona jamii inaungana kwa ujasiri na kuwa wamoja dhidi yao, wanahesabu kama hasara kubwa sana.

Hivyo binafsi natoa shukrani kwa majirani wote waliotutumia rambirambi, lakini pia kwa wale kizazi cha nyoka Watanzania wachache waliokesha humu JF wakibeza na kuchekea mauaji yaliyokua yanaendelea, nawapa zoezi rahisi sana, nenda kajiangalie kwenye kioo kwa zaidi ya dakika kumi, ujiulize huyo mtu aliye ndani ya hicho kioo anakutazama, kama ndiye ulikusudia kuishi naye kwa miaka yote ijayo, au anahitaji kurekebisha kitu.

Utani wetu ubaki kwenye mitandao, lakini likija suala linalogusa uti wa mgongo wa jamii yetu, tunafaa kulikemea sote kwa pamoja, ifahamike hii mipaka imechorwa na mzungu na kutupa majina ya kutumia kwenye utaifa.

Tunarudia tena pole sana, ila serikali kama imeamua kuangamiza hawa alshaabab a.k.a waoga iwe serious wajitoe kwelikweli kama sisi tulivyomwondoa nduli idiamni. Ni kuingia wazina wazima huko somalia na kuwakong’ota . Hawa jamaa wanafundisha watoto wadogo wanagrow na hiyo aggressiveness maana binadamu wa kawaid hawezi kufanya huo ushenzi wa kuuwa binadamu ambao hawana hatia. Kama kweli ni wababe si wawe wanavamia KDF ili tujue wako vizuri? Kwa sababu ya uoga wao wanamuua mtu ambae hana silaha. Wakafie mbali
 
Uncle maguuu njoo tuokoeee!!
FB_IMG_1547670201826.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunarudia tena pole sana, ila serikali kama imeamua kuangamiza hawa alshaabab a.k.a waoga iwe serious wajitoe kwelikweli kama sisi tulivyomwondoa nduli idiamni. Ni kuingia wazina wazima huko somalia na kuwakong’ota . Hawa jamaa wanafundisha watoto wadogo wanagrow na hiyo aggressiveness maana binadamu wa kawaid hawezi kufanya huo ushenzi wa kuuwa binadamu ambao hawana hatia. Kama kweli ni wababe si wawe wanavamia KDF ili tujue wako vizuri? Kwa sababu ya uoga wao wanamuua mtu ambae hana silaha. Wakafie mbali

Asante kwa pole ila huo ushauri wako ni vigumu kuutekeleza maana umewashinda hata Marekani na Urusi kule kwenye ugomvi wao na ISIS, ifahamike vita vyenu na Amin vilikua rahisi sana, vita dhidi ya utawala wa Amin ambao ulikua umechokwa na wananchi wa Uganda ikiwemo hata baadhi ya wanajeshi wake walikua wamemchoka, hivyo ilikua ni kumkomoa akaikmbia nchi mapema, kingine ni kwamba yeye na wafuasi wake walikua waoga wa kifo, hawakua wanajitoa mhanga au itikadi wala nini, walikua wanapora na kutoweka.

Lakini vita vya kisasa unapigana na adui aliyejificha ndani ya raia, amejifunga mabomu na yupo anatamani sana afe akapate thawabu aliyoaminishwa. Hapo kwanza anawaua raia wasiokua na hatia ili kusudi afe na wengi, wewe kama askari komando unategemewa umuondoe humo ndani kwa kutumia ujuzi na kuhakikisha hausababishi maafa ya raia wema.

Kingine, KDF hawawezi kwenda kibabe pale Somalia na kumimina risasi, lazima wawe makini kwa kuhakikisha uungwaji mkono na raia wa kawaida, maana propaganda zikienezwa kwamba wapo kule kuwaua raia, basi wengi watajiunga kwenye kujitoa mhanga dhidi yao, vita vya kisasa sio vifaru na mabunduki tu, ila vinahitaji mikakati ya kijamii na kujua jinsi ya kupata ushirikiano kutoka kwa wote.
Unakuta kundi la wazee wanachunga mbuzi malishoni, hawana ugomvi na mtu wapo kwenye mazungumzo yao, lakini ukiwapa mgongo ghafla unashtuka kumbe ni mashababi na humo kwenye mifugo wameficha silaha za kila aina. Sasa michezo kama hii inahitaji kuwa na mashushu wanaokusaidia kupata taarifa, ila na wao wakikamatwa huchinjwa kama mbuzi.
 
Shukran wadau kwa rambirambi zote mlizotupa, binafsi nimepokea nyingi tu kwenye Whatsapp kutoka kwa washkaji ukanda huu, ni dhahiri likija suala la magaidi Afrika mashariki huungana na kuwa wamoja. Hawa watu hawana mipaka, ni mazombi yaliyozaliwa kwa bahati mbaya, yameaminishwa mambo ya kiajabu ajabu, na nia yao huwa kueneza uwoga, ila wakiona jamii inaungana kwa ujasiri na kuwa wamoja dhidi yao, wanahesabu kama hasara kubwa sana.

Hivyo binafsi natoa shukrani kwa majirani wote waliotutumia rambirambi, lakini pia kwa wale kizazi cha nyoka Watanzania wachache waliokesha humu JF wakibeza na kuchekea mauaji yaliyokua yanaendelea, nawapa zoezi rahisi sana, nenda kajiangalie kwenye kioo kwa zaidi ya dakika kumi, ujiulize huyo mtu aliye ndani ya hicho kioo anakutazama, kama ndiye ulikusudia kuishi naye kwa miaka yote ijayo, au anahitaji kurekebisha kitu.

Utani wetu ubaki kwenye mitandao, lakini likija suala linalogusa uti wa mgongo wa jamii yetu, tunafaa kulikemea sote kwa pamoja, ifahamike hii mipaka imechorwa na mzungu na kutupa majina ya kutumia kwenye utaifa.
poleni sana kwa yote yaliwafika but this time security guys need to be highly congratulated as they have shown indomitable,quick,coordinated responce and great competence.we as east africans need to be together on this critical juncture to greatly condemn to the strongest term possible this terrorist attack which is against morals and human civilization.May GOD keep the lost souls in eternal peace.lastly unless you are a sadist or very uncouth you can't joke when your bros and sisters are in trouble.
 
Ondokeni kwao. Fungasheni virago haraka. Alshabab Walisha wa ambia Ondokeni hamsikii. KDF Wanabaka wanauwa na wana nyanganya mali za wasomali. Si muondoke mu waache wauwane wenyewe na nyie mpate ahueni.
Anyway poleni sana majirani
Shukran wadau kwa rambirambi zote mlizotupa, binafsi nimepokea nyingi tu kwenye Whatsapp kutoka kwa washkaji ukanda huu, ni dhahiri likija suala la magaidi Afrika mashariki huungana na kuwa wamoja. Hawa watu hawana mipaka, ni mazombi yaliyozaliwa kwa bahati mbaya, yameaminishwa mambo ya kiajabu ajabu, na nia yao huwa kueneza uwoga, ila wakiona jamii inaungana kwa ujasiri na kuwa wamoja dhidi yao, wanahesabu kama hasara kubwa sana.

Hivyo binafsi natoa shukrani kwa majirani wote waliotutumia rambirambi, lakini pia kwa wale kizazi cha nyoka Watanzania wachache waliokesha humu JF wakibeza na kuchekea mauaji yaliyokua yanaendelea, nawapa zoezi rahisi sana, nenda kajiangalie kwenye kioo kwa zaidi ya dakika kumi, ujiulize huyo mtu aliye ndani ya hicho kioo anakutazama, kama ndiye ulikusudia kuishi naye kwa miaka yote ijayo, au anahitaji kurekebisha kitu.

Utani wetu ubaki kwenye mitandao, lakini likija suala linalogusa uti wa mgongo wa jamii yetu, tunafaa kulikemea sote kwa pamoja, ifahamike hii mipaka imechorwa na mzungu na kutupa majina ya kutumia kwenye utaifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ondokeni kwao. Fungasheni virago haraka. Alshabab Walisha wa ambia Ondokeni hamsikii. KDF Wanabaka wanauwa na wana nyanganya mali za wasomali. Si muondoke mu waache wauwane wenyewe na nyie mpate ahueni.
Anyway poleni sana majirani

Sent using Jamii Forums mobile app
Bro
-yaani watoke kwenye un mission?!!!
-Wakitoka itasaidia nini somalia na dunia??
Kenya ikitoka inawapa guarantee ya usalama kama jirani ya somalia???
Umewahi kujua lengo la al -kaeda?
 
Asante kwa pole ila huo ushauri wako ni vigumu kuutekeleza maana umewashinda hata Marekani na Urusi kule kwenye ugomvi wao na ISIS, ifahamike vita vyenu na Amin vilikua rahisi sana, vita dhidi ya utawala wa Amin ambao ulikua umechokwa na wananchi wa Uganda ikiwemo hata baadhi ya wanajeshi wake walikua wamemchoka, hivyo ilikua ni kumkomoa akaikmbia nchi mapema, kingine ni kwamba yeye na wafuasi wake walikua waoga wa kifo, hawakua wanajitoa mhanga au itikadi wala nini, walikua wanapora na kutoweka.

Lakini vita vya kisasa unapigana na adui aliyejificha ndani ya raia, amejifunga mabomu na yupo anatamani sana afe akapate thawabu aliyoaminishwa. Hapo kwanza anawaua raia wasiokua na hatia ili kusudi afe na wengi, wewe kama askari komando unategemewa umuondoe humo ndani kwa kutumia ujuzi na kuhakikisha hausababishi maafa ya raia wema.

Kingine, KDF hawawezi kwenda kibabe pale Somalia na kumimina risasi, lazima wawe makini kwa kuhakikisha uungwaji mkono na raia wa kawaida, maana propaganda zikienezwa kwamba wapo kule kuwaua raia, basi wengi watajiunga kwenye kujitoa mhanga dhidi yao, vita vya kisasa sio vifaru na mabunduki tu, ila vinahitaji mikakati ya kijamii na kujua jinsi ya kupata ushirikiano kutoka kwa wote.
Unakuta kundi la wazee wanachunga mbuzi malishoni, hawana ugomvi na mtu wapo kwenye mazungumzo yao, lakini ukiwapa mgongo ghafla unashtuka kumbe ni mashababi na humo kwenye mifugo wameficha silaha za kila aina. Sasa michezo kama hii inahitaji kuwa na mashushu wanaokusaidia kupata taarifa, ila na wao wakikamatwa huchinjwa kama mbuzi.
Unaona sasa mahali unapofeli, jamaa amekupa ushauri mzuri tu na kujaribu kufanya partial relationship kati ya hari ya jeshi kati ya KDF na JWTZ kwa kutumia case ya vita vya Kagera, of course kuna vita nyingi JWTZ imepigana zikiwemo za kukomboa mataifa ya kusini, pia angeweza kutumia kama reference to his point.

Lakini ili utimize azma yenu wa Kenya kujipiga kifua na kujiona superior for petty things umeanza ku underrate vita ya Kagera ooh sijui walikua thaifu, ooh amini alikua hapendwi, ooh ilikua ndogo, ooh vita ilikua ya kizamani sasa blabla zote hizo zilikua za kazi gani?

Kwenye vita ya Kagera, Uganda ilikua na washirika wengi wakiwamo Libya na mataifa ya Ulaya, Tanzania ilikua peke yake mpaka OAU ya wakati huo ilikwepa kusuluhisha ule mgogoro diplomatically, Tanzania personality all alone waged the entire war with his own little resources. Sasa sina haja ya kuongelea yote hayo.

Ungetakiwa tu umuitikie mdau hapo with neutrality response na sio kutafuta namna ya kuidunisha JWTZ kwa excuses za kishamba, Kwani mbona KDF zaidi ya 100 waliuawa huko kwenye kambi yao Somalia na hao alshabaab mpaka Rais wenu kagoma kutoa idadi kamili ya waliouwawa na hatujaongea, kila siku KDF wanategewa mabomu ya barabarani wanauwawa, mkubali tu kupokea michango ya wadau hata kama inauma, vita haipiganwi kwenye social media.
 
Unaona sasa mahali unapofeli, jamaa amekupa ushauri mzuri tu na kujaribu kufanya partial relationship kati ya hari ya jeshi kati ya KDF na JWTZ kwa kutumia case ya vita vya Kagera, of course kuna vita nyingi JWTZ imepigana zikiwemo za kukomboa mataifa ya kusini, pia angeweza kutumia kama reference to his point.

Lakini ili utimize azma yenu wa Kenya kujipiga kifua na kujiona superior for petty things umeanza ku underrate vita ya Kagera ooh sijui walikua thaifu, ooh amini alikua hapendwi, ooh ilikua ndogo, ooh vita ilikua ya kizamani sasa blabla zote hizo zilikua za kazi gani?

Kwenye vita ya Kagera, Uganda ilikua na washirika wengi wakiwamo Libya na mataifa ya Ulaya, Tanzania ilikua peke yake mpaka OAU ya wakati huo ilikwepa kusuluhisha ule mgogoro diplomatically, Tanzania personality all alone waged the entire war with his own little resources. Sasa sina haja ya kuongelea yote hayo.

Ungetakiwa tu umuitikie mdau hapo with neutrality response na sio kutafuta namna ya kuidunisha JWTZ kwa excuses za kishamba, Kwani mbona KDF zaidi ya 100 waliuawa huko kwenye kambi yao Somalia na hao alshabaab mpaka Rais wenu kagoma kutoa idadi kamili ya waliouwawa na hatujaongea, kila siku KDF wanategewa mabomu ya barabarani wanauwawa, mkubali tu kupokea michango ya wadau hata kama inauma, vita haipiganwi kwenye social media.
Hawa jamaa hata kama unawasikitikia lakini wanakera sana, kwao wao kila kinachofanywa na wengine ni rahisi, lakini wanachofanya wao ndio kigumu, kinachowashinda wao, hakuna mwengine atakiweza.

Hawa jamaa katika Dictionary yao, neno humbleness, au kuwa " Muungwana" halipo kabisa. Kwa busara za kibinadamu katika kipindi hiki nchi inaomboleza, hupaswi kuendelea na malumbani hata kama unadhani mtu anakukebehi.

Huyo jamaa ametoa ushauri wake, mtu muungwana angesema tunashukuru kwa ushauri wako tutaufanyia kazi, sio kumjibu kwa kusema vita vya Uganda vilikua rais, Je vya M23, Je vya Msumbiji, Je vya Zimbabwe, Angola na kwengineko note huko ambako JWTZ limeibuka kidedea?.

Muhimu kwa wakenya ni kutafuta ufumbuzi utakaomaliza haya mashambulizi ya Mara kwa Mara, ila kama wanadhani hawawezi kumaliza kwasababu hata France, USA na UK pia wanashambuliwa, basi wakubali kusubiri maumivu yaendelee wakati nchi zingine ziendelee na maisha, kikubwa ni salamu za rambirambi, hizo tutaendelea kuwatumia tu.

Poleni sana watani zetu kwa msiba mzito wa watu 21 hadi sasa. Msitoke kule Somalia kwasababu KDF is very powerful army, litawamaliza Alshabab very soon, by the way so long as Wamarekani na Wafaransa wanauliwa sana na terrorist attacks, kwa wakenya kuuliwa sio kitu cha kushangaza sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa jamaa hata kama unawasikitikia lakini wanakera sana, kwao wao kila kinachofanywa na wengine ni rahisi, lakini wanachofanya wao ndio kigumu, kinachowashinda wao, hakuna mwengine atakiweza.

Hawa jamaa katika Dictionary yao, neno humbleness, au kuwa " Muungwana" halipo kabisa. Kwa busara za kibinadamu katika kipindi hiki nchi inaomboleza, hupaswi kuendelea na malumbani hata kama unadhani mtu anakukebehi.

Huyo jamaa ametoa ushauri wake, mtu muungwana angesema tunashukuru kwa ushauri wako tutaufanyia kazi, sio kumjibu kwa kusema vita vya Uganda vilikua rais, Je vya M23, Je vya Msumbiji, Je vya Zimbabwe, Angola na kwengineko note huko ambako JWTZ limeibuka kidedea?.

Muhimu kwa wakenya ni kutafuta ufumbuzi utakaomaliza haya mashambulizi ya Mara kwa Mara, ila kama wanadhani hawawezi kumaliza kwasababu hata France, USA na UK pia wanashambuliwa, basi wakubali kusubiri maumivu yaendelee wakati nchi zingine ziendelee na maisha, kikubwa ni salamu za rambirambi, hizo tutaendelea kuwatumia tu.

Poleni sana watani zetu kwa msiba mzito wa watu 21 hadi sasa. Msitoke kule Somalia kwasababu KDF is very powerful army, litawamaliza Alshabab very soon, by the way so long as Wamarekani na Wafaransa wanauliwa sana na terrorist attacks, kwa wakenya kuuliwa sio kitu cha kushangaza sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
😂😂 Nami naungana na wewe kuwapa wakenya salamu za rambirambi za style hii, wa marekani wakitwangwa na ISIS na wao wakitwangwa na Alshabaab ngoma droo lakini mtanzania akimtwanga muhasi wa DRC basi vita ni virahisi kule, kaazi kweli kweli
 
Shukran wadau kwa rambirambi zote mlizotupa, binafsi nimepokea nyingi tu kwenye Whatsapp kutoka kwa washkaji ukanda huu, ni dhahiri likija suala la magaidi Afrika mashariki huungana na kuwa wamoja. Hawa watu hawana mipaka, ni mazombi yaliyozaliwa kwa bahati mbaya, yameaminishwa mambo ya kiajabu ajabu, na nia yao huwa kueneza uwoga, ila wakiona jamii inaungana kwa ujasiri na kuwa wamoja dhidi yao, wanahesabu kama hasara kubwa sana.

Hivyo binafsi natoa shukrani kwa majirani wote waliotutumia rambirambi, lakini pia kwa wale kizazi cha nyoka Watanzania wachache waliokesha humu JF wakibeza na kuchekea mauaji yaliyokua yanaendelea, nawapa zoezi rahisi sana, nenda kajiangalie kwenye kioo kwa zaidi ya dakika kumi, ujiulize huyo mtu aliye ndani ya hicho kioo anakutazama, kama ndiye ulikusudia kuishi naye kwa miaka yote ijayo, au anahitaji kurekebisha kitu.

Utani wetu ubaki kwenye mitandao, lakini likija suala linalogusa uti wa mgongo wa jamii yetu, tunafaa kulikemea sote kwa pamoja, ifahamike hii mipaka imechorwa na mzungu na kutupa majina ya kutumia kwenye utaifa.
Mwenyezi Mungu awape faraja. This can happen anywhere
 
Shukran wadau kwa rambirambi zote mlizotupa, binafsi nimepokea nyingi tu kwenye Whatsapp kutoka kwa washkaji ukanda huu, ni dhahiri likija suala la magaidi Afrika mashariki huungana na kuwa wamoja. Hawa watu hawana mipaka, ni mazombi yaliyozaliwa kwa bahati mbaya, yameaminishwa mambo ya kiajabu ajabu, na nia yao huwa kueneza uwoga, ila wakiona jamii inaungana kwa ujasiri na kuwa wamoja dhidi yao, wanahesabu kama hasara kubwa sana.

Hivyo binafsi natoa shukrani kwa majirani wote waliotutumia rambirambi, lakini pia kwa wale kizazi cha nyoka Watanzania wachache waliokesha humu JF wakibeza na kuchekea mauaji yaliyokua yanaendelea, nawapa zoezi rahisi sana, nenda kajiangalie kwenye kioo kwa zaidi ya dakika kumi, ujiulize huyo mtu aliye ndani ya hicho kioo anakutazama, kama ndiye ulikusudia kuishi naye kwa miaka yote ijayo, au anahitaji kurekebisha kitu.

Utani wetu ubaki kwenye mitandao, lakini likija suala linalogusa uti wa mgongo wa jamii yetu, tunafaa kulikemea sote kwa pamoja, ifahamike hii mipaka imechorwa na mzungu na kutupa majina ya kutumia kwenye utaifa.
Kabisa Ugaidi unapaswa kukemewa na dunia yote,gaidi akitaka kutekeleza upuuzi wake aangalia nani ni nani yeye analipua wote so huenda siku ukawa victim so tuukatae upuuzi wa alshabaab
 
Unavyosema ni kweli laiti nasema laiti wangefanya hiyo mission kwa uadilifu. Yaani wasiwabake kina mama wasi kwapue mali zao na wasiue watu wasio na hatia kwani huo unyama wote kuna ushahidi wa video na picha.
Wasomali ni kama wa zanzibari ukitaka vita na mwislam wewe fanya ufisadi kwa kuwa dhalilisha wanawake na uislam kwa ujumla. Nasema serikali ya kenya kwenda somalia sio kosa, kosa ni matendo yao ya hovyo. Natoa pole tena kwa wafiwa wote.
Bro
-yaani watoke kwenye un mission?!!!
-Wakitoka itasaidia nini somalia na dunia??
Kenya ikitoka inawapa guarantee ya usalama kama jirani ya somalia???
Umewahi kujua lengo la al -kaeda?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unavyosema ni kweli laiti nasema laiti wangefanya hiyo mission kwa uadilifu. Yaani wasiwabake kina mama wasi kwapue mali zao na wasiue watu wasio na hatia kwani huo unyama wote kuna ushahidi wa video na picha.
Wasomali ni kama wa zanzibari ukitaka vita na mwislam wewe fanya ufisadi kwa kuwa dhalilisha wanawake na uislam kwa ujumla. Nasema serikali ya kenya kwenda somalia sio kosa, kosa ni matendo yao ya hovyo. Natoa pole tena kwa wafiwa wote.

Sent using Jamii Forums mobile app
usizungumzie udhalilishaji wa wanawake boss ,unakijua kilichosabisha zanzibar kufungua vyuo vya kufunda wanandoa????tafuta ripoti itakusaidia!!!!
 
Asante kwa pole ila huo ushauri wako ni vigumu kuutekeleza maana umewashinda hata Marekani na Urusi kule kwenye ugomvi wao na ISIS, ifahamike vita vyenu na Amin vilikua rahisi sana, vita dhidi ya utawala wa Amin ambao ulikua umechokwa na wananchi wa Uganda ikiwemo hata baadhi ya wanajeshi wake walikua wamemchoka, hivyo ilikua ni kumkomoa akaikmbia nchi mapema, kingine ni kwamba yeye na wafuasi wake walikua waoga wa kifo, hawakua wanajitoa mhanga au itikadi wala nini, walikua wanapora na kutoweka.

Lakini vita vya kisasa unapigana na adui aliyejificha ndani ya raia, amejifunga mabomu na yupo anatamani sana afe akapate thawabu aliyoaminishwa. Hapo kwanza anawaua raia wasiokua na hatia ili kusudi afe na wengi, wewe kama askari komando unategemewa umuondoe humo ndani kwa kutumia ujuzi na kuhakikisha hausababishi maafa ya raia wema.

Kingine, KDF hawawezi kwenda kibabe pale Somalia na kumimina risasi, lazima wawe makini kwa kuhakikisha uungwaji mkono na raia wa kawaida, maana propaganda zikienezwa kwamba wapo kule kuwaua raia, basi wengi watajiunga kwenye kujitoa mhanga dhidi yao, vita vya kisasa sio vifaru na mabunduki tu, ila vinahitaji mikakati ya kijamii na kujua jinsi ya kupata ushirikiano kutoka kwa wote.
Unakuta kundi la wazee wanachunga mbuzi malishoni, hawana ugomvi na mtu wapo kwenye mazungumzo yao, lakini ukiwapa mgongo ghafla unashtuka kumbe ni mashababi na humo kwenye mifugo wameficha silaha za kila aina. Sasa michezo kama hii inahitaji kuwa na mashushu wanaokusaidia kupata taarifa, ila na wao wakikamatwa huchinjwa kama mbuzi.
acha visingizio vya kitoto nina uhakika wakenya wengi wanajua ripoti ya sweet secrets: sugar smuggling and state formation in kenya,which is written by Denish professor from Roskilde university kuhusu kenya (KRA.KDF,POLICE,KBS,magavana,wafanyabiashara mpaka kaka wa rais)
wanavyoshirikiana kuingiza sukari haramu toka brasil.kwa taarifa yako sukari hii inayopitia bandari ya kismayu to kenya through garisa ilikuwa na road block 5 ,tatu za al shabaab na mbili ni za KDF ambazo kila road block moja inaingiza 1.5bn ksh (30 bn tsh) a year mathematically kenya imechangia al shabaab 4.5 bn kshs(90bn tshs) for 3 roadblocks na fedha hizo ndizo zimeua ndugu zetu 21 wa kenya juzi. Sisi kama watanzania tumeathirika na sukari hiyo ambayo KBS ilisema ina mercury,upelelezi wa tz ulikamata baadhi ya sukari hiyo mpakani Sirali na Mtukula but mlipiga kelele tz haitaki biashara na sisi,tutaingizaje uchafu wa brazil wa sh 1200tsh ili uje uue viwanda na wakulima wetu????wewe ni shahidi hali ya wakulima wenu wa miwa ni tete na Mumia is almost dead because of this selfishness.umafia wenu wa sukari umeingia mpaka bunge letu eti zanzibar ina sukari ya kuiuzia bara kumbe ni huo uchafu wenu wa al shababu.inasikitisha kuona ndugu zetu wamekufa hali sisi tuko hai na ndiyo tunachangia mfuko wa fedha wa al shabaab.
 
Back
Top Bottom