Natamani nimuache, ila....

Natamani nimuache, ila....

Sikiliza long distance wa brandy alafu utajua cha kufanya
 
Nenda ukamtembelee huko alipo
 
Duh! Yaani yupo busy hadio anashindwa kupokea simu za mpenzi wake?! Sitaki kuwa mnafiki bana, kama ulivyotangulia kusema; jamaa ameshakuchoka huyo!! Now, it's up to you, kama unajifanya kujua kupenda sana, then endelea kuishi kwa matumaini, otherwise, get prepared!

Labda nikuulize kitu kimoja! Umeshawahi kuachwa?! Kama hujawahi, basi ogopa kuachwa!! Rules of Thumb ni kwamba; kila siku uache wewe na sio kuachwa! How can u always handle it? Unatakiwa kuwa mtaalamu wa kusoma alama za nyakati! Hakuna mtu ambae anaacha ghafla tu kama kuzima kwa kibatari! Lazima kwanza kutakuwa na viashiria vidogo vidogo kuonesha kwamba jamaa si yule wa siku zote! So, ukishaona hivyo, usijisumbue kutaka ku-rescue love....hakuna kitu kama hicho labda kwenye ndoa! UKishaona viashiria vya kuachwa basi wewe fanya haraka kumwacha huyo mwenzo wako kabla hajakuacha rasmi! Unajua ukifanya hivyo nini kitatokea?
1. Mapenzi ni kitu kimoja cha kipumbavu sana! Hata kama jamaa alitaka kukuacha, ukitangulia wewe kumwacha; itamuuma ile mbaya!! Unamwacha si kwamba humpendi, la hasha bali unaamua kuchukua maamuzi magumu! Kwavile unampenda, utaumia sana, tena sana! Lakini baada ya muda, a month or more utasahau tu! Lakini, wakati wewe unaumia kuacha, mwenzako atakuwa anaumia kuachwa!
2. Jamaa kama hakuwa na nia ya kukupiga chini, trust me baada ya kuona unamtema; lazima arudi kwako kukubembeleza na mapozi yake yote yataishia kwenye mapum.bu! Lakini hata kama alitaka kukupiga chini lakini hana ubavu wa kuvumilia maumivu, trust me; atakujia tu!!

Na kishampiga chini jamaa, please; SEE ME!!
 
heee tena akisha muacha NasDaz aje kwako sikiliza qeen Kan mapenzi ni kambi ya jeshi kuna shida, dhiki lakini yote hayo hufanywa kudepend mafanikio kwa hivo usikate tamaa jitahid kushinda ukishindwa utaendelea na vita vyengine kwani utashinda na silaha moja tooo nayo ni "subra" sio peke yako unopata shida ya long distanceri mie wa pili ila mie yangu ni hatari maana country to country but subra ndo itanifanya nishinde
 
Last edited by a moderator:
kaa chini sema naye kwa herufi kubwa hapa umepotea maana yeye mwenye tatizo unakuta hajui kwa kuwa busy na kukkuandalia maisha mazuri kuwa anakukwaza
 
Sema umepata mwingine Bwana, acha kutufanya sisi ni misukule. Muda wote huo uko naye leo ndo unakuja na story isiyokuwa na mkia wala mguu??????
Wanaume wakishapigamo basiiiiiii
 
Sema umepata mwingine Bwana, acha kutufanya sisi ni misukule. Muda wote huo uko naye leo ndo unakuja na story isiyokuwa na mkia wala mguu??????
Wanaume wakishapigamo basiiiiiii

Basi labda nimekupata wewe
 
Back
Top Bottom