Nataka kununua Gari aina ya IST

Bloze

Member
Joined
Nov 15, 2023
Posts
23
Reaction score
56
Wadau habari zenu..

Mimi ni mdada sijawahi kumiliki gari, ndo nataka kununua gari yangu ya kwanza
Nataka ninunue toyota IST old model.

Naombeni ushauri wenu.. ipi ni njia bora kuagiza nje au ninunue showroom za hapa bongo.

Na je, IST ya mwaka gani ndio bora zaidi. Na kampuni gani ni nzuri kuagiza gari?

Note: sitaki kununua gari za mkononi.
 
1. Hongera.
2. Chaguo zuri sana.
3. Agiza nje. Faida zake ni nyingi.
4. IST mwaka wowote nzuri ila make sure ni 1.3L FWD achana na 1.5L AWD
5. SBT au Beforward

Kuongezea:
6. Tafuta silver au nyeupe.
7. Anzia kuangalia ushuru kwanza ujue mwaka gani (2002 hadi 2007) una ushuru mdogo ndio huo mwaka katafute online.
8. Usiishie kutafuta tu cheapest online, angalia na hali ya gari (kwa kukagua Auction Sheet na Condition Report, kama hawana izo achana nalo ilo).
 
Kuagiza ni salama zaidi. Tembelea kwa mawakala wa kuaminika wa kampuni za kuagiza gari nje ya nchi kama vile Beforward kulingana na Mkoa uliopo ( Nimependekeza hii kwakuwa nimewahi kufanya nao kazi).
Kama ni mara ya kwanza usijitose mwenyewe online kuagiza gari maana kuna Wanaijeria wametapakaa huko kwaajili ya kuwapiga watu wanaoingia kichwa kichwa.
NB:
Fika ofisi zao physically
 
Hapa umemaliza mkuu
 
Hapa umemaliza mkuu

FWD ina maanisha ni front wheel drive au ni four wheel drive??
 
Ushauri mzuri kabisa..mleta uzi kama ukihitaji msaada zaidi wa kitaalamu na kuagiza kwa kampuni hizo karibu inbox huduma ni BURE.
 
www sbtjapan com au www.japanesevehicles.com
 
Okay.. so hiyo ya cc 1300 fwd na cc 1500 fwd tofauti ni nini?
Hapo kwenye engine displacement (cc) ni somo jingine, ila kwa ufupi engine displacement (cc) ni kiasi cha hewa na mafuta kinachoweza kuingia kwenye silinda za injini. Ikiwa kubwa (cc nyingi), engine inatoa nguvu zaidi.
Hiko kiasi kinapimwa kwa sentimita za ujazo (cc = cubic centimeters). Ni kama ukubwa wa mapafu ya injini.
Ila we just nunua IST ya cc 1,300 (1.3L)
 
Oooh okay asante sana kwa ushauri.
 
Mtoa mada umefanya chaguo Sahihi kabisaa maana kama ni gari yako ya Kwanza IST ndiyo chaguo maana baada ya kupata uzoefu na IST utajua elimu kubwa ya magari.
Ushauri wangu ni Bora uagize Kupitia kampuni pendwa za be forward na SBT Japan

All in all hongera Kwa hatua yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…