Natafuta wataalamu wa kupanua

Natafuta wataalamu wa kupanua

heshima yenu wakuu nimefanikiwa kupata vijinoti nikaona bora na mie nitafute banda la kujificha pamoja na wanaonizunguka,, hela yenyewe ya kuunga unga aise nilinunua bati za msauzi nikampa fundi kumbe hakuwa na utaalamu nazo hivyo akaniharibia kanitia hasara kama, kuna mtu anamjua mtaalamu wa kupauwa bati la msauz ani pm asiwe wale wa bei za contractors kwani najenga kwenye squatters angalia kiambatanisho
attachment.php

dah, hii kweli hasara, huyo fundi anatakiwa awe ndani mpaka muda huu!!! wenzako huwa wanafanya hivi kama hana muda wa kusimamia au knowledge ya mambo hayo pia ni ndogo; unatafuta mwanafunzi wa mwaka wa pili unampa laki mbili anasimamia.
 
Kama umeweza kununua bati ya south hukutakiwa kutafuta mtu wa bei poa kiasi hicho; kama unaweza kukusanya ufikishe 1.5m nijulishe kwa pm nikutumie fundi expert anakodishwa hadi mikoani ila ni wa Dar.
Nahisi hawezi kufanya hiyo kazi chini ya bei hiyo kwani kazi zake ni za viwango....
 
Heading yako siyo kabisaa, naona umeamua kufurahisha jukwaa kwa lugha zako tata
 
heshima yenu wakuu nimefanikiwa kupata vijinoti nikaona bora na mie nitafute banda la kujificha pamoja na wanaonizunguka,, hela yenyewe ya kuunga unga aise nilinunua bati za msauzi nikampa fundi kumbe hakuwa na utaalamu nazo hivyo akaniharibia kanitia hasara kama, kuna mtu anamjua mtaalamu wa kupauwa bati la msauz ani pm asiwe wale wa bei za contractors kwani najenga kwenye squatters angalia kiambatanisho

Ili kuepuka kupata fundi mbovu tena, usikubali kumtumia fundi ambaye hujaona kazi yake, cha msingi tembea maeneo karibu na nyumba yako ukiona nyumba imepauliwa vizuri ndio omba namba zake za fundi, kwani kuomba humu utapata vimeo tena.
Pili ujue nyumba hiyo itakughalimu sana kwa sababu itahitaji kufumuliwa yote, gharama ya misumali ya mbao na bati pamoja na mbao itakugharimu tena.
Mafundi wa paa wazuri wapo wengi sana wala si kuhangaika.
 
Mkuu pole kwa hasara iliyokupata, utampata fundi mzuri. Angalia nyumba za jirani ambazo zime ezekwa vizuri na uombe contact za hao mafundi
 
Back
Top Bottom