Natafuta kazi ndani ya mkoa wa DSM

Natafuta kazi ndani ya mkoa wa DSM

SELFISH

Senior Member
Joined
Feb 25, 2014
Posts
133
Reaction score
61
Nina FTC ya civil engineering natafuta kazi ya kukaa Dsm tu, nina uzoefu wa kutosha ni zaidi ya miaka 8. Hata ikiwa sio nilio somea sio mbaya.
 
naona unakimbilia mjini ukahonge madem, acha kuchagua mikoa fanya kaz
 
Nina FTC ya civil engineering natafuta kazi ya kukaa Dsm tu, nina uzoefu wa kutosha ni zaidi ya miaka 8. Hata ikiwa sio nilio somea sio mbaya.

Wewe njoo huwezi kosa kazi. FTC Ulisomea wapi. MIST, DIT au ATC.
 
Kuna course zingine ukisoma unakuwa very selective.

Kwamba unatafuta kazi ya kukaa DSM tu.

:msela:
 
Namaanisha nimeshaa zunguka karibia nchi nzima, nimeshindwa hata niwekeze wapi kila mradi ukiisha unahamishwa ndio maana nataka kukaa sehemu moja. nilisoma ATC. Sisi tuko wachache sana na FTC ilishaafutwa.
 
Full technician certificate (FTC) in civil engineering from Arusha Technical College.
 
Utshindwa kusaidiwa sema long form ya ftc

Mkuu labda ni msaidie. FTC ni Full Technician Certificate. Ni elimu ambayo Nyerere aliileta akiiga mfumo wa waingereza na ilikuwa ni kuzalisha mafundi ili waweze kufanya kazi viwandani na za ujenzi kwa ujumla. Kwa lugha nyingine inaitwa Mchundo. Kama umewahi kusikia mafundi Mchundo basi ndio hao.

Kiukweli ilikuwa elimu ngumu sana na ilikuwa inafundisha deeply theory and practical. Ilibadilishwa na kuja katika mfumo wa Diploma miaka 2007 kama sikosei.

Binafsi huwa nawakubali sana FTCs kwakuwa wengi wanajua kazi tofauti na diplomas.
 
Kazi ya kukaa Dsm tu kweli umekosa! Umejaribu kupita vijiweni, beach zote, mabanda ya kupumzikia abiria UBT umekosa kweli.
Basi watakua wameshakuroga maskini.....
 
Et kukaa dsm tuuuu.

Maskini angejua mikoani watu wenye elimu wanavyotanua asingetamani kung'ang'ania mikoani.
Angejenga CV huko kwenye Senior Management levels then akishaunda mtandao anarudi Dsm
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom