Natafuta kazi (Dodoma au Mwanza)

Natafuta kazi (Dodoma au Mwanza)

fahim

Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
54
Reaction score
6
Kwanza pole na majukumu wanajamii. Mi ni mtanzania(me) mwenzenu natafuta kazi ambayo itaniwezesha kujikimu kimaisha nina bachelor ya project planning management&community development.

Sina uzoefu ila ni mchapakazi, moyo wa kujituma na kujitolea panako bidi na mwenye heshima kwawote.

Tafadhali msaada wenu ni muhimu sana nami niweze kujikwamua kwenye hali hii ngumu jamani.

shukrani
 
Kwa bahati mbaya siku hizi ni 20% tu ya kazi hutangazwa. 80% hutolewa kwa "networking" ambapo huenda kwa 20% ya wanaotafuta kazi. Ina maana 80% ya watu wanaotafuta kazi hawajui au hawana networks za kuwapatia kazi.

Kwa mantiki hiyo jamaa yangu nakushauri anza kujenga network hata kwa miaka 2-4. Network inajengwaje?
1. Kujitolea (volunteering) - Kutokana na eneo ulipo nenda kwa mashirika ya umma na yasiyo ya kiserikali wanofanya kazi sawa na ulichosomea, waambie kuwa upo tayari kujitolea kufanya kazi bila mshahara kama sehemu ya kupata uzoefu.

2. Ukibahatika kupata sehemu ya kujitolea fanya kazi kwa bidii na jenga urafiki na watu wa kila aina, huku ukieleza kuwa unatafuta kazi bila kujali ni nani unamwambia

3. Tumia mitandao na mikusanyiko ya kijamii kufahamiana na kujenga urafiki na watu tofauti tofauti. Kama ulisoma mkoa uliopo nenda kwa waliokuwa walimu wako ongea nao kama wanaweza kukupa nafasi kwenye projects zao au kukuunganisha na watafiti wenzao

4. Usikate tamaa. Kazi itapatikana kwa kuwa Hard working and patient. Hata sisi tulipita katika kipindi cha mpito hadi tulipobahatisha kupata kazi.

5. I wish you all the best
 
Pia si lazima ufanye kazi uliyosomea - kuna jamaa yangu alipomaliza Bachelor ya Mech. Engineering UD, nilimshangaa nikamkuta anafuga Nguruwe kibaha kwa sana!!
 
Asante kwa ushauri!, Kwa namna moja au nyingine nimefarijika na umenitia moyo,ila mimi nipo tayari kufanya kazi popote pale, dodoma na mwanza ni pendeleo langu la kwanza,pia sio mpaka iwe kazi niliyoisomea ili mradi iniingizie kidogo nipo tayari kujitolea kama nitapewa chakula na malazi tofauti na hapo nashindwa kwasababu nitakosa mahitaji ya msingi.nawakaribisha tena tafadhali.
 
Kwa bahati mbaya siku hizi ni 20% tu ya kazi hutangazwa. 80% hutolewa kwa "networking" ambapo huenda kwa 20% ya wanaotafuta kazi. Ina maana 80% ya watu wanaotafuta kazi hawajui au hawana networks za kuwapatia kazi.

Kwa mantiki hiyo jamaa yangu nakushauri anza kujenga network hata kwa miaka 2-4. Network inajengwaje?
1. Kujitolea (volunteering) - Kutokana na eneo ulipo nenda kwa mashirika ya umma na yasiyo ya kiserikali wanofanya kazi sawa na ulichosomea, waambie kuwa upo tayari kujitolea kufanya kazi bila mshahara kama sehemu ya kupata uzoefu.

2. Ukibahatika kupata sehemu ya kujitolea fanya kazi kwa bidii na jenga urafiki na watu wa kila aina, huku ukieleza kuwa unatafuta kazi bila kujali ni nani unamwambia

3. Tumia mitandao na mikusanyiko ya kijamii kufahamiana na kujenga urafiki na watu tofauti tofauti. Kama ulisoma mkoa uliopo nenda kwa waliokuwa walimu wako ongea nao kama wanaweza kukupa nafasi kwenye projects zao au kukuunganisha na watafiti wenzao

4. Usikate tamaa. Kazi itapatikana kwa kuwa Hard working and patient. Hata sisi tulipita katika kipindi cha mpito hadi tulipobahatisha kupata kazi.

5. I wish you all the best

Mkuu ushauri mzuri sana..
 
dah hizi kazi jamani mpaka tunachanganyikiwa.mi mwenyewe natafuta pa kujitolea mungu atatuongoza.
 
Kwa bahati mbaya siku hizi ni 20% tu ya kazi hutangazwa. 80% hutolewa kwa "networking" ambapo huenda kwa 20% ya wanaotafuta kazi. Ina maana 80% ya watu wanaotafuta kazi hawajui au hawana networks za kuwapatia kazi.

Kwa mantiki hiyo jamaa yangu nakushauri anza kujenga network hata kwa miaka 2-4. Network inajengwaje?
1. Kujitolea (volunteering) - Kutokana na eneo ulipo nenda kwa mashirika ya umma na yasiyo ya kiserikali wanofanya kazi sawa na ulichosomea, waambie kuwa upo tayari kujitolea kufanya kazi bila mshahara kama sehemu ya kupata uzoefu.

2. Ukibahatika kupata sehemu ya kujitolea fanya kazi kwa bidii na jenga urafiki na watu wa kila aina, huku ukieleza kuwa unatafuta kazi bila kujali ni nani unamwambia

3. Tumia mitandao na mikusanyiko ya kijamii kufahamiana na kujenga urafiki na watu tofauti tofauti. Kama ulisoma mkoa uliopo nenda kwa waliokuwa walimu wako ongea nao kama wanaweza kukupa nafasi kwenye projects zao au kukuunganisha na watafiti wenzao

4. Usikate tamaa. Kazi itapatikana kwa kuwa Hard working and patient. Hata sisi tulipita katika kipindi cha mpito hadi tulipobahatisha kupata kazi.

5. I wish you all the best



Safi sana mkuu Tuko be blessed.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom