Habari zenu wana JF. Nina tatizo ambalo limekuwa likinitesa kwa takribani mwaka sasa. Ninasumbuliwa sana na kiuno yaani ninasikia maumivu makali siwezi hata kuinama kudeki. Nimeshakwenda hospital ya Muhimbili wakanipiga X-RAY lakini halikuonekana tatizo, hivi karibuni nimekwenda regence wakanianzishia physiotherapy nimemaliza lakini nimepata nafuu kwa muda tu. Mpaka sasa sijui tatizo ni nini. Ninakosa raha kwani hata ndoa sienjoy tena. Tafadhari anayejua dawa ya tatizo hili naomba anisaidie. Mungu awabariki.