Nashauri vyeti vya ndoa viwe na kikomo(expire date)

Nashauri vyeti vya ndoa viwe na kikomo(expire date)

magode

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2014
Posts
2,204
Reaction score
3,338
Salaam wana MMU,

Vyeti vya ndoa vinavyotolewa makanisani,misikitini na bomani vyote ni mali ya serikali. Nimejaribu kutafakari jinsi ndoa zinavyokuwa ngumu kila kukicha,kuna watu wanaishi maisha ya mateso sana katika ndoa zao kwa kuheshimu hivyo vyeti wakiamini ni kumkosea Mungu kana kwamba hivyo vyeti ni mali ya Mungu.

Kuepusha madhira yanayoendelea katika ndoa,napendekeza vile vyeti viwe na kipindi cha ukomo ili kuwaokoa watu wengi wanaoona aibu kujitoa katika kifungo cha ndoa.

Wanandoa wakifunga ndoa,wapewe miaka 5 ya matazamio kama mmoja wao katika hiyo miaka 5 atakuwa hajaridhika,anaondoka bila kelele. Kama kila mmoja atakuwa amefurahia maisha,utaratibu utawekwa wa kuongezewa muda.

Huu ni mtizamo wangu kutokana na kile nnachokiona katika jamii. Unaweza kuniona km mpuuzi hapa kwa kuandika haya,lakini yakikukuta utatamani ukiangalie cheti chenu kama kina expire date.

Nawasilisha.
 
NDOA ni zaidi ya CHETI. Kama umemchoka mnaweza kutengana kwa muda. Tatizo ni endapo umeoa mtu usiyempenda, hapa itakula kwako.
 
MWANAKA
Kuna watu wanaishi maisha ya mateso kwa kushika kile walichoelezwa. Huu ni utumwa,na kama ni utumwa lazima sisi km jamii tuagalie namna ya kuwasaidia kuwatoa katika hayo mateso.
 
Last edited by a moderator:
Nyie ndo mlifundishwa ndoa ni kulaliana tu?Unajua maana ya neno kwa shida na raha? Siku zote za maisha yako?Kama hukuwa tayari kuapa hivyo usingepanda altareni.Msichezee taasisi za kiroho.
 
MatikaC
Haswaaa!! Nawashangaa kuna watu eti wanaona kitu cha ajabu! Mbona kuna nchi zimeruhusu ndoa za mkataba!? Binadamu aliyekamilika,anabadilika kutokana na mazingira!
 
Last edited by a moderator:
Bulldog
Mkuu Bulldog hebu niambie ukimkuta mwenzi wako yupo ndani na mtu mwingine utaitaje ni shida au raha!?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu unajua nini maana ya ndoa ? Unapoona appointment za ma CEO wanajali sana marital status unadhani kwa nini ? Kupata kiki ya kugombea urais wanaangalia pia na marital status unadhani kwa nini ?

Wananchi wa Ian Khama wanahuzunika kwamba wanaonekana wana raisi ambaye hajajitosheleza ki mamlaka unadhani kwa nini ? * Ndoa ni kipimo kuwa unaweza kuvumilia,

Kufanya maamuzi magumu kwa kuchuja ipasavyo mawazo unayopewa na watu. Inshort ndoa inakubadilisha take it from me hakuna mtu duniani ambaye habadiliki baada ya kuoa au kuolewa.
 
Kama unaona cheti halali cha ndoa ni mzigo achana nacho. Wewe na mwenzi wako nendeni kwa wakili/mahakamani mkaandikiane huo mkataba wa mahusiano yenye kikomo cha muda na muweke vifungu muhimu vikiwemo vitakavyowalinda watoto wenu baada ya huo mkataba kuisha kama mtapata watoto! LOH! Isipowezekana jiulize kwa nini?
 
Bulldog
Mkuu Bulldog hebu niambie ukimkuta mwenzi wako yupo ndani na mtu mwingine utaitaje ni shida au raha!?

Ndio maana nakwambia ndoa ni taasisi sio ya kuichezea. Utatumia busara kwenye maamuzi.

Shirikisha washenga, wazazi hata viongozi wa dini kutatua kadhia kama hii.
 
Ndoa = Ndoano, uwe tayali kuvua au kuvuliwa kama samaki.
 
Ndio maana nakwambia ndoa ni taasisi sio ya kuichezea. Utatumia busara kwenye maamuzi.

Shirikisha washenga, wazazi hata viongozi wa dini kutatua kadhia kama hii.
Mkuu hiyo misingi unayoisema,ndo hiyo hiyo inawafanya watu waishi kwa mateso,mtu anakubali ushauri wa watu akiamini labda mwenzie atabadilika. Mnarudi hata mwezi hauishi matendo yale yale yaliyosuruhishwa yanarejea. Ndo maana nikasema,km kuna sheria inayomruhusu mtu kutoka itasaidia sana.
 
Ndoa = Ndoano, uwe tayali kuvua au kuvuliwa kama samaki.
Yeah,ndoa ni km kuingiza mkono kwenye chombo usichojua kilichomo ndani yake,ukiona mkono unaumia unautoa! Tatizo jamii inalishwa sumu kwa kuaminishwa kuwa kujitoa kwenye ndoa eti ni dhambi! Lkn jamii hiyo haioni mateso anayopata mtu ktk ndoa. Turekebishe hivyo vyeti.
 
Back
Top Bottom