Napendekeza: kipindi cha dini kingeondolewa mashuleni

Quruxbadan

JF-Expert Member
Aug 12, 2013
232
80
Najua watu wengi mtanichukulia vibaya, kutokana na observation nliyofanya katika muda nliokuepo shuleni, nimeona kua hiki kipindi cha dini kinachokuepo kila ijumaa asubuhi hakifai kabisa kuepo, kinachochea udini na utengano baina ya wanafunzi. Wanafunzi wakiwa huko wanakua brain washed sana, Muislamu anafundishwa kua mkristo ni adui yake na mkirsto nafundishwa muislamu ni adui yake na anatakiwa ampige vita.hawa hawa ndo wanatakiwa wakae darasa moja na kushirikiana katika masomo mbalimbali. Hili si jambo geni ktk shule zetu za serikali. Ikumbukwe kua hawa vijana ndo taifa la kesho ikiwa watalelewa katika misingi ya kuchukiana je hapo baadae nchi yetu itakua katika hali gani??

Nawasilisha kwenu wadau
 
Nafikiri kibaki, angalau Mungu asisahaulike kabisa kwan tunahtaj taifa la wasomi na wenye maadili na hasa wakimheshimu mungu kwan tusipofanya hivo wengi wetu watakulia katika mazingira ya hatari zaidi.
 
Last edited by a moderator:
vile vipindi vya uzaz vibaki na ma concert halafu vya din viondolewe hapo kwa wiki ni mara moja ingekuwa kwa wiki ungesemaje watoto wetu bila kuwalazimisha kumjua mungu utaweza kukitabiri kizaz kijacho na wasiwasi sana na ubongo wako
 
Sitaki kukoment chochote kuhusu huu uzi,najua nikifanya hivyo nitapata ban,hata ¼ mwaka sijatimiza....

Ndugu,chezea akili ya mtu lakini usichezee imani yake....

ANGALIZO...
Futa huu uzi,umekaa kichochezi sana...wenye uelewa wameshanipata...
 
Serikali ina akili sana kuweka kile kipindi, Mungu ni muhimu katika mazingira ya shule. Hivi kweli we umetafakari kwa kina ulichokiandka? Huo uchunguzi umeufanya ktk shule ngapi? Je, wewe ni mpagani, mkristo au mwislam?

Kama wewe ni mpagani, yanayoendelea ktk vipindi vya dini za kikristo au kiislam umeyajuaje? Na je, kama wewe ni mkristo, yanayoendelea ktk dini ya kiislam umeyajuaje? Na kama wewe ni mwislam, yanayoendelea ktk dini ya kikristo umeyajuaje?

We una jambo unalojaribu kuficha. Funguka zaidi tukuelewe, kwani unadhani kama ni kuamasishwa kuchukiana haiwezekani kufanyika ktk nyumba za ibada/kuswalia?

Kama kweli we ni mwalimu by professional napata wasiwasi na taaluma yako.
 
Vya Mungu mpe Mungu.Na vya kaisali mpe Kaisa
Mungu asipolinda mji (masomo) wanafunz wasoma bure.
Tz waislam na wakristo mbna wanaish pa1
 
Nimefundisha mda mrefu sijawahi kusikia wala kuona hayo mafundisho aliyoleta mleta mada.Labda katika shule nyingine.
 
Ninaunga mkono Uzi huu :- ili waumini wa dini zote tuweze kujua na kuelewa " THAMANI YA UBINAADAMU/UTU WETU " kwa akiba ya maneno ni kutambua Heshima na taadhima za MwenyeEzi Mungu kwetu sisi tumeumbwa kwa kukirimiwa hulka,akili, na kutandaziwa ardhii hii tuishii pamoja, Tutafute riziki pamoja kati yetu (kila mmoja anakamilisha duru yake), hapo ndipo inatimia neon ULIMWENGU au DUNIA. Ndipo kutambua Umma huu ni umma mmoja na Mungu ni muumba wetu. STOP !! Tumia njia yeyote lakini at the end of the day tunafika kwake mwenywe wa kwanza na wamwisho. Naomba tukubaliwe kwa matendo yetu mema na misaada kwa jamii. AMINa/Amen
 
We qurux hebu kuwa na stara kidogo,laiti ungalijua neno gaidi lina uzito gan usingalithubutu kultamka hvoo tena kwa kultaja sanjar na uislam,huijui vzur dini na chmbuko lakee,mana sshangai kwa dini hz kuwa na chuki baina yao wakat historia inaonyesha wazwaz kuna chuki na vita mbalmbal za kiiman tangu enzi hzo na mbegu zake mpaka leo znaendelea kuchpua mizizi na mashina,asili haipotei na ndomana udini hutumiwa hadi na magaid ktk kutekeleza adhima yao ya kijasusii,wengi wetu hatusom dini na vitab vnaamrsha nn bali tunacrem tulvofundshwa na wale waliosoma na kuielewa din ktk zana tofauti,hamna dini kat y hz 2 zlizohalalsha dhambi,isipokuwa dhana inakuja kila dini inaamini ynyw ndiyo imesmama ktk haki,hata dini ya illuminant au frimasonia nao wana dhana zao za kuiamin dini yaoo,qurux kuwa mwerev na tafuta dini na uelewe kwa kina,kwan hujawah kusikia ama kushuhudia kuwa kuna padri fulan kasilim ama sheikh fulan kaokoka,?,ushawah kujiulza kwann?,hebu dn isiwe chanzo cha vurugu na vsasii bwana,shulen fuata kile chema unachofundshwa na ndomana Mungu alitupa maarifa ktk kutambua ubaya na wema
 
Najua watu wengi mtanichukulia vibaya, kutokana na observation nliyofanya katika muda nliokuepo shuleni, nimeona kua hiki kipindi cha dini kinachokuepo kila ijumaa asubuhi hakifai kabisa kuepo, kinachochea udini na utengano baina ya wanafunzi. Wanafunzi wakiwa huko wanakua brain washed sana, Muislamu anafundishwa kua mkristo ni adui yake na mkirsto nafundishwa muislamu ni adui yake na anatakiwa ampige vita.hawa hawa ndo wanatakiwa wakae darasa moja na kushirikiana katika masomo mbalimbali. Hili si jambo geni ktk shule zetu za serikali. Ikumbukwe kua hawa vijana ndo taifa la kesho ikiwa watalelewa katika misingi ya kuchukiana je hapo baadae nchi yetu itakua katika hali gani??

Nawasilisha kwenu wadau

Hata katiba ya nchi huijui wewe, ndio wale wale wanaiga kelele bila kuwa na akili ya kufanya mambo. Ila tunashukuru kwa mawazo yako mazuri, ila umechelewa, subiria katiba mpya nyingine ili uweke hayo maoni yako.
 
REKEBISHO.
ni waislam tu ndo wanafundishwa hivyo.
Unataka kiwekwe kipindi cha kigaidi?
Kitawafaa pia hawa wenzetu wakataa nguruwe.

Kwa hiyo kula nguruwe kwako ni sifa? Pig headed. Mtafute msabato atakuelewesha
 
kwa
mujibu wa utetez wako una maanisha kwamba kufundishwa uhasama baina ya
iman tofauti tofauti ndio main agenda ktk vipind vya din kitu ambacho
sio kwel,mkuu kifup hivi vipind ni nguzo mojawapo kuu ambayo ni lazima
ipewe support na wadau wa elim na we ukiwemo kama tuna nia njema na mustakabali
wa maisha yetu nikiwa na maana kua dini ina faida nyingi ktk jamii
 
Kwa mujibu wa dini ya kikristo tunafundisha upendo kuwapenda hata wasio wakristo tena tunafundishwa kusamehe tena 7 mara 70 hatufundishwi kuwachukia wenzetu maana hata yesu alikaa na kula pamoja na wenye dhambi maana bila kukaa nao kwa amani na upendo watawezaje kulijua neno,
Ndg mleta uzi ukizuia kipindi cha dini basi wazuiwe na kwenda kanisani na msikitini? bila shaka wewe ni kati ya wale wanaowaita wenzao makafir.
 
Kwa mujibu wa dini ya kikristo tunafundisha upendo kuwapenda hata wasio wakristo tena tunafundishwa kusamehe tena 7 mara 70 hatufundishwi kuwachukia wenzetu maana hata yesu alikaa na kula pamoja na wenye dhambi maana bila kukaa nao kwa amani na upendo watawezaje kulijua neno,
Ndg mleta uzi ukizuia kipindi cha dini basi wazuiwe na kwenda kanisani na msikitini? bila shaka wewe ni kati ya wale wanaowaita wenzao makafir.

Shule niliyosoma Advance pale Mbeya Waislamu ndio wanabaguliwa. Tena wanafunzi wakristo vipindi vya dini wanaambiwa na Wachungaji(Kwakuona mwenyewe) waislamu wanafuga majini hivyo wawe nao mbali. Unyanyasaji wakidini upo pande zote. Tembea uijue nchi vizuri
 
Nafikiri kibaki, angalau Mungu asisahaulike kabisa kwan tunahtaj taifa la wasomi na wenye maadili na hasa wakimheshimu mungu kwan tusipofanya hivo wengi wetu watakulia katika mazingira ya hatari zaidi.
Hivi siku hizi mungu ni member wa JamiiForum ??
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom