Mbalamwezi1
JF-Expert Member
- Dec 20, 2013
- 2,073
- 2,026
Ni ukweli usiopingika kuwa tanzania kwa sasa ili tuendelee tunahitaji mabadiliko ya kimfumo,kuondoa mfumo wa sasa uliojaa rushwa,urasimu na ufisadi!mabadiliko haya yanaweza kuletwa na aliyepo ndani ya mfumo huu kama atakuwa na nia ya dhati na thabiti ya kutaka mabadiliko, au mabadiliko hayohayo yanaweza kuletwa na mtu ambaye ataingia ktk mfumo wa sasa kutokea nje kabisa!Hivyo basi yeyote kati ya wagombea wa urais anaweza kuleta mabadiliko kikubwa ni nia na dhamira ya dhati ya kutaka kuleta mageuzi ya kimfumo!Tuache ushabiki na mahaba niue kwa wagombea hawa tusikilize sera tuchambue tuone kama zinatekelezeka!Tuonane Oktoba 25.