DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Mgombea ubunge wa Jimbo la Mtama na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, amesema suala la Katiba mpya limeingizwa katika Ilani ya CCM 2025/30 kama sehemu ya dhamira ya chama hicho kuhakikisha mchakato huo unasimamiwa kwa mujibu wa taratibu.
Akizungumza Alhamisi, Oktoba 2, 2025, katika mkutano wa kampeni wa mgombea urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, uliofanyika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid jijini Arusha, Nnauye amesema Katiba si nyaraka za uchaguzi pekee bali ni mwongozo wa maisha ya wananchi wote.
“Katiba haitungwi kuwa Katiba ya uchaguzi, inatungwa kuwa Katiba ya maisha ya watu. Tukiiandaa kwa ajili ya uchaguzi tutakuwa tumetunga Katiba ya uchaguzi. Hii ndiyo busara iliyosababisha CCM kuingiza suala la Katiba mpya kwenye Ilani yake ya uchaguzi,” amesema Nnauye.
Ameongeza kuwa Watanzania wanapaswa kuitumia fursa ya kupiga kura Oktoba 29, 2025, ili kuchagua mchakato utakaosimamia uandaaji wa Katiba mpya, huku akisisitiza kuwa wanaopinga hatua hiyo wana haki ya kutojitokeza lakini wasiwazuie wananchi wengine kushiriki.
“Tarehe 29 ukienda kupiga kura, unapiga kura kuhakikisha mchakato wa Katiba mpya unasimamiwa. Tumpigie kura mwanademokrasia wa kweli, Dkt. Samia Suluhu Hassan,” amesema.
Pia Soma:
Akizungumza Alhamisi, Oktoba 2, 2025, katika mkutano wa kampeni wa mgombea urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, uliofanyika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid jijini Arusha, Nnauye amesema Katiba si nyaraka za uchaguzi pekee bali ni mwongozo wa maisha ya wananchi wote.
“Katiba haitungwi kuwa Katiba ya uchaguzi, inatungwa kuwa Katiba ya maisha ya watu. Tukiiandaa kwa ajili ya uchaguzi tutakuwa tumetunga Katiba ya uchaguzi. Hii ndiyo busara iliyosababisha CCM kuingiza suala la Katiba mpya kwenye Ilani yake ya uchaguzi,” amesema Nnauye.
Ameongeza kuwa Watanzania wanapaswa kuitumia fursa ya kupiga kura Oktoba 29, 2025, ili kuchagua mchakato utakaosimamia uandaaji wa Katiba mpya, huku akisisitiza kuwa wanaopinga hatua hiyo wana haki ya kutojitokeza lakini wasiwazuie wananchi wengine kushiriki.
“Tarehe 29 ukienda kupiga kura, unapiga kura kuhakikisha mchakato wa Katiba mpya unasimamiwa. Tumpigie kura mwanademokrasia wa kweli, Dkt. Samia Suluhu Hassan,” amesema.
Pia Soma:
- Nape: Anaehoji utu wa Rais Samia anajitoa ufahamu
- Nape: Wale wenye mashaka na Samia waache porojo za barabarani