mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,410
- 4,988
Nape Nnauye, amesema wanaompinga Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, wanapaswa kuja na takwimu na si maneno matupu.
Nape amesema tangu alipoingia madarakani mwaka 2021, Dkt. Samia ameweka rekodi ya kipekee ya uadilifu katika kusimamia rasilimali za taifa na kuzitumia kwa manufaa ya wananchi wote.
Akihutubia wananchi wa Moshi Mjini kwenye mkutano mkubwa wa kampeni za Dkt. Samia, Nape alieleza kuwa kiongozi huyo amedhihirisha uwezo wa kipekee wa kusimamia makusanyo ya fedha za serikali na kuhakikisha zinaelekezwa moja kwa moja kwenye miradi ya maendeleo.
Hatua hiyo imeleta mwamko mpya wa uwajibikaji na imani kwa wananchi kuwa rasilimali zao zinatumika ipasavyo.
Nape amesema tangu alipoingia madarakani mwaka 2021, Dkt. Samia ameweka rekodi ya kipekee ya uadilifu katika kusimamia rasilimali za taifa na kuzitumia kwa manufaa ya wananchi wote.
Akihutubia wananchi wa Moshi Mjini kwenye mkutano mkubwa wa kampeni za Dkt. Samia, Nape alieleza kuwa kiongozi huyo amedhihirisha uwezo wa kipekee wa kusimamia makusanyo ya fedha za serikali na kuhakikisha zinaelekezwa moja kwa moja kwenye miradi ya maendeleo.
Hatua hiyo imeleta mwamko mpya wa uwajibikaji na imani kwa wananchi kuwa rasilimali zao zinatumika ipasavyo.