MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 710
Jana, kwenye Taarifa ya Habari ya ITV, Nape Nnauye alionekana akizungumzia kuhusu suala la maadili.
Alisema kwamba CCM haitasita kuwawajibisha viongozi wanaokiuka maadili ya uongozi. Kimsingi alisema watakaobainika kwenda kinyume na maadili watawajibishwa ipasavyo. Nadhani alikuwa anagusia suala la IPTL-ESCROW!
Kama Nape alitaka kuwafurahisha "wajinga waliwao" kule Lindi, basi aliwapata wengi, lakini sisi tunaoujua ukweli, tunajua kwamba hizo ni "porojo" na "hadithi za Alinacha".
CCM ilikataa kata-kata suala la maadili kuwapo kwenye rasimu ya katiba inayopendekezwa. Hoja zote za maadili zilinyofolewa na Sitta wa Viwango na Mwendokasi, tena kwa mwendokasi wa ajabu!
Sasa kama suala la maadili halipo kwenye katiba, litakuwaje kwenye maagizo, ilani na masharti ya uongozi ya CCM?
Jaribu tena Nape. Hapa kwangu hupiti.
Alisema kwamba CCM haitasita kuwawajibisha viongozi wanaokiuka maadili ya uongozi. Kimsingi alisema watakaobainika kwenda kinyume na maadili watawajibishwa ipasavyo. Nadhani alikuwa anagusia suala la IPTL-ESCROW!
Kama Nape alitaka kuwafurahisha "wajinga waliwao" kule Lindi, basi aliwapata wengi, lakini sisi tunaoujua ukweli, tunajua kwamba hizo ni "porojo" na "hadithi za Alinacha".
CCM ilikataa kata-kata suala la maadili kuwapo kwenye rasimu ya katiba inayopendekezwa. Hoja zote za maadili zilinyofolewa na Sitta wa Viwango na Mwendokasi, tena kwa mwendokasi wa ajabu!
Sasa kama suala la maadili halipo kwenye katiba, litakuwaje kwenye maagizo, ilani na masharti ya uongozi ya CCM?
Jaribu tena Nape. Hapa kwangu hupiti.