Tetesi: Nape Nnauye kufukuzwa uanachama wa CCM

Status
Not open for further replies.

Barakaeli174

Senior Member
Aug 2, 2015
171
142
Wana Jf,

Nape Nauye anaandaliwa mtego ili afukuzwe na uanachama kwa kiherehere chake kama wanavyodai, lazima afahamu kwanini Sophia Simba alifukuzwa ni kwa maneno yake ya kupinga...

Sasa Mwenyekiti wa chama kasema ana sauti kubwa na akisema anasema yeye ndio Mwenyekiti. Namuomba kaka yangu Nape awe makini sana, asiongee lolote kuanzia muda ambao alipokea baruwa ya kuachishwa uwaziri. Namsihi awe makini achunge sana mdomo wake, awe na akiba ya maneno.
 
Nape bado anasafari ndefu kisiasa ukichanganya na maisha aliozoea nikwamba hawezi kujichanganya ktk hili
 
hayo ni maruweruwe kaka...Nape ni Mwanasiasa mkomavu sana...na ana ngozi ngumu sana...kwa tunaomfuatilia toka kwenye siasa za UVCCM ana historia inayojitosheleza...ni muhimu aongeee hili kuweka kumbukumbu sawa na baada ya hapo abaki mtazamaji!
 
Na akijipendekeza, akakanyaga miwaya anafukuzwa kweli, na kisha haiwi kitu..
Lkn hapa tunaona matukio yanayoshabihiana na yale ya ufisadi, na baadae, utakaso, na utakatifu, na uadilifu wa "mzee wa kimasai"..
Nape aliefungia bunge kuonekana mubashara, yaonekana kashakuwa "masiah" wa wakosa msimamo....
 
aaaa...nimeamini "ZIMWI LIKUJUALO HALIKULI UKAKWISHA"
sipati mkuu vasco da Gama huko msoga bay anasikitikaje.
Pia baba kinana mbona hatukuoni ukijitokeza kuokoa jahazi linalozidi kujaa
maji kiasi cha kuanza kupoteza uzania (EQUILIBRIUM) au wataka yatokee yale ya
meli ya Titanic ndipo uibuke..?? Tafadhari sana naomba ujitokeze kokote kule uliko
mshitue na babu philip Mangula
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom