Kitendo cha katibu mwenezi wa ccm kuisema serikali yake kimekuwa kikinitatiza sana. Mara ya kwanza nilimuona akikagua majengo ya Udom na kuanza kukandia eti yamejengwa chini ya kiwango. juzi kwenye tv tbc nimemwona akizungumzia ugomvi wa madaktari na serikali ambapo alishauri eti wakae meza ya mazungumzo.Ninachojiuliza mtoto wako unapoona nidhamu yake mbovu huwa unaenda kumtangaza barabarani? au unamwadhibu ukiwa kama mzazi . iweje huyu mtu anaikosoa serikali yake tena kupitia vyombo vya habari?. Kwangu mimi naona ni usanii uliovuka mipaka yaani serikali inawatafuna wadanganyika Nape anatumwa kupulizia kuonyesha ina huruma na wananchi