Paul Alex
JF-Expert Member
- Jul 14, 2012
- 4,240
- 9,527
Kuna wakati unaona rais akipewa taarifa na kuifanyia kazi papo hapo!
Hili linaweza kuwa jambo jema mara nyingine ila kuna wakati linaweza kuwaumiza watu!
Sijui ufikiri wa wengi kwenye hili ila kwenye nchi zetu hizi ndogondogo rais anakuwa almost 'semi-god'.
Rais alipaswa kuwa kama judge mahali fulani kwenye uongozi wake, 'sio kwa kudukua sms za watu lakini!'.
Kama kuna jambo tata la kufanyia maamuzi rais anapaswa kuzisikiliza pande zote kwa busara na kutoa uamuzi.
Mimi naona hata hao watu wanaompa taarifa mara nyingi wanaweza kumlisha matango pori tu hata bila ya wao kujua ukitegemea na hiyo taarifa wameipata wakiwa upande gani wa jambo- (Obsevars au active participants au na wao wamesikia tu kutoka watu ambao nao wanawaamini).
Rais anaweza pia kutokuingia kwenye makosa mengi ya kimaamuzi kama ataacha hierarchy (bottom-up) ifanye kazi yake. Kuharakisha kufanya maamuzi ni jambo moja na kufanya maamuzi sahihi ni jambo lingine.
Maamuzi ambayo yanaumiza watu au yanagusa maisha ya watu wengi yanapaswa yafanye kwa busara kubwa ambayo inatanguliwa na sikio linalosikia pande zote.
Tumeshuhudia watu wakifukuzwa kazi kwa maamuzi ambayo sio sahihi.
Kampuni zikisimamishwa kwa maamuzi ya kuwahi.
Watu wakifilisiwa kwa maneno tu yanayomponyoka rais.
Rais akishaongea mara nyingi kama sio mara zote ndio inakuwa mwisho wa jambo.
Waitaliano hupenda kusema "ROMA LOCUTA CAUSA FINITO". Yaani Roma ikishaongea ndio mwisho wa jambo.
Shida inakuja pale ambapo Roma inaponyokwa tu na maneno.
Tuanze kwa kusema rais aandaliwe hotuba na wakati wote aongee kilichoko kwenye hotuba.
Halafu tutafute namna ya kumbana rais afanye kazi kama taasisi na sio kujiwakilisha yeye mwenyewe tu na kutumia rasilimali zetu kujaribia mawazo yake! (Katiba mpya)
Karibu..
Sent using Jamii Forums mobile app
Hili linaweza kuwa jambo jema mara nyingine ila kuna wakati linaweza kuwaumiza watu!
Sijui ufikiri wa wengi kwenye hili ila kwenye nchi zetu hizi ndogondogo rais anakuwa almost 'semi-god'.
Rais alipaswa kuwa kama judge mahali fulani kwenye uongozi wake, 'sio kwa kudukua sms za watu lakini!'.
Kama kuna jambo tata la kufanyia maamuzi rais anapaswa kuzisikiliza pande zote kwa busara na kutoa uamuzi.
Mimi naona hata hao watu wanaompa taarifa mara nyingi wanaweza kumlisha matango pori tu hata bila ya wao kujua ukitegemea na hiyo taarifa wameipata wakiwa upande gani wa jambo- (Obsevars au active participants au na wao wamesikia tu kutoka watu ambao nao wanawaamini).
Rais anaweza pia kutokuingia kwenye makosa mengi ya kimaamuzi kama ataacha hierarchy (bottom-up) ifanye kazi yake. Kuharakisha kufanya maamuzi ni jambo moja na kufanya maamuzi sahihi ni jambo lingine.
Maamuzi ambayo yanaumiza watu au yanagusa maisha ya watu wengi yanapaswa yafanye kwa busara kubwa ambayo inatanguliwa na sikio linalosikia pande zote.
Tumeshuhudia watu wakifukuzwa kazi kwa maamuzi ambayo sio sahihi.
Kampuni zikisimamishwa kwa maamuzi ya kuwahi.
Watu wakifilisiwa kwa maneno tu yanayomponyoka rais.
Rais akishaongea mara nyingi kama sio mara zote ndio inakuwa mwisho wa jambo.
Waitaliano hupenda kusema "ROMA LOCUTA CAUSA FINITO". Yaani Roma ikishaongea ndio mwisho wa jambo.
Shida inakuja pale ambapo Roma inaponyokwa tu na maneno.
Tuanze kwa kusema rais aandaliwe hotuba na wakati wote aongee kilichoko kwenye hotuba.
Halafu tutafute namna ya kumbana rais afanye kazi kama taasisi na sio kujiwakilisha yeye mwenyewe tu na kutumia rasilimali zetu kujaribia mawazo yake! (Katiba mpya)
Karibu..
Sent using Jamii Forums mobile app