Naombeni ushauri

kaduchu

Member
Joined
Jun 15, 2014
Posts
80
Reaction score
29
Habari wana JF,
Kwanza napenda kumshukuru mwenyezi mungu kwa kunipatia kazi mwaka huu wa 2014, pili natoa shukrani zangu za dhati kwa jukwaa hili kwa kunipatia updates zote kwa miaka miwili niliyokua kwenye msoto mkali wa kutafuta kazi.

Amini usiamini mwenyezi mungu ndio muweza wa yote, ndio mjomba wa wale wasio na wajomba wa kuwapachika maofisini, ndio mwenye cheo kupita vyeo vyote vya hao wanaowapachika watoto wao maofisini wakiwaacha watoto wa wakulima wakiendelea kuangaika.wewe mtoto wa mkulima kama mimi, ukimtegemea mungu na kuzidisha jitihada basi umepona.

Turudi katika mada

nimeangaika kwa muda wa miaka miwili nikifanya interview hapa na pale hatimaye mwaka huu mungu akafungua milango ya ajira kwangu. Ilikuwa ni mwezi wa saba mwaka huu ndipo nilipoitwa kazini halmashauri fulani hapa nchini, mpaka kufikia sasa nina wiki tatu kazini.

Tatizo linakuja kuwa nilikuwa nimeshafanya interview kwenye taasisi ya serikari mojawapo hapa nchini jana nikapigiwa simu niripoti kazini, nikifikiria huku nachukua TGS D ambayo take home ni chini ya laki 4, na huko nilikoitwa uhakika wa take home ya laki 7 na nusu ninao.



SWALI LINAKUJA : Naagaje huku niliko? na je inaruhusiwa kutoka serikarini kwenda serikarini kwa nafasi ya entry level kama yangu?
Nisaidieni nifanye maamuzi sahihi jamani, hasa wenye experience na suala kama hili
 
ubwani na chochote hapo cha msingi wahi haraka sana kwenye shirika la umma achana na tamisemi..
 
Vuta subra watakuja
wazoefu kakini usisahau kufuata taratibu ambazo kimsingi ndio hua zinamfanya MTU arudishwe kazini kama aliko enda kumebuma. Wakumbuke wasio jiweza kama sadaka kwa MUNGU WETU.
 

Weka aina ya kazi zote ulizoitiwa, ya sasa na uliyoitiwa, then one will be in a position to advise wisely.
 
Weka aina ya kazi zote ulizoitiwa, ya sasa na uliyoitiwa, then one will be in a position to advise wisely.
nimeitwa kwa nafasi ya muhasibu daraja la pili, na huku halimashauri nipo kwa nafasi hiyo hiyo
 
Kama bado hawajakuweka kwenye payrol halmashauri....wahi shirika la umma haraka ongea na hr wake uweke mambo sawa
 
Vuta subra watakuja
wazoefu kakini usisahau kufuata taratibu ambazo kimsingi ndio hua zinamfanya MTU arudishwe kazini kama aliko enda kumebuma. Wakumbuke wasio jiweza kama sadaka kwa MUNGU WETU.
nashukuru sana kwa ushauri wako. japo hizo taratibu ndo sizijui sasa. naogopa hata kuuliza kwa wafanyakazi wenzangu hapa kwa sababu sijawajua kiundani wasije wakaja kua vikwazo. ndio maana nikaleta mada humu. naombeni mnisaidie huo utaratibu
 
nashukuru sana kwa ushauri wako. japo hizo taratibu ndo sizijui sasa. naogopa hata kuuliza kwa wafanyakazi wenzangu hapa kwa sababu sijawajua kiundani wasije wakaja kua vikwazo. ndio maana nikaleta mada humu. naombeni mnisaidie huo utaratibu

Mkuu kwa wiki tatu utakuwa tayari umeingizwa kwenye acha tu kusumbuka kwenda huko kwa sababu hutapata mshahara.
 
nazidi kupokea ushauri jamani. hasa kama kuna mtu amewahi kukutana na suala kama hili
 
shirika la uma haliingiliani na tanisemi..

ndio maana hata mishahara yao hailipwi na hazina. ndio maana wana scale zao tofauti.

sina imani kwamba wafanyakazi wa tanesco, tra, nssf, tpa nao wapo kwenye payroll za hazina.

dogo kama no shirika la uma nenda karipoti kisha omba udhuru wowote hata wa kufiwa ( ua mtu yoyote ambae ameshafariki) au jifanye mgonjwa then fanya uchaguzi sahihi..
 
asante mkuu, na mimi najuaga hivyo lakini kuna wadau wananitisha wanadai serikari ni serikari tu kama nikienda huko sitapata mshahara
 
Nitafute kweny no 0713836878ntakupa ushaur vzr ata mim nafanya kaz kweny shirika la serikali kuna watu wanahamia toka tamisemi na check namba zao zile zile.
 
Nitafute kweny no 0713836878ntakupa ushaur vzr ata mim nafanya kaz kweny shirika la serikali kuna watu wanahamia toka tamisemi na check namba zao zile zile.
mkuu acha uchoyo weka humu wote tufaidike
 
wewe bado hata hujamaliza probation period na ulipewa ikipindi cha mwaka cha matazamio wajulishe kwa siku 30 ,au soma standing Orders D 57 na D 58
 
hapo kama ni serikar tu serikar si kaz ngumu unaomba kubadkisha kurungenz tuuu kutoka.idara uliopo kwenda idara unayoenda.
kwa barua na utafankiwa
 
umepewa comfirmation latter kama bado aaaaaaah unasubir nini kimbia
 

Acha kumdanganya mleta mada.Nani kakwambia tamisemi na SU haviingiliani?
Sawa kila sehemu wana scale zao lkn wote wanalipwa na hazina ya serikali.na payroll ni moja
tu.
Hata mimi nilikuwa najua hivo lakini nimekosa kazi SU kisa nshaingia payroll kupitia TAMISEMI.
Aliyempa ushauri mzuri ni yule alomwambia kmameshaingia payroll asihangaike kwenda tena serikalini idara nyingine lbda akahamishe datasheet kwa ruhusa ya mwajiri.
Lakini akienda kinyemera siku anaingizwa payroll kule SU jina litagoma kwenye system ya LAWSON
 
asante mkuu, na mimi najuaga hivyo lakini kuna wadau wananitisha wanadai serikari ni serikari tu kama nikienda huko sitapata mshahara

Huyo anakupoteza.iwe tamisemi.tra.tanesco n.k wote ni serikali na wapo payroll moja.Sema ufate taratibu uhamishe datasheet vingnevyo hutoingia payroll mara ya pili.Kama unabisha nenda lkn kuna siku utarudi hapa kuniambia lbda ubadili majina kitu ngumu sana.
Mimi ni shahidi nimetoka tamisemi kutaka kuja duce.ilikuwa mbinde hadi leo hakijaeleweka karibia mwaka.Tatizo nshafutwa payroll lkn system inanitambua tu.Na kitu nilichokuja kujua na sishauro mtu ufanye ni kuondolewa payroll ya serikali aisee kurudi utasota.
 
Niikua naomba kujua DUCE ni shirika la umma au ni chuo cha serikali au sababu ,scale zipo tofauti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…