ELcapitano Maestro
Member
- Dec 12, 2020
- 14
- 34
"Niliwahi kuwa katika Mahusiano na binti flani ambae nilidumu nae katika mahusiano kwa mwaka mmoja na nusu.
Sasa baada ya miezi 7 ya mahusiano kuna siku huyo binti aliniambia ana mimba, kwa kweli nilishtuka juu ya taarifa hio lakini nikajisemea moyoni kuwa kama ikiwa yangu nitalea, japo sikuwa tayari kuwa na mtoto kipindi hicho.
Sasa baada ya kuchunguza na kumbana sana kwa maswali na kutaka twende kupima yule binti akasema kuwa hana mimba alitaka kunipima tu ajue nitasemaje, ili chukua kama siku tatu hivi ndo akaja kusema ukweli huo kuwa hana mimba.
Basi maisha yakaendelea, sasa baada ya kupita miezi mingine 8 akaja kusema huyo binti kuwa...hivi sasa ana mimba yangu kweli, mimi nikawa na mkatalia alivyoona vile akawaambia ndugu zake wa kike wawili wakanipigia simu wakawa wananitishia kuwa ile mimba ya mdogo wao ni yangu na kila kitu wanajua kuhusu mimi, japo mi kusikia hivyo lakini mimba niliikataa.
Wakati huo nilikuwa nimesafiri kidogo nilienda mkoa mara moja sasa nilipanga nikirudi nikamchukue huyo binti nikampime, lakini hilo sikuwaambia ila nilikuwa naendelea kukataa kuwa ile mimba si yangu.
Nilichofanya nika M-block kwa muda yule bint nione atafanya nini, alichofanya akawa ananitafuta kwa namba nyingine huku akisema kuwa nina ana mimba yangu.
Sasa mimi nikarudi zangu dar, nikamcheki yule bint lakini wimbo ukawa ni ule ule kuwa ana mimba, sasa mimi nilichofanya nikawa namwambia si yangu basi akawa anatukana sanaa lakini mimi nilisimamia msimamo ule ule.
Sasa yule binti akaona isiwe kesi ikabidi aniambie kuwa anataka nimpe pesa kisha aongezee na yake ili akatoe hio mimba mi nikamwambia kuwa sina hela.
Sasa mimi nikawa naendelea sana kumbana na kutaka aseme ukweli ilipita kama mwezi na wiki 2 akaja kusema mimba ile imetoka, hivyo anataka yaliyopita tuyasahau tuanze maisha mapya na akalia sanaa kuwa ananipenda mi nikamsamehe lakini sikutaka kuonana nae kwanza.
Baada ya kumsamehe ikapita kama wiki, sasa ikawa anaradhimisha sana tufanye ule mchezo huku akisema kuwa amenimiss sanaa, na kila siku wimbo ni huo huo, mi nikajiuliza mbona anataka sanaa japokuwa mwanzoni alikuwa akisema amenimiss mi huwa najiongeza chap, lkn sasa hivi imekuwa too much nikaona hii si kawaida.
Kwakuwa yule bint ananipenda sanaa nikatumia mwanya huo kwa kumbana na maswali ili kutaka aseme ukweli kuwa kwann anataka sana tufanye tendo na muda wote maongezi ni hayo hayo...Sasa baada ya kumbana sanaa akaja kusema ukweli kuwa aliambiwa na wale ndugu zake kuwa aje aniwekee dawa ya mapenzi ili nimpende yeye tu, akanitumia hadi picha ya hio dawa ambayo alitaka kuja kuniwekea...daah nikachoka kabisa, lakini aliomba msamaha sanaa kuwa hajakusudia kufanya hivyo ila ni ndugu zake waliomshawishi hivyo ni msamehe sanaa.
SASA NAOMBENI USHAURI NIFANYAJE!???
Sasa baada ya miezi 7 ya mahusiano kuna siku huyo binti aliniambia ana mimba, kwa kweli nilishtuka juu ya taarifa hio lakini nikajisemea moyoni kuwa kama ikiwa yangu nitalea, japo sikuwa tayari kuwa na mtoto kipindi hicho.
Sasa baada ya kuchunguza na kumbana sana kwa maswali na kutaka twende kupima yule binti akasema kuwa hana mimba alitaka kunipima tu ajue nitasemaje, ili chukua kama siku tatu hivi ndo akaja kusema ukweli huo kuwa hana mimba.
Basi maisha yakaendelea, sasa baada ya kupita miezi mingine 8 akaja kusema huyo binti kuwa...hivi sasa ana mimba yangu kweli, mimi nikawa na mkatalia alivyoona vile akawaambia ndugu zake wa kike wawili wakanipigia simu wakawa wananitishia kuwa ile mimba ya mdogo wao ni yangu na kila kitu wanajua kuhusu mimi, japo mi kusikia hivyo lakini mimba niliikataa.
Wakati huo nilikuwa nimesafiri kidogo nilienda mkoa mara moja sasa nilipanga nikirudi nikamchukue huyo binti nikampime, lakini hilo sikuwaambia ila nilikuwa naendelea kukataa kuwa ile mimba si yangu.
Nilichofanya nika M-block kwa muda yule bint nione atafanya nini, alichofanya akawa ananitafuta kwa namba nyingine huku akisema kuwa nina ana mimba yangu.
Sasa mimi nikarudi zangu dar, nikamcheki yule bint lakini wimbo ukawa ni ule ule kuwa ana mimba, sasa mimi nilichofanya nikawa namwambia si yangu basi akawa anatukana sanaa lakini mimi nilisimamia msimamo ule ule.
Sasa yule binti akaona isiwe kesi ikabidi aniambie kuwa anataka nimpe pesa kisha aongezee na yake ili akatoe hio mimba mi nikamwambia kuwa sina hela.
Sasa mimi nikawa naendelea sana kumbana na kutaka aseme ukweli ilipita kama mwezi na wiki 2 akaja kusema mimba ile imetoka, hivyo anataka yaliyopita tuyasahau tuanze maisha mapya na akalia sanaa kuwa ananipenda mi nikamsamehe lakini sikutaka kuonana nae kwanza.
Baada ya kumsamehe ikapita kama wiki, sasa ikawa anaradhimisha sana tufanye ule mchezo huku akisema kuwa amenimiss sanaa, na kila siku wimbo ni huo huo, mi nikajiuliza mbona anataka sanaa japokuwa mwanzoni alikuwa akisema amenimiss mi huwa najiongeza chap, lkn sasa hivi imekuwa too much nikaona hii si kawaida.
Kwakuwa yule bint ananipenda sanaa nikatumia mwanya huo kwa kumbana na maswali ili kutaka aseme ukweli kuwa kwann anataka sana tufanye tendo na muda wote maongezi ni hayo hayo...Sasa baada ya kumbana sanaa akaja kusema ukweli kuwa aliambiwa na wale ndugu zake kuwa aje aniwekee dawa ya mapenzi ili nimpende yeye tu, akanitumia hadi picha ya hio dawa ambayo alitaka kuja kuniwekea...daah nikachoka kabisa, lakini aliomba msamaha sanaa kuwa hajakusudia kufanya hivyo ila ni ndugu zake waliomshawishi hivyo ni msamehe sanaa.
SASA NAOMBENI USHAURI NIFANYAJE!???