Naombeni ushauri wa haraka

Naombeni ushauri wa haraka

KIDHEHA

Member
Joined
May 21, 2012
Posts
51
Reaction score
14
Habarini mimi ni kijana nina miaka arobaini, nilikuwa na mwanamke nikazaa nae watoto wawili tukaachana kwa sababu za kutoelewana na mimi na ndugu majirani, kiufupi ni mwanamke mgomvi sana hawezi ishi na ndugu jamaa au marafiki, alishakalishwa sana na hakujirekebisha.

Sikua na ndoa nae na tangia tumeachana ni miaka mitatu. Nashangaa kila baada ya muda namkumbuka na kutaka kurudiana nae wakati huohuo ndugu hawataki hata kumsikia kwa sababu ya tabia zake za kutoweza jirekebisha.

Naombeni ushauri nifanyeje nimsahau kabisa ili niweze tafuta mwingine.

Na huyo mwanamke wala nilikuwa simpendi kiivyo ni ujana tu ulinisukuma ila sikuwa na mapenzi nae sana.

Ushauri tafadhali.
 
Ndio mpenzi wako wa kwanza nini?
Inawezekana umemiss tabia zake...
 
Ukiona hivyo ujue bado una mapenzi naye...lol
 
Inawezekana.ile ile tabia yake ya ugomvi ndo unayompendea
 
Mkuu KIDHEHA, tatizo lako wewe huna msimamo na maamuzi yako na ndio maana bado unapata mawazo ya kumkumbuka na kutaka kurudiana nanye. Waswahili wanasema "Ukitaka kumuua nyani, usimwangalie usoni" lakini pia waswahili wanasema "Mwenye macho haambiwi tazama." Wakati ungali bado unaweza kupenda jihadhari usije ukapenda kama kipofu.

Fikiria sana uone kama maisha yako na yule unayemchagua kuwa mwenzi wako wa maisha yatakuwa ya furaha ama ya kutopatana na kuhuzunisha baada ya harusi. Wanawake na wanaume wengi wameoana kana kwamba jambo la pekee lililowapasa kulijali ni kuwa wanapendana au la. Kuchagua mwenzi wa maisha kwafaa kufanywa kwa busara ili kuwawezesha wazazi na watoto pia, kuwa na hali nzuri kiroho, kiakili na kimwili.
 
Tatizo haujielewi licha ya umri kukutupa mkono wewe sio kijana tena huo umri wako unatosh kusimamia mambo yako

ngoja niishie hapa tu
 
Mwenzako keshaenda sumbawanga kukufanyia kazi umrudie. Ndio maana kila mara anakujia kichwani. Maombi ni kinga
 
Kweli JF ni jungu la ushauri. Lakini sikiliza:
Umezaa naye watoto 2. Jiulize, una moyo mgumu kiasi gani hata usiwakumbuke watoto wako hao? Unakula kikapita kweli wakati watoto wako wanalelewa na mzazi mmoja?
Jiulize:
Huo ushauri wa kupokea kwa ndg zako ati hawataki kumsikia, unamtwaa muwe naye au naye na nduguzo? Kitandani mlilala yeye na weye na nduguzo mpaka ukapata watoto 2?
Mke ni wako sio wa ndugu zako. Wao wana wake zao, hata siku moja hawajakukaribisha mtumie wote. Acha upofu, unampenda sana huyu mama watoto tena ugomvi wake ni kwa vile alikuwa anataka uachane na hao wanaokufundisha muachane naye.
Ushauri:
Kamtwae mama watoto wako kabla hajatwaliwa na watu wengine ukalia kilio cha mbwa ukiyaona malovee yake kwa huyo mbahatika.
 
Ningeomba JF watoe mwongozo wa mashart ya ushaur wa haraka. Nimekuja mbio nikajua mtu katekwa mabwepande.
 
hahahaha. ..na wewe ni kijana,? cc rubii
 
Last edited by a moderator:
Kwanza wanaokubeza hujitambui nawaona ujinga unawasumbua tu. Ingekua ni dereva wewe uko DUI, hauko driven on your senses. U dont need lobotomy, control your medulla! Usitake mtu akuongoze maisha ya furaha yako!

40 kwa bongo unaonekana mzee, majuu (Nz) mzee anaanzia 80, so sawa tu kutokujua nako ni kujifunza
 
Habarini mimi ni kijana nina miaka arobaini, nilikuwa na mwanamke nikazaa nae watoto wawili tukaachana kwa sababu za kutoelewana na mimi na ndugu majirani, kiufupi ni mwanamke mgomvi sana hawezi ishi na ndugu jamaa au marafiki, alishakalishwa sana na hakujirekebisha.

Sikua na ndoa nae na tangia tumeachana ni miaka mitatu. Nashangaa kila baada ya muda namkumbuka na kutaka kurudiana nae wakati huohuo ndugu hawataki hata kumsikia kwa sababu ya tabia zake za kutoweza jirekebisha.

Naombeni ushauri nifanyeje nimsahau kabisa ili niweze tafuta mwingine.

Na huyo mwanamke wala nilikuwa simpendi kiivyo ni ujana tu ulinisukuma ila sikuwa na mapenzi nae sana.

Ushauri tafadhali.

Ndugu miaka 40 bado unajiita #Kijana? Kweli? Aisee huu ubakaji wa umri utaisha lini?

Seriously!
 
Habarini mimi ni kijana nina miaka arobaini, nilikuwa na mwanamke nikazaa nae watoto wawili tukaachana kwa sababu za kutoelewana na mimi na ndugu majirani, kiufupi ni mwanamke mgomvi sana hawezi ishi na ndugu jamaa au marafiki, alishakalishwa sana na hakujirekebisha.

Sikua na ndoa nae na tangia tumeachana ni miaka mitatu. Nashangaa kila baada ya muda namkumbuka na kutaka kurudiana nae wakati huohuo ndugu hawataki hata kumsikia kwa sababu ya tabia zake za kutoweza jirekebisha.

Naombeni ushauri nifanyeje nimsahau kabisa ili niweze tafuta mwingine.

Na huyo mwanamke wala nilikuwa simpendi kiivyo ni ujana tu ulinisukuma ila sikuwa na mapenzi nae sana.

Ushauri tafadhali.

Ndugu miaka 40 bado unajiita #Kijana? Kweli? Aisee huu ubakaji wa umri utaisha lini?

Seriously!
 
Ataishi na wewe au na ndugu? Unaolea ndugu mke?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom