Naombeni msaada watanzania wenzangu

Danah

Member
Joined
May 9, 2014
Posts
19
Reaction score
5
Habari zenu jamani. Mimi ni mtanzania nilieamua kuja kufanya kazi huku Oman kutokana na ugumu wa maisha. Ila sasa nimeamua nirudi nyumbani kutokana na maumivu makali ya mgongo yatokanayo na kazi nyingi nifanyazo.

Hivyo nikaomba kurudi nyumbani Tanzania, wamenikubalia lakini wanataka nilipe gharama zao ambazo ni milion moja pia nijilipie nauli.

Kwa kweli watanzania wenzangu mimi sina uwezo huo, ningekua nao nisingekua huku leo. Naomba tu wana jamii wenzangu mwenye kuguswa na hili anisaidie niweze kurudi nyumbani, sina cha kuwalipa zaidi ya asante tu, naamin na Mungu atawabariki sana.

Naombeni msaada wenu. Natanguliza shukrani zangu za dhati kwenu na Mungu awabariki. Asanteni.
 
Pole sana mkuu mungu atakubariki utarundi salama.

lakn kaa ukijua huo ndio uanaume siyo uanaume wa dar wakupigwa na wanawake na kukimbia wototo wandogo kisa panya road
 
wanaume wa dar eti wana matatizo ya panya road mpaka wamekimbia wake zao
 
Pole sana mkuu mungu atakubariki utarundi salama.

lakn kaa ukijua huo ndio uanaume siyo uanaume wa dar wakupigwa na wanawake na kukimbia wototo wandogo kisa panya road

poti kenehe mhola?
 
Pole sana mkuu mungu atakubariki utarundi salama.

lakn kaa ukijua huo ndio uanaume siyo uanaume wa dar wakupigwa na wanawake na kukimbia wototo wandogo kisa panya road

Amekwambia yeye ni mwanaume?
 

Tutakuaminije?
 
ndugu yangu toa maelezo ya kutosha na vielelezo vyake tutakuaminije kwani siku hizi matapeli ni wengi
n a wengi wanakuja kwa njia mmbalimbali sana na gia za kila namna za kutapeli hivyo kuwa muwazi zaidi
 

Wewe ni mwizi na tapeli la kinageria lililojifunza kiswahili. Watanzania ni wajanja huwapati ng'oo! Mpuuzi wewe!
 
Toa maelezo zaidi, utasaidiwa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…