Naombeni msaada wa kimawazo

Naombeni msaada wa kimawazo

yorkshire

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2016
Posts
2,533
Reaction score
3,175
Habari zenu mandugu!!!...

Bila kuwachosha naomba niende moja kwa moja kwenye lengo husika la kuanzisha uzi huu .Siku 7 zilizopita mdogo wangu alitumiwa hela na mama yetu mdogo ambaye yupo dar ,alimtumia kiasi fulani cha pesa kwa ajili ya mambo ya shule sasa bahati mbaya sana laini ya simu aliyotumia haikuwa imesajiliwa kwa jina lake pia haikumbuki vema namba zake na isitoshe laini hiyo alijisahau akaitafuna mdomoni akidhani anatafuna kitu ni siku mbili baada ya kutumiwa.

Sasa shida imekuja kuwa ile laini haisomi pia namba yake aliyotumiwa hela dogo haikumbuki vema na isitoshe mama mdogo nae haikumbuki tena maana hakuisave .Tumejaribu kuwapigia huduma kwa wateja Tigo pesa ili watusaidie kwa hili wanadai mpk namba hiyo iwepo ndo tusaidike sasa nikasema ngoja nilete kwenu huenda tukapata suluhisho maana humu kuna wajuzi wa kila namna
 
Nenda...ofisi za tigo ambazo upo karibu nazo
 
Nenda...ofisi za tigo ambazo upo karibu nazo
Sasa ukienda hapo tigo watakuuliza namba ya hiyo laini then kitambulisho ambacho kimesajiliwa kwa namba hiyo jambo ambalo halitakuwa na majibu ....kumbuka ametumia laini ambayo imesajiliwa kwa jina jingine tu ambalo halikumbuki .Dogo alimuomba hela Ma mdg katika normal situation sana na hakutarajia kama kweli angemtumia na yeye ma mdg hakumuuliza amtumie dogo kwenye namba ipi
 
Piga *150*.. whether ni tigo au mpesa then angalia statement yako utaona miamala yako ya mwisho utaipata hyo namba then piga customer care ya kampuni yako waombe kurudsha muamala
 
Mama mdogo apige simu huduma kwa wateja au aendr ofisi za tigo zilizo karibu aeleze kiasi alichotuma na awaeleze vizuri muamala urejeshwe kwake
 
Mwambie mama mdogo aangalie transaction history yake ataiona hiyo namba kisha akienda kwenye kuda la service provider wake ataomba ku reverse muamala urudi kwake alafu hapo mtatafuta njia nyinge ya kutumiana.

Uzuri ni kuwa line haijapotea kusema labda hela inaweza ikatolewa bila nyie kujua.
 
Mamdogo aende ofisi za tigo awaeleze kiasi alichotuma wacheki transaction zake watarudisha pesa kwake kisha ataituma tena kwenu kwa namba mtakayompa
 
Habari zenu mandugu!!!...

Bila kuwachosha naomba niende moja kwa moja kwenye lengo husika la kuanzisha uzi huu .Siku 7 zilizopita mdogo wangu alitumiwa hela na mama yetu mdogo ambaye yupo dar ,alimtumia kiasi fulani cha pesa kwa ajili ya mambo ya shule sasa bahati mbaya sana laini ya simu aliyotumia haikuwa imesajiliwa kwa jina lake pia haikumbuki vema namba zake na isitoshe laini hiyo alijisahau akaitafuna mdomoni akidhani anatafuna kitu ni siku mbili baada ya kutumiwa.

Sasa shida imekuja kuwa ile laini haisomi pia namba yake aliyotumiwa hela dogo haikumbuki vema na isitoshe mama mdogo nae haikumbuki tena maana hakuisave .Tumejaribu kuwapigia comester care tigo pesa ili watusaidie kwa hili wanadai mpk namba hiyo iwepo ndo tusaidike sasa nikasema ngoja nilete kwenu huenda tukapata suluhisho maana humu kuna wajuzi wa kila namna
Kwanza, wambie huyo mdogo wako aache tabia ya kutafuna ovyo vitu, siku atatafuna visivyotafunika. Pili kama mama'ako mdogo haikumbuki namba hiyo ajaribu kukumbuka kama hakutuma pesa kwenye namba nyingine katika kipindi hicho, hiyo inaweza kusaidia kama atakwenda tigo lakini kama aliendelea kutuma kwenye namba zingine basi hesabuni maumivu...
 
Mwambie mama mdogo aangalie transaction history yake ataiona hiyo namba kisha akienda kwenye kuda la service provider wake ataomba ku reverse muamala urudi kwake alafu hapo mtatafuta njia nyinge ya kutumiana.

Uzuri ni kuwa line haijapotea kusema labda hela inaweza ikatolewa bila nyie kujua.
CASE SOLVED....!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom