Naombeni msaada ndugu zangu

Naombeni msaada ndugu zangu

M nason

Member
Joined
Nov 17, 2015
Posts
8
Reaction score
0
Habari wanajf. Naitwa Mariam ni mwanafunzi wa diploma ya ualimu wa msingi ktk Chuo kimoja hapa Dar,Niko mwaka wa 1 ndio tumeanza juzi tu..Maisha Yangu yamekua ya changamoto nyingi na mapito magumu sana lakini Mungu ni mwema mwaka huu nikapata mfadhili wa kunisomesha ualimu akawa amenilipia ada kwa semester ya kwanza tu,bahati mbaya sana huyu msamaria Mungu amempenda zaidi ametangulia mbele za haki kiukweli nimechanganyikiwa mnoo Nina uchungu mwingi sana moyoni kwani sijui hatma ya masomo Yangu. Hivyo ndugu zangu naombeni msaada wenu kupata mfadhili wa kunisaidia ada katika semester mbili zilizobaki au mchango wowote,sitohitaji pesa ya mtu mkononi Bali iingizwe moja kwa moja kwenye acc. Ya Chuo,au hata kupata kibarua cha aina yoyote kile cha kufanya baada ya muda wa masomo saa 7mchana ili kinisaidie kujilipia ada pasipo kumtegemea mtu. Naombeni mnisaidie ndugu zangu kiukweli nimekata Tamaa kabisa ya maisha kwani hii elimu ndio ilikua kilakitu kwangu,Atakayeguswa no. Zangu ni 0677 123322. Ahsanteni sana
 
Ungekuwa wazi nafikiri hilo ombi lako lingesikilizwa,inavyooneka wewe siyo muwazi unaposema chuo kimoja dar unakuwa na maana gani?taja chuo na jina lako kamili ili upate kusaidiwa.
 
Ungekuwa wazi nafikiri hilo ombi lako lingesikilizwa,inavyooneka wewe siyo muwazi unaposema chuo kimoja dar unakuwa na maana gani?taja chuo na jina lako kamili ili upate kusaidiwa.

Kweli kabisa,Tutajuaje kama kweli ni mwanafunzi.Ataje chuo tumhoji vizuri then tumsaidie
 
Kwanza kwa sentens zko inaonyesha moja kwa moja ww sio female ni male .taja jina la chuo na jina lako kamili,au km vp karibu Mombasa.
 
Ungekuwa wazi nafikiri hilo ombi lako lingesikilizwa,inavyooneka wewe siyo muwazi unaposema chuo kimoja dar unakuwa na maana gani?taja chuo na jina lako kamili ili upate kusaidiwa.
Okay.. Naitwa Mariam nasson. Nipo Al-Haramain Teaching college. Hujui ni kwa kiasi gani nahitaji msaada that's why nikaweka hadharani mawasiliano Yangu ili kama mtu ana nia ya kunisaidia anipate na nimweleze zaidi
 
Ndugu zangu asanteni kwa mawazo yenu. Nipo Al-Haramain teaching college. Hamjui tu ni kwakiasi gani nahitaji msaada wenu
 
Kwanza kwa sentens zko inaonyesha moja kwa moja ww sio female ni male .taja jina la chuo na jina lako kamili,au km vp karibu Mombasa.
Naitwa mariam Nason nipo Al-Haramain teaching college ndugu Yangu hujui tu ni kwa kiasi gani nahitaji msaada
 
Weka account namba ya chuo na P.o.Box za chuo tutakutumia payment slip baada ya malipo. Ada ni sh. Ngapi?
 
Weka account namba ya chuo na P.o.Box za chuo tutakutumia payment slip baada ya malipo. Ada ni sh. Ngapi?
Ada ni laki Tisa na nusu kwa mwaka..nimeshalipa semester ya kwanza laki nne, semester ya pili ni 265,000 na semester ya 3 ni 285,000 Mungu akubariki ndugu yangu
 
Vizuri,msaidieni dada kwakweli ninyi wenye uwezo.Kwani ameweka wazi kila kitu,me nawaamini sn wanajf watamsaidia.
 
Back
Top Bottom