Naombeni mawazo yenu

Naombeni mawazo yenu

Mafikizolo

JF-Expert Member
Joined
May 8, 2014
Posts
3,487
Reaction score
1,626
Habari za mujengoni wana JF!!

Mimi ni msichana nina miaka 20, sasa leo nimekuwa na mawazo,mpaka sasa sijajua nifanye maamuzi gani kwani wazazi wangu wanataka nirudi shule nikarudie form three ili nisafishe cheti changu kiwe pouwa kwani matokeo yangu hayakuwa mazuri.
Mimi nilivyo maliza form four nilisoma short course flani ivi ambayo baadae nilikuaja kupata kazi kwenye shirika flani sema sija ajiriwa direct,nafanya kazi nina mwaka watatu sasa nipo nafanya kazi. Kiukweli mimi nilikua napenda sana kusoma na ninatamani kusoma lakaini sikurudi form three sasa sielewi ni fanye maamuzi yapi kati ya kurudia form three au nitafute chuo kama nitapata nisome kitu ambacho ninaweza hata kujiajiri mwenyewe,nimefikiria nimewaza ila sijapata jibu sahihi nikaona si vibaya kushare na nyie mkanipa mawazo yenu juu ya hili

NB:Nisingependelea matusi kama uwezi kunipa mawazo pita ivi------------------->
 
Usijaribu kuresit inawacost wengi tafuta chuo uanze hata certificate. Ingekuwa vizuri ueleze pia ufaulu wako ili wadau wakushauri vizuri.
 
Kurisiti nikupiga hatua 1 mbele' 3 nyuma! Kama matokeo yako yanaruhusu anza certificate, then diploma na kuendelea!! Kila lakheri!!
 
Hahaha,Dada yangu humu Jf siku zote usiseme hutaki matusi.
Kuna watu wanajulikana kwa kejeli humu watakuja utawasikia.

Ushauri wangu ni kwamba bado mdogo sana na fursa unayo.
Kwanza pata radhi za wazazi,kaanao chini ili uwape ushauri wa utakachofanyia maamuzi.
Tabia ya kurejea mtihani inatakiwa kichwa kiwe kimetulia kweli.
Maana mie kuna dada mmoja amerejea mitihani mpaka akapata mume huko huko,ameolewa na bado Credit moja hajaipata.
Na ukizingatia kwamba wewe Tayari umeishaijua pesa na umeingia kwenye ajira.
Kurejea mtihani inapendeza zaidi mara tu ya kufeli kisha unaunganisha,hapo kichwa kinakuwa vizuri.Au either kungekuwa na Shule maalim kama zilizopo Dar ambazo unatenga muda wa jioni kwenda kusoma na mchana unafanya yako,hapo angalau.
Wazazi wako watakuwa wanajua kwamba ulikuwa unapenda kusoma kama unavyosema wewe mwenyewe na ndio maana wametembea na akili yako na wazo hilo.
Ila tambua kwamba kuna watu wanapenda kusoma lakini ukweli ni kwamba kila wakisoma kichwani hakikai kitu,mie nina shemeji yangu alikuwa anapenda kusoma kupita maelezo,lakini kila akisoma bado uwezo unakuwa sio kabisa licha ya kwamba unamuona yupo busy na masomo,hii ni hekma ya mungu.
Wazo la pili ni kwamba Tambua kwamba unapenda nini,ili ujiunge na chuo kama VETA ili upate taaluma(Professional skils) ili iwe rahisi kujiajiri.Hii nahisi itakusaidia sana kama utakuwa mjanja wa kucheza na fursa
 
Kama ulipata divisin 5 pamoja na ufaulu kushushwa ni bora tu utafute chuo.
 
Thanx a lot my dear. Mimi napenda sana nisomee IT au Udesigner ndo vitu ambavyo napenda sana. Nashukuru kwa ushauli wako nitaufanyia kazi
Hahaha,Dada yangu humu Jf siku zote usiseme hutaki matusi.
Kuna watu wanajulikana kwa kejeli humu watakuja utawasikia.

Ushauri wangu ni kwamba bado mdogo sana na fursa unayo.
Kwanza pata radhi za wazazi,kaanao chini ili uwape ushauri wa utakachofanyia maamuzi.
Tabia ya kurejea mtihani inatakiwa kichwa kiwe kimetulia kweli.
Maana mie kuna dada mmoja amerejea mitihani mpaka akapata mume huko huko,ameolewa na bado Credit moja hajaipata.
Na ukizingatia kwamba wewe Tayari umeishaijua pesa na umeingia kwenye ajira.
Kurejea mtihani inapendeza zaidi mara tu ya kufeli kisha unaunganisha,hapo kichwa kinakuwa vizuri.Au either kungekuwa na Shule maalim kama zilizopo Dar ambazo unatenga muda wa jioni kwenda kusoma na mchana unafanya yako,hapo angalau.
Wazazi wako watakuwa wanajua kwamba ulikuwa unapenda kusoma kama unavyosema wewe mwenyewe na ndio maana wametembea na akili yako na wazo hilo.
Ila tambua kwamba kuna watu wanapenda kusoma lakini ukweli ni kwamba kila wakisoma kichwani hakikai kitu,mie nina shemeji yangu alikuwa anapenda kusoma kupita maelezo,lakini kila akisoma bado uwezo unakuwa sio kabisa licha ya kwamba unamuona yupo busy na masomo,hii ni hekma ya mungu.
Wazo la pili ni kwamba Tambua kwamba unapenda nini,ili ujiunge na chuo kama VETA ili upate taaluma(Professional skils) ili iwe rahisi kujiajiri.Hii nahisi itakusaidia sana kama utakuwa mjanja wa kucheza na fursa
 
zanzibar spices ameshakujibu vizuri.....tehe tehe tehe tehe watu wana majibu humu almost ya kila kitu
 
Nashukuru kwa ushauli ahsante sana
Kurisiti nikupiga hatua 1 mbele' 3 nyuma! Kama matokeo yako yanaruhusu anza certificate, then diploma na kuendelea!! Kila lakheri!!
 
sasa ukirisiti alafu ukafail tena kama mwanzo utamlaumu nani!?
kwann usiendelee na hiyo kazi yako au ushafukuzwa!?
 
Thanx a lot my dear. Mimi napenda sana nisomee IT au Udesigner ndo vitu ambavyo napenda sana. Nashukuru kwa ushauli wako nitaufanyia kazi

Kama ni Web Designing njoo nyumbani kwangu niwe ninakufundisha evening classes.

I look forward to hearing from you soon.
 
Sijafukuzwa ila lazima niangalie na future ya mbeleni sio unaangalia tu hapa nilipo
sasa ukirisiti alafu ukafail tena kama mwanzo utamlaumu nani!?
kwann usiendelee na hiyo kazi yako au ushafukuzwa!?
 
Teh teh nyumbani kwako wapi jamani Sumu
Kama ni Web Designing njoo nyumbani kwangu niwe ninakufundisha evening classes.

I look forward to hearing from you soon.
 
Kama ni Web Designing njoo nyumbani kwangu niwe ninakufundisha evening classes.

I look forward to hearing from you soon.

We SUMU wewe jina lako lenyewe linatisha,unataka kumfundisha kweli au ndio unataka kufanya kama alivofanyiwa ndugu wa Zanzibar Spices alivokuwa anarisiti mpaka akapata na mume hukohuko? Lol
 
Teh teh hahahahahaha inabidi nicheke tu
We SUMU wewe jina lako lenyewe linatisha,unataka kumfundisha kweli au ndio unataka kufanya kama alivofanyiwa ndugu wa Zanzibar Spices alivokuwa anarisiti mpaka akapata na mume hukohuko? Lol
 
Back
Top Bottom