Naombeni majibu juu ya hili kwa yeyote atakayefungua hapa

ISACOM

JF-Expert Member
Jul 22, 2009
543
405
Kuuliza si ujinga.Nataka kujua hivi kama umepata degree ya kwanza halafu ikakuwezesha kupata Masters.Halafu ukagundua kuwa ile first degree yako haina soko na uliamua kubadili ukachukua masters tofauti na ile first degree yako.Je ukiamua kurudi chuo kusoma miaka mingine mitatu kama umri unakuruhusu na ukafanikiwa kupata degree pure nyingine.Swali linakuwa hivi'' hiyo degree uliyoipata kwa awamu ya pili ukiamua kutumia na Masters uliyopata kwa degree ya kwanza itakubalika?Na je kigezo cha kuwa hiyo Masters na degree kupishana miaka,ikionekana Masters imeitangulia miaka degree uliyoombea kazi haitoleta utata?
 
Kuuliza si ujinga.Nataka kujua hivi kama umepata degree ya kwanza halafu ikakuwezesha kupata Masters.Halafu ukagundua kuwa ile first degree yako haina soko na uliamua kubadili ukachukua masters tofauti na ile first degree yako.Je ukiamua kurudi chuo kusoma miaka mingine mitatu kama umri unakuruhusu na ukafanikiwa kupata degree pure nyingine.Swali linakuwa hivi'' hiyo degree uliyoipata kwa awamu ya pili ukiamua kutumia na Masters uliyopata kwa degree ya kwanza itakubalika?Na je kigezo cha kuwa hiyo Masters na degree kupishana miaka,ikionekana Masters imeitangulia miaka degree uliyoombea kazi haitoleta utata?

Kama uliweza pata Masters kwa degree ambayo wewe unadhani haifai, then huna haja ya kufanya tena Bachelor.
Mfano umepata Bachelor ya Engineer lakini baadae ukafanya Master ya
Law then you don't need to do Bachelor of Law!
Pia you can do Bachelor of Arts and the do a postgraduate diploma (equivalent to Masters) in any other subject
 
kwa nini kurudia bachelor tena wakati hiyo uliyokuwa nayo mwanzo ilikuwezesha kupata hiyo masters ya sasa?? nini maana ya kusoma hiyo masters?
 
Nitapenda kuchangia kama ifuatavyo:
1.Unaweza kusoma bachelor hata tatu kwa mapenzi yako na kuendana na knowledge unayotaka kupata.Epuka kusoma kama fashion.Lenga kwenye kutafuta maarifa na pia uangalie matumizi ya hizo degree.

2.Kuna namna mbalimbali za kuji position hata kama degree uliyoipata mwanzo unashindwa kuitumia. Unaweza kuitafutia linkage na masomo mengine maana dunia ya sasa inataka mtu multi-disciplinary na siyo mwenye mtizamo mmoja tu.Mfano, siku hizi kila mtu anakimbilia kusoma Law..ati kwa vile wanadhani inalipa kwa kuwaangalia mawakili wanavyotengeneza pesa! Wanasahau kuwa huko tuendako kuwa na degree ya LLB peke yake si mali kitu... unatakiwa uwe na taaluma nyingine kama Finance, management, medicine, forensic, development management,IT etc. maana specialisation ni muhimu.

Unaweza kusoma kozi fupi fupi kwenye masuala ya afya ya jamii ( public health), environment, HIV/AIDS, POVERTY,Human Rights, NGDOs etc HAYA siyo lazima uyachukulie degree bali waweza kusoma postgrad ukaichanganya na fani yako nyingine uliyoisomea ukajikuta mambo yako ni poa sana.
3. Kuhusu kutumia hizo degree kutafutia kazi, inategemea jinsi utakavyofanya maombi ya kazi na kazi husika zinataka mtu mwenye vyeti gani.Pia unashauriwa kupata uzoefu hata kama ni kwa kujitolea.Watz wengi hawajaielewa concept ya volunteersim na hapa ndipo wenzetu wazungu na wahindi au hata watu wa nchi nyingine za Africa hutupiga bao.Kujitolea bila hata kulipwa kuna faida zake a). Unapata fursa kuingia kwenye taasis na kujifunza chini ya watu mahiri na hapo hapo b). unajenga CV yako kiasi kwamba utakapokuja kuomba kazi ukiulizwa una uzoefu unaweza kujibu kwa ma confudence kuwa unayo.Watu wawe na malengo kila hatua kuanzia kusoma hadi kujiandaa kutafuta kazi.
 
Ungesema kabisa hizo first degree ni zipi na the masters degree ni ipi haswa, si ajabu hutohitaji kufanya first degree nyingine kufukia ile ya mara ya kwanza ili iende sambamba na Masters unayoitaka.
 
Ungesema kabisa hizo first degree ni zipi na the masters degree ni ipi haswa, si ajabu hutohitaji kufanya first degree nyingine kufukia ile ya mara ya kwanza ili iende sambamba na Masters unayoitaka.

"Ilo ni tatizo la watu kusoma kwa kufuata mkumbo, mtu unaenda chuo kikuu hata hujui kwanini unaenda pale au unataka kuwa nani? na kufanya kazi gani katika maisha yako.Lazima kuomba ushauri kabala ya kusoma,na lazima hujue unasomea nini?.Sasa fikiria unasoma 4 years alafu unatafuta njia za kufukia degree ya kwanza, unapoteza muda.
 
Kuuliza si ujinga.Nataka kujua hivi kama umepata degree ya kwanza halafu ikakuwezesha kupata Masters.Halafu ukagundua kuwa ile first degree yako haina soko na uliamua kubadili ukachukua masters tofauti na ile first degree yako.Je ukiamua kurudi chuo kusoma miaka mingine mitatu kama umri unakuruhusu na ukafanikiwa kupata degree pure nyingine.Swali linakuwa hivi'' hiyo degree uliyoipata kwa awamu ya pili ukiamua kutumia na Masters uliyopata kwa degree ya kwanza itakubalika?Na je kigezo cha kuwa hiyo Masters na degree kupishana miaka,ikionekana Masters imeitangulia miaka degree uliyoombea kazi haitoleta utata?


Pamoja na ushauri mzuri wa wanajamvi, nakushauri uache harakati za kusoma ili upate kazi tu (kuwa manamba). Soma kwa mchepuo wenye lengo la kuwa na maarifa ya kukabiliana na changamoto za maisha kwanza na kazi ya kuajiriwa ifuate kama unapenda. Ukiwa na mtizamo wa kusoma ili uwe manamba mkubwa utatumikishwa sana dunia ya sasa. Pole kama nimekuudhi.
 
Nitapenda kuchangia kama ifuatavyo:
1.Unaweza kusoma bachelor hata tatu kwa mapenzi yako na kuendana na knowledge unayotaka kupata.Epuka kusoma kama fashion.Lenga kwenye kutafuta maarifa na pia uangalie matumizi ya hizo degree.

2.Kuna namna mbalimbali za kuji position hata kama degree uliyoipata mwanzo unashindwa kuitumia. Unaweza kuitafutia linkage na masomo mengine maana dunia ya sasa inataka mtu multi-disciplinary na siyo mwenye mtizamo mmoja tu.Mfano, siku hizi kila mtu anakimbilia kusoma Law..ati kwa vile wanadhani inalipa kwa kuwaangalia mawakili wanavyotengeneza pesa! Wanasahau kuwa huko tuendako kuwa na degree ya LLB peke yake si mali kitu... unatakiwa uwe na taaluma nyingine kama Finance, management, medicine, forensic, development management,IT etc. maana specialisation ni muhimu.

Unaweza kusoma kozi fupi fupi kwenye masuala ya afya ya jamii ( public health), environment, HIV/AIDS, POVERTY,Human Rights, NGDOs etc HAYA siyo lazima uyachukulie degree bali waweza kusoma postgrad ukaichanganya na fani yako nyingine uliyoisomea ukajikuta mambo yako ni poa sana.
3. Kuhusu kutumia hizo degree kutafutia kazi, inategemea jinsi utakavyofanya maombi ya kazi na kazi husika zinataka mtu mwenye vyeti gani.Pia unashauriwa kupata uzoefu hata kama ni kwa kujitolea.Watz wengi hawajaielewa concept ya volunteersim na hapa ndipo wenzetu wazungu na wahindi au hata watu wa nchi nyingine za Africa hutupiga bao.Kujitolea bila hata kulipwa kuna faida zake a). Unapata fursa kuingia kwenye taasis na kujifunza chini ya watu mahiri na hapo hapo b). unajenga CV yako kiasi kwamba utakapokuja kuomba kazi ukiulizwa una uzoefu unaweza kujibu kwa ma confudence kuwa unayo.Watu wawe na malengo kila hatua kuanzia kusoma hadi kujiandaa kutafuta kazi.


Hapa JF anafaidi aliye uliza na aliyesoma!
 
Back
Top Bottom