Kwanini magumashi mengi?.
Yeye mwenyewe ndio alikuwa anajaribu ndio maana hajaonekana tena.
OK, magumashi mengi sababu huku kwanza sio rahisi kupata unachokitaka kwa wakati,
Hata ukikipata kwa wakati bado kutakuwa na ugumu kuelewa hicho ulichokipata kwa wakati japo inategemea ni kitu gani.
Kutokana nakuchelewa kupata unachokitaka kwa wakati basi lazima utakuwa umeshapoteza muda mwingi kupata hicho unachokitaka au kupoteza hamu ya kitu chenyewe.
ila kama angeenda youtube ambako huko angesearch hicho kitu anachokitaka angekipata ndani ya sekunde kadhaa na kukielewea sio chini ya dakika 5 au 10, au kama angepitia quora angeuliza hicho anachokitaka angekipata ndani ya muda mfupi kuliko hapa.
Hayo yote yanatokana na jamii ya jamiiforums japo sio wote na hao ambao sio wote ni wachache,
Ukiondoa hao sio wote ambao Ni wachache katika hiyo jamii ya jamiiforums,
Wanaobaki Labda hawana muda na mambo kama hayo anayoyaulizia mleta mada,
Pia labda hawayapendi, labda wanadhani ni utoto, ni kupoteza muda, majukumu mengi, kazi zimewakaba sana, labda wako bize na siasa, au labda wako bize kula/kuliwa tunda kimasikhara sababu hata ule uzi una views karibu mill3, ila angalia Uzi huu.
Na hao wachache waliobaki ndio watakao sababisha kitokee kile nilichokiandika wakati naanza kuandika nilichoandika,
Ila huko kwingine nilikomwambia aende, hao wachache wa huku kule ni wengi.
Pia labda mtoa mada hakuwa anajaribu, labda alikuwa hajui kuhusu magumashi ya huku, hivyo alifuata ushauri wangu kuliko kupoteza muda mwingi hapa, au labda ni mmoja kati ya Jamii ya jamiiforums ukiwatoa hao wachache.
Kwa muono wangu huo, hizo ni sababu chache za magumashi Kati ya nyingi.