Mundamushimu
JF-Expert Member
- Aug 23, 2017
- 752
- 432
Habari wana jf Doctor,
Mimi nina umri wa miaka ....... nina nina mke mmoja watoto 3 na wajukuu 4. Tangu mwaka 2014 nimeanza kusumbuliwa na meno yakaanza kuuma, mpaka 2015 mwezi wa 8 tayari yalikuwa yameng'olewa meno 6. Nikaamua kwenda kupata matibabu zaidi Nkinga Hospital iliyopo mkoa wa Tabora.
Huko meno yalisafishwa yote na kupewa dawa ambazo mwa kiasi fulani zilisaidia. Baadaye likaanza tatizo la kutoa harufu mbaya kinywani, mimi mwenyewe nilijisikia vibaya sana pamoja na usafi wa kuyasafisha meno mara 3 kwa siku kwa dawa za meno. Nilijihisi mpweke kwani nilishindwa kuongea karibu na wenzangu na mke wangu ni kama alinitenga naye alikuwa analala mzungu 4.
Nikaamua kurudi tena Nkinga Hospital, nikapatiwa dawa za kunywa na kusafisha Kunywa. Nashukuru Mungu kinywa kikaacha kutoa harufu. Tatizo ambalo limenipata tena 2017 mwezi wa 6 meno yalianza kulegea pasipo maumivu yoyote, yakapoteza mpangilio kinywani yakawa hovyo hovyo tu na sasa siwezi kutafuna vitu vigumu, kwa kukosa mpangilio nimekuwa naung'ata ulimi mara kwa mara nimeenda mpaka Buhando Hospital lakini dawa ninazopewa hazinisaidii.
Naomba kupitia jukwaa hili kama yupo anayejua dawa anielekeze maana ni mateso kinywa hakitoi harufu tena ila meno yamelegea yote. Asanteni.
Mimi nina umri wa miaka ....... nina nina mke mmoja watoto 3 na wajukuu 4. Tangu mwaka 2014 nimeanza kusumbuliwa na meno yakaanza kuuma, mpaka 2015 mwezi wa 8 tayari yalikuwa yameng'olewa meno 6. Nikaamua kwenda kupata matibabu zaidi Nkinga Hospital iliyopo mkoa wa Tabora.
Huko meno yalisafishwa yote na kupewa dawa ambazo mwa kiasi fulani zilisaidia. Baadaye likaanza tatizo la kutoa harufu mbaya kinywani, mimi mwenyewe nilijisikia vibaya sana pamoja na usafi wa kuyasafisha meno mara 3 kwa siku kwa dawa za meno. Nilijihisi mpweke kwani nilishindwa kuongea karibu na wenzangu na mke wangu ni kama alinitenga naye alikuwa analala mzungu 4.
Nikaamua kurudi tena Nkinga Hospital, nikapatiwa dawa za kunywa na kusafisha Kunywa. Nashukuru Mungu kinywa kikaacha kutoa harufu. Tatizo ambalo limenipata tena 2017 mwezi wa 6 meno yalianza kulegea pasipo maumivu yoyote, yakapoteza mpangilio kinywani yakawa hovyo hovyo tu na sasa siwezi kutafuna vitu vigumu, kwa kukosa mpangilio nimekuwa naung'ata ulimi mara kwa mara nimeenda mpaka Buhando Hospital lakini dawa ninazopewa hazinisaidii.
Naomba kupitia jukwaa hili kama yupo anayejua dawa anielekeze maana ni mateso kinywa hakitoi harufu tena ila meno yamelegea yote. Asanteni.