asante kwa maneno yako mazuri nayaheshimu. sikuwa na nafasi ya kusema kila kitu hapa maana ningechukua nafasi kubwa hata kusoma ungeshindwa.
lakini nimetoa mfano mmoja tu wa mambo anayonifanyia huyo mpenzi wangu wa awali, lakini kuna mengi ikiwa ni pamoja na hata kufukia kuwa na uhusiano wa kimapenzi na rafiki yangu na niligundua hilo na akaomba radhi.
yako mengi lakini pamoja na yote hayo bado nimekuwa mvumilivu mwaka wa sita huu hadi ninapoona kama huko tunakoelekea si shwari na umri wa kuoa unazidi kuyoyoma ndipo nikaona niangalia upande mwingine.
Nimeshakaa naye several times na kuongea naye, tuki-solve kitu leo, after sometime kinarejea upya hadi najikuta nachoka. hadi kufikia kuanzisha uhusiano mpya nimevumilia mengi sanaa toka kwake lakini nimefikia kukata tamaa
[/COLOR]
mpendwa LD umeongea ,maneno ya msingi sana,ubarikiwe,isipokuwa kwa hako ka red tu,du,tumekukosea nini?
Uko kwenye mtanziko mkubwa..ushauri wa kwanza - tulia punguza kabisa mawasiliano na huyu wa pili ili uone reaction yake,usifanye papara.Kwa Huyu wa kwanza jishughulishe na mtoto wako basi, acha aendelee na maisha yake kama ambavyo amekudokeza.
Hakuna jambo baya kama ku-deal na watu wasiojali feelings zako...hawajali kama vitendo wanavyovifanya vinakuumiza au la.Tulia mkuu..mambo mazuri hayataki papara
6 years?? Mlikuwa bado mnafanya nini? Namshukuru saaana huyo dada wa pili.....maana kakuonesha ipasavyo ili siku nyingine uwe na akili na si kuchanganya watu wawili!!
Ni kweli unaweza ukaongea mengi hapa. Lakini natamani tungepata neema ya kumsikiliza na huyo dada pia. Yani hakuna kujihesabia haki hapa. Kama uliona hakufai, ilikuwa ni swala la kumtangazia kuwa hakufai na humpendi na umechoka kuvumilia.
Na unakwenda kuanza mahusiano na mtu mwingine, lakini kama nimekusoma nikakuelewa ni kwamba unawachanganya wote wawili. Ahii kwani umeambia ni Maharage na ubwabwa hata uvichanganye pamoja?
Kwa kweli sipendi maamuzi ya hivi. Huna msimamo kaka unacheza pata potea na maisha ya wadada wa watu?
Thanks Double R, tatizo huyu wa kwanza amebadilika sana hadi nakata tamaa, anadiriki hata kuanzisha kitu kama mradi bila kunishirikisha hata kidogo na nikimuuliza anasema kila mtu ana mambo yake binafsi. Sio kwamba ningemkataza isipokuwa kuniarifu tu ingetosha na zamani hakuwa hivi. Hiyo ndio ikanifanya hata kutafuta ustaarabu mpya pamoja na kuwa tuna mtoto, lakini nashukuru sana kwa ushauri wako
Kaka yangu nimesoma na kukuelewa,kwanza ww ndio ulikosea kuanzia mwanzon kwan inaonekana tangu umemzalisha yule dada hukuonesha msimao japo hata wa kupeleka barua na kujitambulisha achia mbali kuonesha dalili za kuwa muoaji na ndio iliyopelekea kubadilika kwa huyo mzazi mwenzi.
Na naamin hapo ukweli uko wazi kwa hao wadada kuwa mdada wa kwanza ndio wife material ukiachia huyo wa pili kwa sababu hizi;
1.wa kwanza ni mstarabu na mvumilivu kwa kuwa nawe tangu wakatu huo mpaka amefaham una mwingine still hajakutoa nduki
2.wa kwanza pamoja na dharau aliyooneshwa na huyo wa pili kwa msg hiyo hakujibu wala kujibizana naye hata kwa matusi alikuwa mstarabu na kukutafuta na kukuonyesha utumbo wa huyo wa pili,
3.wa kwanza hakuanzisha fujo yoyote baada ya kujua una mwingine ameamua kuwa kimya na kukupokea bila kujali wakati huyo wa pili hata mwaka bado tayari keshalianzisha.
4.wa kwanza ni msaada kwa familia maana hata alipoona huna mwelekeo ameamua kusimama kwa miguu yake ili hata ukisepa aweze kulea mwanae,kwan umeonesha dalili zote za kutokuwa na msimamo,
there for binafsi nakushauri rudi kwa mama watoto wako mnaejuana madhaifu yenu na mmevumiliana kwa miaka yote hiyo na mna mtoto muoane mlee mwanenu acha kuhangaika na micharuo,huyo dada wa pili anaonekana ni muongo na mtu wa shari wakati wote,kazi ni kwako.
Umekaa na mpenzi wako ndani ya miaka 6, tena mmejaaliwa mtoto wa miaka minne! Hujamtamkia mpango wa kumuoa wakati hajaonesha tabia yoyote mbaya. Eti unadai amebadilika! Ngekuwa wewe ungefanyaje?
Umekurupuka na kwenda kutafuta mpenzi mwingine aliyezalishwa na kuachwa bila kujua ni kwa nini aliachwa. Umemuingiza kwenye uhusiano anaanza kuleta malumbano na kuonyesha tabia zake za "uashangedere" bado huoni kama hakufai????
Geuka fastaaaa, rudi kwa yule wa kwanza kamuoe na utulie mtoto wa kiume lol! Inaonekana utafurahia maisha ya ndoa.
Utaacha mtu mzuri na kufuata pakacha! Huyo wa kwanza kwanza kuangalia maisha yake baada ya kukuona huna msimamo! Miaka yote hiyo bila ndoa, unategemea anafikiria nini? Angekuwa mwingine miugomvi isingekatika, na l tell u; anajua una mtu nje hata kabla hajapata hiyo FB message, it shows tu, wanawake huwa tunajua!
Ila nahisi mapenzi Makubwa yapo kwa huyo wa pili! Hana sifa kwakuwa
1. Ni liar
2. Mshari/mgomvi
3. Si mvumilivu (kumbuka uko naye less than a year, na tayari yupo desparate)
Any way Dunia yako, chaguo ni lako!
kabla sijajua wengn wamekushauli vp, naomba tuanze hivi: kwa upeo wangu mdogo niliokuwa nao,kaka jua kwamba mahusiano ya sasa ni bora ubaki na yule mwenye matatizo uliyoyazoea siku zote kuliko kuanzisha upya...utasema unapunguza matatizo unashangaa unakutana na makubwa kuliko yule wa kwanza ulikotoka....pia hebu jaribu kujitambua nani unampenda sana, na utulie na huyo.coz kuwa na wanawake wa wili kwa wakat mmoja utachanganyikiwa zaid af zaid kwenye mazingira km hayo yako ya kusaka chaguo la kuoa...na kingine ni kwamba, wanawake weng wanapenda kujitutumua wa ma bi wakubwa ili waonekane na huyo wa pili anaasili ya uongo hadi hapo amethibitisha hilo...hebu jaribu kuongea na mama watoto wako muulize nn tatzo solve matatizo yenu,tulia kaka. huyo wa pili si mwema kabisa kwa mtazamo wangu.jiunge na wa kwanza funga ndoa leeni mtoto wenu.na pia we kaka umemzalish mtoto wa watu hata kwao hujaenda miaka yote hii kwel?hujtumia busara hapo...inawezeka tena uwezekano mkubwa ukawa umechangia kumbadilisha napo ni baada ya kuona wewe husomek miaka yote hiyo unamwangalia tu huna plan yoyote...achana na huyu wa pili tulia na wa kwanza utakutana na makubwa utabaki unajuta...for more ushaur just find me
Pamoja mkuu,mungu akusaidie ufanye maamuzi sahihi kwa maisha yako na hata watoto wako pia ili siku moja wasije wakakuuliza ni kwa nn uliwachagulia mama wa ajabu!!!Nakushukuru sana kwa maoni yako yameniingia akilini na nimekusoma kwa mstari. Once again thanks a lot for such constructive advices. I appreciate!