Naomba ushauri ndugu zangu

Naomba ushauri ndugu zangu

Joined
Apr 1, 2021
Posts
57
Reaction score
51
Poleni na majukumu ndugu zangu,

Nianze Kwa kumshukuru Mungu muumba wa mbingu,nchi na vilivyomo. Kuna habari njema nimeipokea ila imekua na walakini Kwa moja ya washauri wangu,Kwa muda sasa yapata miaka miwili nimekuwa natafuta kazi/ajira na sikuweza kufanikiwa kupata kazi ya matamanio yangu ila nimeishia kupata kazi za kinyonyaji mno Hadi Leo hii mwenyezi Mungu kaniona.

Leo asubuhi nimepata email kutoka kwenye kampuni ya SHELL yenye makao makuu mjini London Uingereza kabla ya barua ya Leo (employment offer) nilipokea tena barua ya kukubaliwa ombi la kazi(kumbuka kwenye tangazo la kazi ilikua ni graduate training program and employment) mnamo December 30,2021 iliyonitaka nijaze taarifa zangu baadhi kama leseni ya udereva na vinginevyo,na badae niliisaini na kuituma kabla ya saa 48 zao kuisha na nilifanyia hivo.

Hivyo basi ninavyoandika hapa Leo nimepokea form ya ajira na taarifa zote za ajira yangu nikatakiwa niisaini Kwa mkono then Nii submit na nimefanya hivo pia,,form hiyo imeelekeza natakiwa kuwa na visa ya kusafiria ndani ya siku 14 kabla hawajanitumia ticket ya Ndege kwenda kuanza kazi mnamo mwezi wa pili mwishoni na aina ya kazi ni ya mkataba wa miaka mitatu.

Hivo basi kabla sijaanza harakati za kutafuta passport na visa imebidi nipite Hulu mnishauri kitu Kwa kuwa kuna ndugu mmoja kashanitia wasiwasi ya kwamba hawa ni matapeli wakati huo mimi niliomba kazi kupitia official website yao ya shell.

Nimeenda ubalozi wa UK mchana huu nikaambiwa nifatilie na kujidhihirisha juu ya hii kazi na kitu kibaya zaidi aliyenijibu hivi ni mlinzi Kwa kuwa kasema kuna wengine wameenda kuulizia ila wamejibiwa wapitie mtandaoni wajidhihirishe kwanza hivo kutokana na majibu hayo wamenipunguzia asilimia na ari ya kupambana.

Naomba Kwa ambaye ashawahi kuomba kazi Kwa hawa watu wa Shell Oil Exploration and production UK anipe ushuhuda kabla sijaanza kupambania passport na visa.Jamani naombeni ushauri na maelezo zaidi,,soko la ajira ni gumu Sana Kwa sasa tanzania
#asanteni
Nimeweka barua niliyotumiwa hapo chini
Screenshot_20220113-114117.jpg
Screenshot_20220113-114121.jpg
 
Pole sana mkuu.
Naomba nikukatishie furaha yako na nikwambie wazi kuwa hao ni MATAPELI.

Proof:

Recent incidents have occurred involving organisations falsely claiming to recruit on behalf of Shell. These organisations, claiming to either work for or be affiliated with Shell, notify individuals that their qualifications were found suitable to work as an employee (local or expatriate) for Shell and solicit the transfer of significant sums of money to pay for work permits, insurance policies, etc.

Please note that Shell does not (nor do any of the organisations that recruit on our behalf) ever ask for money or payments from applicants at any point in the recruitment process. All individuals who are successful in gaining an offer of employment from Shell, whether directly or indirectly, are always required to go through a formal recruitment process.

Please note that these communications are fraudulent. They do not originate from Shell nor are they associated with Shell's recruitment process.

Salient points of such communications are that they come from non-Shell e-mail addresses (e.g. from a yahoo.com address); the use of English is poor; and at some stage money is requested.

We recommend that you do not respond to unsolicited business propositions and/or offers from people with whom you are unfamiliar. Do not disclose your personal or financial details to anyone you do not know. If you receive such proposals, we would advise you to contact your local police station and provide them with all information you may have from the senders (email addresses, phone/fax details, etc.).
 
mimi wameniambia kuwa niwatumie dolla elfu 2, nikatuma kumbe ni mataperi ilikuwa mwaka jana mwezi wa 3, nililia mpaka nikazilai sina hamu nao kabisa hao
 
Nimekuwa na google Kila taarifa walionitumia naona haipo na haihusian na hii kampuni ya shell,,Hadi Sasa nimeshapata majibu,,asanteni sana ndugu zangu
 
mimi wameniambia kuwa niwatumie dolla elfu 2, nikatuma kumbe ni mataperi ilikuwa mwaka jana mwezi wa 3, nililia mpaka nikazilai sina hamu nao kabisa hao
Dollar elfu 2 na ukatuma?
Una elimu ya kiwango gani mkuu?
 
mimi wameniambia kuwa niwatumie dolla elfu 2, nikatuma kumbe ni mataperi ilikuwa mwaka jana mwezi wa 3, nililia mpaka nikazilai sina hamu nao kabisa hao
Mkuu unatuma za Nini. Waambie kuwa nikishapata kazi mtanikata.
Pia hao wazungu huwa hawanaga njaa huwa wanahitaji mtu pure na sio mbabaishaji. Hawana njaa Kama huku kwetu ama umasikini.ukiwa na cheo unao ndugu wengi so yabidi uwashike mkono
 
Back
Top Bottom