Posho City
JF-Expert Member
- Mar 15, 2012
- 646
- 415
Mimi ni mwalimu by profession,nilihitimu stashahada ya ualimu 2007 nkaajiriwa wilaya ya Bukoba mjni.2009 kaenda bachelor ya adult education and community development(Bed Adec),pale Udom na nimehitimu 2012.Lakini niliporudi kazini afisa elimu akawa ananituhumu eti mie nilihusika kusambaza meseji za kuhimiza mgomo wa walimu wa mwezi wa8,2012.Na maajabu kipindi mgomo unaendelea alikuja shuleni kwangu akakuta sipo,akanipigia simu na kunieleza kuwa sitasimamia sensa,nkamjibu sawa.Baada ya hapo ukizingatia serikalini maslahi kidogo nilihamua kuja Dar nkatafuta private na wananilipa fresh,lakini nataka baada ya miaka angalau minne nirudi serikalini.Tangu desemba 2012 amenifungia na mshahara,Je kusudi baada ya muda huo nirudi serikalini inabidi nifanyeje?Naajiriwa upya au narudi kule wilayani nakiri kuwa mtoro kazini?