Naomba nishaurini kuna mapenzi hapa

Naomba nishaurini kuna mapenzi hapa

mapengo junior

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2011
Posts
1,135
Reaction score
276
Habari wana MMU.

Kijana mwenzenu yananisibu haya.

Nina mpenzi wangu ikifika october 24 tunatimiza mwaka mmoja, ila kuna kitu nashindwa kumuelewa, wakati tunaanza mahusiano alikuwa hamalizi wiki moja anakuja home kwetu.

Siku zilivyozidi kwenda akapunguza kuja kwetu nikimuuliza anasema eti anaona aibu watamchoka home, mimi nikamwambia wakikuchoka, mimi c wao akasema haya atabadilika.

Baadae akarudia tena sasa imekuwa kubwa kuliko yaani tangia tuonane tar 28.04.2014 mpaka leo hatuja onana tunaongea kwa simu na msg tuu.

Nikimuuliza majibu hana, anasema hata yeye anashangaa eti hajui kwa nini hatuonani, cha kushangaza anadai eti ananipenda na anataka niwe mumewe mungu akipenda.

Ila me naona haoneshi ukweli kwa hayo maneno anayosema.

Je ni kweli wapenzi mnaweza mkakaa zaidi ya miezi 3 msionane tena hapahapa dar?

Kama inawezekana hivi sababu inaweza ikawa nini?

kama haiwezekani je kuna mapenzi ya kweli hapa?


Pliiz toa ushauri kama unaona umeguswa si vema kutukana.

Nawasilisha.
 
Since issue ni kuja kwenu have you tried meeting her some place else apart from your home ? If nay then try that before jumping into conclusion of any sort.
 
Hivi haya ni mambo ya kuuliza kwenye mtandao kweli..?!!
 
Unamuita kwenu au kwako?
wewe ukweni ni mahali pa kuheshimu sio kwenda kwenda tu kama unaingia msalanani
hata ingekuwa ndo mie unaniita kwenu siji ng'oooo!!!!
 
Hivi haya ni mambo ya kuuliza kwenye mtandao kweli..?!!

Teh tutafanyaje sasa na sisi ni product za mitandao?
ngoja tuulize tu tukkosa kujibiwa tuna google.....
 

Attachments

  • image.jpg
    image.jpg
    16.5 KB · Views: 430
Huu muda unaopoteza kwa kutozingatia shule utakuja kuujutia sana.
kama unataka uzinzi mwite hotel malizeni mambo yenu huko, ungekuwa na kwako angekuja wanawake wanahitaji uhuru full kujiachia. unadhani waliopanga magetto yao hawana kwao?
 
Hiyo miezi 3 wewe umefanya juhudi gani muonane. Na ni lazima muonane nyumbani kwenu? Nafikiri amekuona hujitambui ndo maana anakupa kisogo. Dogo be active and creative. Otherwise utaishia kulilia lia tu
 
Alie juu mgoje chini kama hashuki mpandilie huko huko. Mtoto wa siku hizi mnakosa maadili kabisa mwanaume hajakuoa unataka aje kwenu kufanya nini???
 
Utoto unakusumbua. Binti mnaanza tu uhusiano unaenda kum-parade home! Tena alivyo na akili akakwambia wasije wakamchoka, we huoni tatizo. Give her some respect.

By the way, huyo binti ashapata mwanaume mwenye akili zake. Siku nyingine, tafuta sehemu za kukutania na mpenzi wako.
 
Jamani kila siku yeye ndo wakuja kwenu kiukweli inachosha.Hebu mtafutege sehemu nyingine uone kama atakataa kuja
 
Umemuoa me naona sababu yake ni ya msingi kwa kua haweza kuja kwenu daily kumbuka wataanza kumchoka mapema hata ukiia itaonekana hakuna.
Tofauti halafu wewe huko kwunu unampeleka girlwako ni ukosefu wa adabu.
Bora ingekua unaish mbali na.wazazi kwenu????? Sjui ila naona sababu yake ya msingi kuhus kutokuoana.had leo sasa hapo kaeni chini mkae mzungumze tena sio.kwenu mbali kabisaaaa uache hiyo
 
kuna mambo mawili yawezekana amechoka kuja kwenu au amekuchoka wewe
 
kwako au kwenu mmhh kama ni kwenu hata mim siji
 
Una uhakika dada zako hawajaanza maneno kisa kuja kwenu? why unakaa home? mwenyewe nisingekuja kabisaaa. be creative acha u baby mama.
 
Kiukwel inachosha sana kila siku wewe ndo uwe unamfuta mtu yeye kuja hapana na wanaume wengine wanakaa kwenye getto zao bas kila siku we ndo kiguu na njia km una akili timamuu lazima ujistukie...uyo dada ana akili kastuka sasa wewe mtoto wa watu aje kwenu tena kwa baba na mama jiongezeeee...try to get her out some days
 
Back
Top Bottom