Naomba msaada, nakaribia kuhitimu chuo nahitaji kazi

Naomba msaada, nakaribia kuhitimu chuo nahitaji kazi

tax compliant

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2016
Posts
1,211
Reaction score
1,200
Ni matumaini yangu kuwa nyote mu wazima kabisa.

mimi ni kijana wa miaka 23 na pia ni mhitimu mtarajiwa katika chuo cha usismamizi wa fedha (IFM) (2016), namshukuru Mungu kwa afya njema aliyonijalia kwani imenisaidia kufanya vibarua vya hapa na pale na kuendelea kuishi, lengo kuu la kuja hapa jukwaani na kuomba msaada wenu ni hali yangu ya sasa. hali yangu ya kiuchumi ni mbaya sana lakini pia natamani sana kupata fursa ya kuendeleza career yangu,

pamoja na kujaaliwa afya njema kiasi cha kumudu kufanya kibarua chochote imekua vigumu sana hata kupata kibarua ingawa natafuta kila siku iendayo kwa Mungu tena kwa bidii sana. Naweza kufanya kazi yoyote wakuu ilimradi ni kazi halali, kwa sababu nahitaji pia kupata uzoefu ntashukuru sana hata nikipata nafasi ya kujitolea bila malipo yoyote (internship au volunteering),

pia ninaweza kuisaidia organization kwenye masuala mazima ya kodi na pia uhasibu kwani nimesomea usimamizi wa kodi (bachelor in taxation) na nimefaulu vizuri (4.0 GPA) na nimefanya kazi hiyo na mamlaka husika (TRA) kwa kipindi cha miezi mitatu kama assistant tax officer.

Wakuu nina mambo mengi sana ya kuandika na pengine naweza kuishia kuwachosha, naombeni kwa yeyote anayeweza kunisaidia kwa namna moja au nyingine ani-PM ili tuwasiliane zaidi. Natanguliza shukrani.
"FEAR GOD AND WORK HARD"

mamlaka husika (TRA) hivyo nina uzoefu pia
 
Pole tax mwenzangu hii coz n ya kidosho sana Mara wanasema mtu wa tax huwezi kuwa mhasibu kiukweli najutaga sana kusoma tax
 
Acha Uoga DOGO, hata bado haujagraduate unaweweseka, Watu tuna 5 years mtaani mpaka tumekuwa sugu, kila mtu amezaliwa na bahati yake, VUTA PUMZI, KAZA BUTI UTAPATA AJIRA sooner or Later.......
 
Acha Uoga DOGO, hata bado haujagraduate unaweweseka, Watu tuna 5 years mtaani mpaka tumekuwa sugu, kila mtu amezaliwa na bahati yake, VUTA PUMZI, KAZA BUTI UTAPATA AJIRA sooner or Later.......

Asante kwa ushauri
 
Kiongozi,, una nia njema kabisa katika kufikia malengo yako ya maisha,, ila changamoto ya kazi ni kubwa sana,, wakati unaendelea kutafuta ajira,, pia endelea kuwekeza mind yako kwenye ujasiriamalio,, fikiria ni fursa gani unaweza Kuifanya na ikakuingizia kipato,,,
 
Kiongozi,, una nia njema kabisa katika kufikia malengo yako ya maisha,, ila changamoto ya kazi ni kubwa sana,, wakati unaendelea kutafuta ajira,, pia endelea kuwekeza mind yako kwenye ujasiriamalio,, fikiria ni fursa gani unaweza Kuifanya na ikakuingizia kipato,,,

Ushauri murua kabisa, nitaufanyia kazi mkuu. Shukrani sana
 
Acha Uoga DOGO, hata bado haujagraduate unaweweseka, Watu tuna 5 years mtaani mpaka tumekuwa sugu, kila mtu amezaliwa na bahati yake, VUTA PUMZI, KAZA BUTI UTAPATA AJIRA sooner or Later.......
Nimeamua leo kuangalia nyuma na hatimaye yametimia. Mungu mkubwa.
 
Ni matumaini yangu kuwa nyote mu wazima kabisa.

mimi ni kijana wa miaka 23 na pia ni mhitimu mtarajiwa katika chuo cha usismamizi wa fedha (IFM) (2016), namshukuru Mungu kwa afya njema aliyonijalia kwani imenisaidia kufanya vibarua vya hapa na pale na kuendelea kuishi, lengo kuu la kuja hapa jukwaani na kuomba msaada wenu ni hali yangu ya sasa. hali yangu ya kiuchumi ni mbaya sana lakini pia natamani sana kupata fursa ya kuendeleza career yangu,

pamoja na kujaaliwa afya njema kiasi cha kumudu kufanya kibarua chochote imekua vigumu sana hata kupata kibarua ingawa natafuta kila siku iendayo kwa Mungu tena kwa bidii sana. Naweza kufanya kazi yoyote wakuu ilimradi ni kazi halali, kwa sababu nahitaji pia kupata uzoefu ntashukuru sana hata nikipata nafasi ya kujitolea bila malipo yoyote (internship au volunteering),

pia ninaweza kuisaidia organization kwenye masuala mazima ya kodi na pia uhasibu kwani nimesomea usimamizi wa kodi (bachelor in taxation) na nimefaulu vizuri (4.0 GPA) na nimefanya kazi hiyo na mamlaka husika (TRA) kwa kipindi cha miezi mitatu kama assistant tax officer.

Wakuu nina mambo mengi sana ya kuandika na pengine naweza kuishia kuwachosha, naombeni kwa yeyote anayeweza kunisaidia kwa namna moja au nyingine ani-PM ili tuwasiliane zaidi. Natanguliza shukrani.
"FEAR GOD AND WORK HARD"

mamlaka husika (TRA) hivyo nina uzoefu pia
Wewe si ulikuwa una kebehi wenzako wanaoulizia majibu ya usaili TRA? Na kujigamba kuwa uko kwenye jopo ndo mnachambua majina? Acha mbwembwe kijana.
 
Wewe si ulimtu a una kebehi wenzako wanaoulizia majibu ya usaili TRA? Na kujigamba kuwa uko kwenye jopo ndo mnachambua majina? Acha mbwembwe kijana.
Mmmh mkuu umenifananisha, sijawahi na sintokuja kumkebehi mtu pitia vizuri mafaili yako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom