Mnajichanganya tu, ni vema uishi unavyoweza au unavyoona wewe ni sawa. Mke au mume anaweza kukuletea majanga makubwa hujawahi kuona na ukajuta maisha yako yote.
Mume /mke anaweza kukuletea aibu kubwa kwenye hiyohiyo jamii ambayo itakuambia ukioa utaheshimika na ukadharaulika maisha yako yote. Usishangae ukamtunza mke ukaja kusikia anatembea na bodaboda anayekujaga anamtuma nyumbani.
Usishangae ukasikia mume anatembea na dada wa kazi uliyemtoa kijijini aje kuwasaidia kazi. Au akatembea na mdogo wako wa damu uliyemleta kumsomesha hapa mjini.(I've seen this tena mdogo mtu kasomeshwa Hadi chuo kikuu na akamnyang'anya mine dada mtu mpaka leo ni ugomvi hawakutani kijijini mmoja akienda mwingine haendi mpaka huyo aondoke )
Kama unaoa we la tu just kwa Nia ya kwamba umepata mwenza na mnataka kujenga maisha pamoja ikiwemo familia kwamba mtalea watoto pamoja Ila isiwe kwamba jamii itakuona umestaarabika au kwamba kipimo Cha akili ndoa haina hayo Kama ndoa ni akili akina Bill Gates na Jeff bezos angekuwa kwenye ndoa mpaka leo.
Hizi ndoa ndio unasikia chanzo Cha kifo, chanzo cha umasikini, pia chanzo cha mifarakano mikubwa sana. Sasa usikimbilie mdoa Kama huiwezi ndoa.
Sio lazima wote kuwa kwenye ndoa, sio kila mtu alipangiwa kuwa na ndoa just sikiliza moyo wako unataka nini? Pia haya mambo ni bahati tu jinsi maisha yalivyobadilika binadamu amekuwa wa tofauti imani ya sasa na zamani ni tofauti.
Mwanamke wa Sasa sio yule wa miaka ya 60-80 same as men are. Elimu, utandawazi, lifestyle, ukuaji wa miji, population, migration na mambo kadhaa wa kadha yamechangia tradition, customs, Norma kubadilika na kupelekwa hata mahusiano kubadilika.
Mahitaji ya mwanamke wa Sasa kwenye ndoa sio mahitaji ya mwanamke wa miaka ya zamani. Sasa hivi mwingine anakuja anataka watoto tu akipata humbabaishi anasepa.
Mwingine anakuja anataka security financial etc akichuma anasepa humbabaishi hata kidogo uvumilivu umekuwa chungu siku hizi hakuna kijana wa kike au wa kiume anaweza kutumia busara ya umilivu . Wenyewe wanaamini ukivumilia ni ujinga lakini hatuangalii ndoa kwa mapana yake na hatusemi uvumilie tu hata kama Kuna hatari ya kuuwawa au kujeruhiwa Ila uvumilivu wa kawaida ambapo hata ukienda kwa binadamu mwingine itabidi umvumilie sababu atakukera tu.
Wengi wameingia kwenye ndoa kwa sababu ya umri , social status, kasumba, ujinga nk.
Ndoa sio kufuliwa, kuogeshwa, kupewa hela, kununuliwa gari , kupata uroda wa bure nk. It's more than that. Ni watu ambao tumeshaoa ndio tunaweza kuelewa ndoa ni kitu gani Ila ni ngumu kwa ambaye hajaoa kuelewa hata kidogo Ila aliyeko kwenye ndoa ananielewa haihitaji kuongea sana anaelewa tu ndoa.
Ndoa ni zaidi ya hayo, ni karaha, ni raha ,huzuni, mateso, manung'uniko, mapenzi, kusaidiana, kutesana, kuchukuliana, kununiama, kuchekeshana, kujibalaguza, kujinafikisha wakati mwingine, kujibebisha, uongo, ukweli Yani kila kitu kipo kwenye ndoa it's just a package ambayo utabahatika kuipata ipi basi itakufanya ubaki na ndoa au uiache.
So, usidhani ndoa ni lelemama kwamba is about kuzaa, kulana, etc, jiulize wewe binafsi unaitaka ndoa???