Naogopa kumwumiza ushauri please

Naogopa kumwumiza ushauri please

Mlanje

Senior Member
Joined
May 16, 2013
Posts
141
Reaction score
77
Helo ndugu zangu wanajamii, najua tunaendelea na maisha vizuri.

Mimi ni mwanaume wa miaka 29 niliachana na mpenzi wangu mwaka jana so baada ya muda mrefu kuwa mpweke nilianzisha urafiki na dada mmoja aliyeniambia anafanya kazi kwenye supermarket moja hapa mjini. Baadae nilimtongoza na akakubaliana nami so nikaona vyema na pia yeye anadai hajawahi kulala na mwanaume.

Wiki iliyopita nimegundua kuwa amemaliza form four mwaka jana na ana miaka 18 vitu ambavyo sikujua hapo awali,kiukweli naona nimemzidi sana umri(miaka 11) na pia sihitaji kusubiria amalize mambo yake ya shule maana nafikiria kuoa mapema. Yeye anadai ananipenda sana yaani usiku akipiga simu akakuta inatumika basi analia sana na pia sitaki kumtoa hiyo bikira yake maana najiona sisitahili hiyo heshima bali mtu mwenye mapenzi ya dhati kwake.

Naombeni ushauri wenu jinsi ya kumwambia kwani sifikirii kuwa nae kwanza ni mdogo sana kiumri na pia siwezi kumsubiri amalize shule

Samahani kwa uandishi usio mzuri.
 
hongera kijana na ubarikiwe ... huyo binti mwambie ukweli tu mapema itamuuma ila inambidi akubaliane na uwamuzi wako ....... ila kama ukiendelea nae akili yake bado aijamature vizuri kwa kweli
 
Safi sana wacha niende kafe nikakupe LIKE !! Kwanza ntarudi kwa ushauri.
 
Hongera kwa kuwa muungwana.

Huyo wa kulia lia kwasababu ya simu kuwa busy tu inabidi umuache kwa akili maana anaweza hata akajiumiza ukimwambia humtaki. Mkalishe chini umsisitizie sana swala la kusoma. Mwambie we upo tu huendi popote ye asome alafu mambo mengine baadae. Usijamiiane nae, kama huwa mnaonana mara kwa mara punguza (jifanye uko busy),mapenzi yenu yawe ya simu zaidi huku ukipunguza mawasiliano taratibu.
 
Hongera kwa kuwa muungwana.

Huyo wa kulia lia kwasababu ya simu kuwa busy tu inabidi umuache kwa akili maana anaweza hata akajiumiza ukimwambia humtaki. Mkalishe chini umsisitizie sana swala la kusoma. Mwambie we upo tu huendi popote ye asome alafu mambo mengine baadae. Usijamiiane nae, kama huwa mnaonana mara kwa mara punguza (jifanye uko busy),mapenzi yenu yawe ya simu zaidi huku ukipunguza mawasiliano taratibu.

mkuu Lizzy umesomeka vyema, na nyongeza ndogo hapo juu ingekuwa vyema kama ungetafutwa utaratibu wa huyu mdogo wetu wa miaka 18 akaenda kusoma mbali kidogo na mji anaoishi sasa, lengo ikiwa ni kupunguza mawasiliano na hatimaye kufa kabisa (fimbo ya mbali haiui nyoka), lakini pamoja na hili msisitizo wa kusoma uwe juu zaidi manake ukimkwepa haraka sana anaweza poteza dira afu akanaswa na wale wasio waungwana..
 
Mwenyezi mungu akuzidishie kila lenye kheir na wewe na akupe watoto wenye hekma kama zako,inshallah utampata mwenye kheir na wewe awe mkeo muishi kwa amani na masikizano.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom