neha mimi
JF-Expert Member
- Aug 19, 2014
- 344
- 152
Habar zenu wapendwa, jamani mimi kuna jambo lanitatiza ni kuhusu hii ndoa ambayo naishuhudia kutetereka kwake kama sio kufa kabisa ni hivi; miaka kadhaa iliyopita walifunga ndoa lakini mume na mke wakawa wanaishi mikoa tofauti ni kutokana na kazi zao lakini baadae mume akamshuri mke wake atafute uhamisho ili amfuate mumewe mwanamke akakataa.
Basi maisha yakawa yanaendelea kama kawaida lakini kumbuka mwanamke anaishi kwao hivyo mumewe akirudi likizo afikie ukweni then aende lodge kulala na mkewe na sio kwamba alikuwa hana pa kuishi la hasha mke alipangishiwa nyumba nzima eti kodi ilipoisha akarudi tena kwao eti hataki kukaa mwenyewe ana mtoto na msichana wa kazi.
Basi bwana baada ya mda kwenda sana na watu kumshauri sana ndo mwanamke akaamua kutafuta uhamisho ili amfuate mumewe tena bila kumwambia kibali kilivyokamilika ndo akamwambia mimi nakuja huko sasa basi mume kamwambia asiende coz na yeye anakaribia kuhama mke ashapata uhamisho wa mkoa huo wakati mume anakaribia kuhama sasa hapo ndo mke anahaha ile mbaya anawaza labda mumewe ana mke mwingine ndo mana hataki aende.
Hivi hapo nani wa kulaumiwa jamani manake mwanamke analalamika anaona kaonewa na ni mkorofi huyo, ushauri pliiz kuokoa hii ndoa changa.
Basi maisha yakawa yanaendelea kama kawaida lakini kumbuka mwanamke anaishi kwao hivyo mumewe akirudi likizo afikie ukweni then aende lodge kulala na mkewe na sio kwamba alikuwa hana pa kuishi la hasha mke alipangishiwa nyumba nzima eti kodi ilipoisha akarudi tena kwao eti hataki kukaa mwenyewe ana mtoto na msichana wa kazi.
Basi bwana baada ya mda kwenda sana na watu kumshauri sana ndo mwanamke akaamua kutafuta uhamisho ili amfuate mumewe tena bila kumwambia kibali kilivyokamilika ndo akamwambia mimi nakuja huko sasa basi mume kamwambia asiende coz na yeye anakaribia kuhama mke ashapata uhamisho wa mkoa huo wakati mume anakaribia kuhama sasa hapo ndo mke anahaha ile mbaya anawaza labda mumewe ana mke mwingine ndo mana hataki aende.
Hivi hapo nani wa kulaumiwa jamani manake mwanamke analalamika anaona kaonewa na ni mkorofi huyo, ushauri pliiz kuokoa hii ndoa changa.